Wanafunzi wa Chuo cha Serikali za Mitaa Kampasi ya Shinyanga wametembelea Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga kuwaona wagonjwa, kufanya usafi eneo lote linalozunguka Hospitali hiyo, kujitolea damu na kutoa misaada mbalimbali za Kijamii.
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wangonjwa na wananchi mbalimbali wameeleza namna wanavyoridhishwa na uwepo wa Chuo cha Serikali za Mitaa Mkoani Shinyanga kwa kuwa uwepo wake unadhihirika katika mambo mbalimbali yanayohusu jamii.
Pamoja na mambo mengine, wanafunzi hao wamechanga pesa na kwenda kuziona jamii zenye uhitaji na hii ni katika kuonesha kuwa pamoja na kujipatia elimu kama sehemu ya jamii wanashiriki shughuli mbalimbali za kijamii.
Kwa upande wa Maneja Kampasi wa Chuo hicho Mkoani Shinyanga Dkt.John Kasubi amesema kuwa Chuo kitaendelea kujitolea kwa Jamii ya Shinyanga kila kinapopata fursa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo na kuwataka wananchi wakipe ushirikiano ili kuionesha Jamii kuwa mbali na utoaji wa elimu pia Chuo kinajitolea kuisaidia jamii inayokizunguka chuo hicho.
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, amemuagiza Mkandarasi Kampuni ya Afcons ya India kuzingatia maelekezo ya serikali kuhusu viwango vipya vya mishahara kwa wafanyakazi wa ngazi za chini, vinavyotaka kulipwa shilingi 16,500 kwa siku sawa na shilingi 515,000 kwa mwezi.
Agizo hilo amelitoa leo wakati wa ukaguzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika mji wa Kayanga, wilayani Karagwe, baada ya kubaini kuwa mkandarasi huyo anawalipa vibarua shilingi 12,500 kwa siku, kinyume na maelekezo ya serikali.
Alisema serikali ilielekeza viwango hivyo vipya vya mishahara kuanza kutumika Januari Mosi mwaka huu, na kusisitiza kuwa malipo hayo yaanze mara moja pamoja na kusainiwa kwa mikataba mipya inayoendana na mabadiliko hayo.
“Nakuelekeza kuwasilisha nakala za mikataba hiyo mipya katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kwa viongozi wa sekta ya maji katika mkoa husika”, alisema Kundo.
Sanjali na hilo, alionesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo, ambao awali ulipangwa kukamilika Desemba 2025 kabla ya kuongezewa muda hadi Septemba mwaka huu.
Kutokana na hali hiyo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na viongozi wa sekta ya maji mkoani kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini iwapo vifaa vya utekelezaji wa mradi vimeagizwa na kama mpango kazi uliopo unatekelezeka kwa muda uliopangwa.
Alisema Wizara ya Maji haitavumilia uzembe wa mkandarasi wakati wananchi wakiendelea kupata changamoto ya huduma ya maji safi na salama.
Mradi huo wa Maji wa Miji 28 wa Kayanga, unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 64.32 na unatarajiwa kuwanufaisha wakazi 352,790, na mpaka sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji.
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imekutana na kuzungumza na wananchi wa Mtaa wa Golani, Kata ya Kimara, Wilaya ya Ubungo kwa lengo la kutatua changamoto ya upatikanaji huduma ya maji katika mtaa huo.
Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Bi. Everlasting Lyaro amewatoa hofu wananchi wa Golani kwamba Mamlaka inatambua changamoto ya maji katika mtaa huo na zipo hatua za muda mfupi na mrefu ambazo zinachukuliwa ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana.
“Kwanza tuwaombe radhi wananchi wa hapa Golani kwa changamoto ya maji mnayoipitia, tunatambua maji ni haki ya kila mmoja wetu”, alisema Bi. Everlasting.
Alisema kwa kuanza Mamlaka italeta matenki Matano (05) yenye ujazo wa Lita 10,000 kila moja na kuyajaza maji yatakayouzwa kwa bei elekezi zoezi na zoezi hilo litafanyika kuanzia 15.01.2025 ili kukabiliana na changamoto hiyo kama hatua za awali ambazo ni za muda mfupi.
“Tutaratibu mgao wa maji katika eneo hili ambapo mtapata maji mara tatu kwa wiki, Alhamisi, Jumapili na Jumatatu”, alisema Bi. Evarlasting.
Akizungumzia utatuzi wa changamoto hiyo kwa mpango wa muda mrefu alisema DAWASA itajenga kituo cha kusukuma maji eneo la kwa Mama Stela kitakachosaidia maji kufika sehemu mbalimbali zilizookua hazipati huduma hiyo hapo awali.
Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa kihuduma DAWASA Kinyerezi, Mhandisi Antony Budaga alisema watumishi hawatakaa ofisi badala yake watatoka kuwafikia wananchi na kuhakikisha yaliyopangwa katika kikao hicho yanatekelezwa.
Mkazi wa Golani, Rajabu Said ameshukuru jitihada zinazofanyika kuhakikisha changamoto ya maji mtaani hapo inakwisha kwamba wananchi wanapata matumaini ya upatikanaji wa huduma ya maji amabayo itawaondolea kero ya ununuzi wa maji kwa watoa huduma binafsi inayowagharimu fedha nyingi.
Mwezeshaji kutoka Umoja wa Maabara Tanzania, Kezia Mbwambo akifafanua jambo kuhusu mifumo ya ubora kwa wataalam wa maabara kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye mafunzo yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam.
Na Okello Thomas
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imetoa mafunzo ya utekelezaji wa ISO/IEC 17025:2017 kwa wataalamu wa maabara ili kuongeza umahiri katika utendaji wa kila siku katika maabara.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko amesema Kiwango cha ISO/IEC 17025:2017 kinaipa maabara uwezo wa kuonesha umahiri katika kufanya uchunguzi na kutoa matokeo yanayotambulika na kukubalika kitaifa na kimataifa
“Utekelezaji wa kiwango hicho si hitaji la ithibati pekee, bali ni nyenzo muhimu ya kuimarisha ubora, uaminifu na ushindani wa huduma za maabara”, alisema Dkt. Mafumiko.
Alisema maabara kupata ithibati na kuitekeleza kwa vitendo yatatoa sifa njema si tu kwa mamlaka bali pia kwa taifa kwa ujumla.
“Nitumie fursa hii kusisitiza kwamba juhudi na uwajibikaji wenu ndiyo msingi wa mafanikio ya ithibati katika mamlaka”, alisema Dkt. Mafumiko.
Alisema mamlaka itaendelea kutoa rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa ubora ulioanzishwa kulingana na mahitaji ya viwango vya ubora wa kimataifa (ISO).
Mwezeshaji kutoka Umoja wa Maabara, Bi. Kezia Mbwambo alisema kuwa Kiwango cha ISO/IEC 17025:2017 ni mfumo wa usimamizi uliotengenezwa na Shirika la Viwango vya Kimataifa (ISO) linalolenga seti ya mahitaji ambayo taasisi au shirika linapaswa kufikia katika mfumo wa ubora ili kupata hati ya ISO.
Naye Riphat Lusingo ameishukuru mamlaka kwa kuwezesha mafunzo hayo na kuahidi kwa niaba ya wataalamu wengine wa maabara kuendelea kujituma katika kutekeleza mifumo ya ubora kwa kuzingatia matakwa ya viwango vya kimataifa vya maabara kwa kufuata taratibu na miongozo husika.
Wataalam wa Maabara kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) wakifuatilia mafunzo ya Mifumo ya Ubora ISO/IEC 17025:2017.
Mtaalam wa Maabara, Judith Swai (kushoto) akimuuliza swali mwezeshaji wa mafunzo kutoka Umoja wa Maabara Tanzania, Kezia Mbwambo.
Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mohamedi Hassani Moyo amewataka madiwani wa Halmashauri za Ruangwa na Mtama kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi na kufuata kanununi na taratibu za uongozi.
Moyo alisema hayo wakati akifungua mafunzo elekezi yenye lengo la kuwajengea uwezo katika Nyanja za uongozi, usimamizi na uwajibikaji katika kuwatumikia wananchi waliowachagua.
Alisema mafanikio ya halmashauri hizo yanategemea ushirikiano wa madiwani, wataalamu na wananchi na kuwasihi kutoingiza maamuzi binafsi na badala yake kuhakikisha wanadhibiti mianya ya rushwa na kutanguliza mbele maslahi ya umma.
“Jukumu lenu kubwa ni kudumisha amani, uzalendo, umoja, na uwajibikaji kwasababu ndio yanayochochea maendeleo”, alisema Moyo.
Aidha, aliwataka madiwani kutambua walichukua fomu na kugombea nafasi hizo kwa ajili ya kutumikia wananchi na si vinginevyo, hivyo aliwakumbusha kuacha alama katika uongozi wao ili wakumbukwe kwa mema.
Aliwataka kuepuka chuki kati yao na wataalamu pamoja na wananchi na badala yake kwenda kusimamia fedha za serikali zinazoletwa katika halmashauri ili ziweze kuleta maendeleo kwa wananchi.
Wataalamu mbalimbali wa Bajeti kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa wamekutana Jijini Dodoma na kufanya mapitio ya mpango mkakati wa Chuo hicho kuanzia 2026 hadi 2031.
Mafunzo hayo ya siku tano kuanzia Tarehe 06 hadi 09 Januari, 2026 yametolewa na Kurugenzi ya Mipango ya Mipango ya Chuo hicho ili kuwapa uelewa mpana wataalamu hao katika utekelezaji mipango kimkakati itakayoleta tija katika Chuo hicho.
Akifungua Mafunzo hayo, Mkuu wa Chuo hicho, Dkt.Yusuph Mashala amewataka wataalamu hao kufuatilia kwa umakini kwani mipango yote ya maendeleo itatokana na mpango mkakati huo.
Katika kuhakikisha Chuo cha Serikali za Mitaa kinakuwa na kuendelea kutoa huduma kwa umma kwa sasa kina kampasi tatu ambazo ni Kampasi Kuu Hombolo, Kampasi ya Shinyanga na Kampasi ya Dodoma Mjini na pia Chuo kimeshapata eneo Mkoani Njombe ili kuendelea kutoa huduma kwa kanda ya Nyanda za juu Kusini.
Serikali imeitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) kuendelea kusimamia kikamilifu upatikanaji wa huduma za bima nchini hususani zinazowahusu wageni kutoka nje ili kuboresha huduma hiyo na kuendelea kuvutia wawekezaji, watalii na wafanyabiashara kwa maslahi ya taifa.
Maelekekezo hayo yalitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Mahmoud Thabiti Kombo alipotembelea banda la mamlaka hiyo katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Zanzibar (ZITF) kuelekea Maadhimisho ya 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Katika ziara hiyo, Waziri Kombo alipata fursa ya kuelimishwa kuhusu majukumu ya TIRA katika kusimamia na kuendeleza sekta ya bima, hususan katika kuhakikisha ulinzi wa maslahi ya wageni kutoka nje wanaoingia Tanzania kwa madhumuni ya utalii, biashara na shughuli nyingine.
Alisema kuna umuhimu wa kuwepo kwa mifumo madhubuti ya bima kwa wageni ili kulinda usalama wao, kuongeza imani ya wawekezaji na watalii, pamoja na kuimarisha taswira ya Tanzania kimataifa kama nchi salama na yenye mazingira rafiki ya uwekezaji na utalii.
Aidha, alielekeza wadau wa bima kushirikiana kwa karibu na taasisi nyingine za serikali zinazohusika na masuala ya uhamiaji, utalii na afya hasa wizara yake ili kuhakikisha bidhaa za bima kwa wageni zinaeleweka, zinapatikana kwa urahisi na zinakidhi mahitaji halisi ya soko la kimataifa.
Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Kanda ya Unguja, Kurenje Mbura alimhakikishia Waziri Kombo kuwa mamlaka itaendelea kusimamia sekta ya bima kwa weledi na kushirikiana na wadau wote ili kuboresha huduma za bima kwa wageni wa nje na mizigo inayoagizwa kutoka nje jambo litakalosaidia kukuza sekta ya utalii, biashara na uchumi wa taifa kwa ujumla.
Maonesho hayo kuelekea Maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yalianza Tarehe 29/12/2025 na yanatarajiwa kumalizika tarehe 16/01/2026 katika Viwanja vya Nyamanzi Dimani Zanzibar.
The Tanzania Revenue Authority (TRA) has recorded an unprecedented revenue performance in the first half of the 2025/26 financial year after collecting Sh18.77 trillion between July and December 2025, surpassing its target by more than 3.7 per cent.
The collections reflect a growth of 13.6 per cent compared to Sh16.52 trillion collected during the same period of the 2024/25 financial year.
A statement issued yesterday by TRA Commissioner General Yusuph Mwenda said the results demonstrate improved efficiency in tax administration and rising voluntary compliance among taxpayers. Strong performance in the second quarter significantly boosted the half-year outcome.
During the October to December 2025 period, TRA collected Sh9.8 trillion against a target of Sh9.66 trillion, attaining an efficiency rate of 101.45 per cent.
The quarterly collections represent a 12.26 per cent increase compared to Sh8.73 trillion collected in the corresponding period last financial year.
December 2025 marked a historic milestone after TRA collected Sh4.13 trillion in a single month, the highest amount ever recorded since the Authority’s establishment.
“The record surpassed the previous peak of Sh3.58 trillion achieved in December 2024”, Said the statement..
The Authority said the revenue growth was supported by strong performance across key economic sectors.
Manufacturing led with an 18.1 per cent growth, followed by finance and insurance at 16.3 per cent, information and communication at 12.9 per cent, mining at 9.8 per cent, administration and support services at 7.8 per cent, and trade at 7.5 per cent.
TRA said it remains confident of meeting its annual revenue target of Sh36.06 trillion for the 2025/26 financial year, supported by sustained economic activity and enhanced tax compliance.