• Wimbo maalum kwa ajili ya kumpa heshima Mt. Yosefu. Ni wa kusikiliza (Audio), kutafakari, na kuomba ulinzi wa Mt. Yosefu. Furahia kazi ya sanaa kutoka kwa Wanakwaya wa Kwaya ya Damu Takatifu ya Yesu, Tegeta, Dar es Salaam, Tanzania.

  • Na Vincent Mpepo

    Makamu Mkuu wa chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Profesa Alex Makulilo amewataka wafanyakazi wa chuo hicho kubadilika kifikra na kiutendaji ili kuendana na ushindani katika mifumo ya uendeshaji taasisi za elimu ya juu kutoka ndani na nje ya nchi.

    Profesa Makulilo alitoa wito huo jana wakati wa mkutano wake wa kwanza na wafanyakazi wa chuo hicho akihudumu kwa nafasi hiyo mara baada ya uteuzi wake mapema Mwezi Juni, 2025.

    Alisema sura ya elimu ya juu hivi sasa imebadilika sana na kwamba kwa kuangalia mwenendo wanaweza kuelewa kinachoendelea huku mabadiliko hayo yakiathiri soko la chuo hicho.

    “Idadi ya vyuo vikuu na vyuo vikuu huria imeongezeka kwenye nchi ambazo hazikuwa navyo”, alisema Profesa Makulilo.

    Alisema idadi ya wanafunzi wa kimataifa kutoka nje ya nchi imepungua akitolea mfano wa idadi ya wanafunzi wa uzamili kutoka Kenya kwa mwaka wa masomo wa 2022/2023.

    “Takwimu zinaonesha idadi ya wanafunzi wa uzamili kutoka Kenya imepungua kutoka wanane (08) hadi sita (06) maana yake ushindani umeongezeka”, alisema Profesa Makulilo.

    Aidha alizungumzia ushindani kutoka ndani ambao umetokana na vyuo vikuu vingine hapa nchini kutoka kwenye mfumo wa mazoea wa madarasa na kuingia kwenye mfumo wa elimu huria na masafa yaani (ODL).

    “Wengine wameenda mbele zaidi na kuanza kujenga vituo vya mikoa na wanaviita majina kama kampasi za kilimo, elimu bahari au madini na kadhalika”, alisema Profesa Makulilo.

    Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Josiah Katani aliwakumbusha wafanyakazi wa chuo hicho taratibu za utumishi wa umma ikiwemo kuwahi kazini, kuomba ruhusa wanapokuwa safari au kukumbwa na changamoto yoyote.

    “Barua zinazoenda uongozi wa juu lazima zipitishwe kwa msimamizi wako wa kazi”, alisema Profesa Katani.

    Aliwaasa watumishi kuomba likizo kwa kutumia mfumo, kuhakiki taarifa zao na waende likizo kwa tarehe walizojaza kwenye kwenye mfumo na ikitokea kuna mabadiliko ni lazima wapate kibali kwa uongozi.

    Profesa Katani aliwakumbusha  wafanyakazi wa chuo hicho kujaza kujaza kwa wakati majukumu yao katika mfumo wa usimamizi wa utendaji kazi katika utumishi wa umma yaani (PEPMIS)ili kuondokana na adha ya kutopanda vyeo.

    “Alama za chini kabisa kwa mfanyakazi ni 75%”, alisema Profesa Katani.

    Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Taaluma, Utafiti wa Ushauri wa Kitaalamu, Profesa Saganga Kapaya aliezea maendeleo ya uhuishaji na utengenezaji wa mitaala na kubainisha kuwa zoezi hilo linaendelea vizuri.

    Alisema idadi ya mitaala ya programu katika shahada za awali, uzamili na uzamivu zilizowasilishwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania ni 109 baada ya kupitishwa kwenye kamati za maamuzi za juu za chuo hicho.

    Aidha aliwataka wafanyakazi wa chuo hicho kuboresha huduma kwa mteja ili kutoa huduma nzuri zitakazowafanya wanafaunzi waliodahiliwa kuendelea na masomo chuoni hapo badala ya kuhama au kuacha.

    Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za. Elimu ya Juu Tanzania tawi la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Salatiel Chaula akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wa chuo hicho alisema wamepokea maelekezo wapo tayari kwa utekelezaji  ili kusukuma mbele gurudumu la taasisi hiyo.

  • Na Mwandishi Wetu

    Mtangazaji mstaafu wa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Edda Sanga, ameelezea kukerwa na utangazaji wa mzaha na ucheshi unaovunja miiko ya tasnia hiyo kwa kuwa madai kuwa studio ni eneo la kuheshimiwa sio kupiga kelele au kurushiana maneno.

    Sanga alitoa kauli hiyo jana wakati wa mafunzo kwa watangazaji chipukizi kutoka vyuo vya kati, yaliyoandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 74 ya utangazaji Tanzania.

    Alisema heshima ya utangazaji imepungua kwa sababu baadhi ya walipewa nafasi za utangazaji hawana wala maadili jambo linalosababisha wasikilizaji kuacha kufuatilia vipindi na maudhui kwa ujumla.

    “Studio ni eneo la heshima, utangazaji sio kupiga kelele wala eneo lakurushiana maneno,” alisema Sanga.

    Akizungumzia eneo la uandaaji wa maudhui katika vipindi vya mahojiano, Sanga alisema lina udhaifu mkubwa kwa sababu baadhi ya waandishi wa habari hususani wa kizazi kipya,hawajiandai wanapotaka kufanya mahojiano na kuzalisha maudhui ambayo hailengi kuisaidia jamii.

    Alisema suala la waandishi wa habari kushindwa kuwatafuta watu mahususi ambao ni vyanzo vya kuaminika kuzungumzia mada badala yake huwatumia wale wanaopatikana mara kwa mara na kushauri kuwatafuta watu wenye weledi na maarifa ya kuzunngumza mada husika.

    “Eneo la mahojiano bado lina changamoto kwa baadhi ya waandishi hawajiandai ipasavyo, wala hawatafuti watu sahihi wenye ujuzi wa kuzungumzia mada husika hivyo kuathiri ubora wa taarifa zinazozalishwa,” alisema Bi Edda.

    Katika mafunzo hayo, washiriki walijadili kuhusu hali ya kizazi kipya katika kulinda maadili ya kitaifa na uzalendo ambapo wazungumzaji walieleza hofu yao juu ya kupotea kwa misingi ya mshikamano wa kijamii kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia.

    Balozi Christopher Liundi, alisema kukosekana kwa uzalendo miongoni mwa vijana kunachangiwa na kutopatiwa elimu mapema kuhusu umuhimu wa suala hilo,pamoja na athari zamatumizi ya simu na mitandao ya kijamii.

    “Siku hizi rafiki mkubwa wa watu amekuwa ni simu hakuna tena upendo wa kweli wala urafiki wa dhati kama zamani, watu hawatembeleani, hawatafutani tena kama enzi zetu,” alisema Balozi Liundi.

    Alisema redio na vyombo vya habari kwa ujumla vina nafasi kubwa ya kusaidia kurejesha maadili ya kijamii, lakini hilo linawezekana tu endapo watangazaji na waandishi wa habari watafanya kazi zao kwa kuzingatia weledi, maadili na dhamira ya kuelimisha jamii.

    Debora Mwenda ni miongoni mwa waandishi wakongwe tangu uhuru alisema anakerwa na baadhi ya matamshi ya baadhi ya watangazaji wa kisasa ambao hushindwa kutamka majina ya nchi ikiwemo Tanzania na miji mingine mikubwa duniani.

    Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Watangazaji Wakongwe wa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Judica Losai alisema kutokana na kukua kwa teknolojia kunahitajika kuandaliwa vipindi au maudhui inayotumia dakika chache ikiwa na ubora unaotakiwa ili kumvutia msikilizaji.

  • Na Vincent Mpepo

    Watangazaji wakongwe wa iliyokuwa Redio Tanzania Dar es salaam (RTD) ambayo kwa sasa ni sehemu ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wametumia siku ya maadhimisho ya miaka 74 ya utangazaji Tanzania kubalishana uzoefu na waandishi wa habari watangazaji chipukizi ili kuhakikisha wanarithisha amali njema katika tasnia ya hiyo.

    Wakizungumza wakati wa mafunzo ya siku moja yaliyofanyika jana katika Ukumbi wa Break Point Kijiji cha Makumbusho jijini Dar es salaam, wakongwe hao wamesema licha ya kukua kwa sayansi na teknolojia kunakoigusa tasnia ya habari hususani utangazaji misingi ya uandishi wa habari haijabadilika.

    Akifungua mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Chama cha Wakongwe wa Redio Tanzania Dar es salaam, Suleiman Kumchaya alisema madhumuni ya mafunzo hayo ni kubadishana mawazo na waandishi wa habari watangazaji kwa kuelezea uzoefu waliokuwa nao kwa miaka kadhaa kama sehemu ya mchango wao kwa tasnia ya habari.

    “Unapojali kazi yako siku zote utasikiliza na kufuatilia kinachoendelea katika tasnia yako”, alisema Kumchaya.

    Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya chama hicho, Balozi Mstaafu, Christopher Liundi alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa waandishi wa habari watangazaji kwa kuwa yatasaidia kurudisha taaluma hiyo katika misingi lakini imekuwa fursa nzuri ya pamoja kujadili changamoto na fursa zilizopo.

    Balozi Liundi alisema msingi wa taaluma ya uandishi wa habari umejikita katika kulinda maslahi ya umma kwa kuwa wafanyacho kila seku ni sehemu ya elimu waitowayo na hawana budi kujiongezea maarifa kila iitwapo leo na ndio maana hata miundo ya ajira na kiserikali inatambua suala hilo.

    “Uandishi wa habari ni taaluma yenye mifumo yenye viwango vya juu vinavyofahamika na kupimika hivyo ni muhimu kwa waandishi kuiheshimu kwa kufuata taratibu, kanuni na sharia ambazo kila mhusika atawajibika kwazo”, alisema Balozi Liundi.

    Alisema ni muhimu kwa waandishi watangazaji kuzingatia misingi ya taaluma hiyo inayowataka wawajibike kwa umma kwa uadilifu unaozingatia usahihi, umahiri na weledi katika kazi zao.

    Makamu Mwenyekiti wa Wakongwe RTD, Jacob Tesha alizungumzia changamoto ya maudhui ya vyombo vya habari kutoka nje yanayotumiwa na baadhi ya vyombo vya habari na athari zake katika utamaduni wetu na kuwataka waandishi wa habari wasomi kuzalisha vipindi vyenye asili ya kitanzania ili kulinda utamaduni wetu.

    Kwa upande wake Mkufunzi wa Masomo ya Habari na Mawasilinao ya Umma kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Bujo Ambosisye aliwashukuru wakongwe hao kwa kujali na kujitoa kwao kwa ajili ya waandishi wa habari chipukizi na kwamba ni mara ya pili kwake kukutana na wakongwe hao katika mafunzo hayo.

    ‘Niliwahi kukutana na baadhi ya wakongwe katika tasnia ya habari miaka kadhaa ilyopita wakati wa maazimisho ya wiki ya ukombozi wa bara Afrika na kimsingi tunanafaika sana na uwepo wenu”, alisema Ambosisye.

    Katika mafunzo hayo mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo misingi ya uandishi wa habari za redio, uandishi wa habari za redio kabla na baada ya maendeleo ya teknolojia, changamoto katika kipindi kisichokuwa cha uchaguzi na kipindi cha uchaguzi.

  • Na Vincent Mpepo

    Wanawake walio kwenye ndoa wametakiwa kuwasaidia waume zao katika majukumu ya kifamilia kwa kufanya kazi badala ya kuwa wategemezi na walalamishi ili kuwapunguzia msongo wa mawazo na vifo waume zao.

    Kauli hiyo imetolewa jana na Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania (KKKT), Ismail Mwipile wa Usharika wa Segerea jijini Dar es salaam wakati wa mahubiri ya ibada ya ndoa ambapo Mfanyakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Stewart Kaberege alifunga pingu za masiha na Bi Suzana Kweka.

    Alisema kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la wajane linatokana na changamoto za ndoa ambazo kwa kiasi fulani zinasababisha na msongo wa mawazo kwa wanaume kutokana na kuzidiwa kimawazo, majukumu na wakati mwingine kutopata msaada kutoka kwa wake zao.

    “Niwakumbushe wanawake mlio kwenye ndoa kuwatii, kuwaheshimu na kuwasaidia waume zenu majukumu ili mzeeke pamoja”, alisema Mchungaji Mwipile.

    Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Profesa Alex Makulilo ambaye aliongoza wafanyakazi wa chuo hicho katika hafla za sherehe ya ndoa ya Stewart Kaberege alisema ndoa si jambo lelemama kwani linahitaji wawili walioamua kuishi pamoja kuwa na akili za ziada.

    Aliwapongeza maharusi hao kwa hatua hiyo muhimu na kuwataka kuishi kwa kadiri ya maelekezo ya dini na Imani yao.

    Aidha aliwaasa kuzaa watoto wengi ili kuijaza dunia kama maandiko yanavyowataka wakristo kufanya hivyo.

    “Stewart na mkeo msijibane sana, nendeni mkazae kuijaza dunia”, alisema Profesa Makulilo

    Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi, Ntimi Kasumo aliwakaribisha wageni na kuwashukuru kwa michango yao ya hali na mali ambayo imesaidia kufanikisha hafla hiyo na kwamba alisimia 20 ya michango hiyo imewekwa kwenye akaunti ya maharusi hao kama zawadi.

    Uchunguzi uliofanywa na mwandishi umebaini kutokuwepo kwa umoja kati ya wafanyakazi wa chuo hicho husasani kati ya watumishi wanataaluma na waendeshaji kutokuwa na mizania katika matukio mengi ya kijamii.

  • Na Tabia Mchakama

    Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeshuhudia ulipwaji wa fidia kwa Bi. Bahati Ngowi kufuatia kufuatia kifo cha mume wake Profesa Ngowi aliyepata ajali ya gari maeneo ya Mlandizi Kibaha mkoani Pwani tarehe 28 Machi 2022.

    Akishuhudia tukio hilo Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware alizitaka kampuni za bima kuhakikisha zinalinda na kutetea haki za wateja wao wa bima wanapopatwa na majanga ili kuleta utulivu na ahueni kwa waathirika.

    Aidha alimshukuru Mhe. Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa kwa kumuelekeza mhanga huyo mahali sahihi lakini na kuipongeza kampuni ya bima ya Mayfair kwa kumpatia mama huyo fidia stahiki iliyoendana na janga bila ya usumbufu wowote.  

    “Ninawaalika watanzania kuja TIRA ikiwa mtakutana na changamoto yoyote ya kibima”, alisema Kamishna Dkt. Saqware.

    Kwa upande wake, mnufaika wa bima, Bi. Bahati Ngowi alisema TIRA imekuwa msaada mkubwa kwa sababu alianza kufuatilia madai hayo mahakamani mara baada ya ajali kutokea na mwaka 2025 alielekezwa kufika TIRA na Mhe. Waziri Mkuu wa Tanzania, Majaliwa Kasim Majaliwa.

    Kampuni ya bima ya Mayfair imemlipa Bi. Bahati Ngowi kiasi cha shilingi milioni mia moja na arobaini na tano (145,000,000).

  • Kwaya ya watoto wa shule ya Jumapili wakihudumu katika ibada SiKu ya Jumapili (picha na Vincent Mpepo).

    Na Vincent Mpepo

    Mtenda Kazi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Anna Mauki amewataka washarika wa kanisa hilo kuona fahari ya umoja wa makanisa yaliyoungana na kuwa kanisa moja kwa kuwa ndani yake kuna mafanikio mengi.

    Bi. Anna Mauki aliyasema hayo Siku ya Jumapili wakati wa mahubiri na kuwataka wakristo wa sasa kuona kuwa wana sehemu ya kufanya ili kuhakikisha historia ya kanisa hilo kwa miaka 62 ijayo inakuwa na kumbukumbu nzuri zaidi kwa wao kuhusika katika mambo mbalimbali.

    Alisema waasisi wa umoja huo walifanya vitu na maono yao ndiyo yanayoonesha mafanikio ya kanisa kwa sasa kupitia kazi, shughuli na huduma mbalimbali zilizopo akitaja baadhi kama hospitali, vyombo vya habari, shule za msingi na sekondari pamoja na vyuo vikuu ambavyo vinamilikiwa na kanisa na vina mchango kwa jamii.

    “Tupende kazi za umoja kwakuwa ni kazi za Mungu”, alkisema Bi.Mauki.

    Alisema kanisa liendelee kuwaandaa watoto kuja kuwa wakristo wawajibikaji siku zijazo na kwamba maanadalizi hayo huanzia katika ngazi ya familia.

    “Kanisa lina utaratibu mzuri wa kuwapokea watoto tangu wakiwa wadogo na limeendelea na programu mbalimbali katika makuzi yao mpaka utu uzima”, alisema Bi.Mauki.

     Alisema na bado familia ina wajibu mkubwa kuhakikisha inafuatilia makuzi na mwenendo wa mtoto ili awe mkristu mwajibikaji.

    Aidha aliwataka wakristo kuacha tabia ya kufuatilia mambo yasiyowahusu na badala yake wajikite katika yanayowahusu.

    Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi Mtaani hapo, Exaud Mchome alitoa taarifa ya maendelep ya ujenzi na kwamba kwa kwa wiki ile ujenzi haukuenda vizuri kutokana na mafundi wanaofanya kazi hiyo kutofikia viwango stahiki.

    Aliwashukuru washarika kwa kuendelea kujitoa kwa ajili ya kazi ya ujenzi unaoendelea kanisani hapo na kusisitiza ambao bado hawajakamilisha ahadi zao kwa awamu ya kwanza ya Januari hadi Juni kukamilisha ili kupisha zoezi la mavuno lililopo mbele.

    Wakati huo huo, Mwinjilsti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mnzava aliwashukuru wazazi waliowaruhusu vijana wao kushiriki Tamasha la Twenzetu kwa Yesu kwani licha ya kuwa ni mtoko ni sehemu ambayo imewapa mafunzo yatakayowasaidia kuikulia Imani.

    Aidha, aliwakumbusha washarika kuendelea kutoa sadaka ya mfuko wa elimu kwa kuwa ina majukumu ya kusaidia watoto wengi kupata elimu.

  • By Vincent Mpepo

    The Open University of Tanzania (OUT) has conducted training on awareness and understanding of Sign Language for its frontline administrative staff who interact directly with clients, including people with hearing impairments, with the goal of improving communication and service delivery.

    Speaking at the official opening of the training held recently in Dar es Salaam, the Deputy Vice Chancellor for Learning Technologies and Regional Services, Professor Leonard Fweja said the training is a significant step that demonstrates the university’s commitment to offering inclusive education services, emphasizing that information is the foundation of communication in society.

    “As we all know, our society comprises people facing various challenges, but there are always ways to overcome these challenges through communication,” said Prof. Fweja

    He added that communication facilitates the efficient delivery, provision of services and enhances cognitive functioning.

    Head of the Department of Linguistics and Literary Studies, Dr. Zelda Elisifa urged participants to continue practicing what they had learned to reinforce their understanding, warning that without continuous use, the knowledge would fade and the training would become ineffective.

    She said the university plans to integrate Sign Language interpretation into all services and programmes by June 2026.

    “To achieve this goal, our department prioritized secretaries and reception staff for this opportunity to acquire basic skills in Tanzanian Sign Language (TSL),” said Dr. Elisifa.

    A participant from the Directorate of Student Services, Mwanawetu Mbonde expressed appreciation to the department and the Faculty of Arts and Social Sciences for organizing and facilitating the training as the skills acquired would enhance their ability to serve clients from all groups, including the deaf community.

    Mbonde suggested that the training duration be extended and possibly conducted outside the regular work environment to allow participants to fully concentrate, as it was challenging for some to attend sessions while simultaneously handling office responsibilities.

    On her side, a staff member from the University Library Directorate,Khadija Katele recommended that the number of participants from her directorate be increased in future sessions, emphasizing that the library serves a broad user base, including people with hearing impairments.

    The two-day training was facilitated by Daud Gamba, Head of Deaf Section and Sign Language Interpretation at the University of Dar es Salaam’s Centre for Disability Services (CDS).

    The training aimed to achieve three core objectives: first, to deepen participants’ knowledge and understanding of deafness, Tanzanian Sign Language, and the essential communication needs of the deaf community.

    Another key objective was to equip participants with practical, everyday communication techniques for engaging effectively with deaf individuals, helping to minimize communication barriers within the OUT community and finally was to empower them with strategies to promote an inclusive and supportive environment for all forms of communication.