• By Alvar Mwakyusa

    Tanzania is expected to experience varied rainfall during the Masika season from March to May 2026, with wetter conditions in some regions and drier weather in others, the Tanzania Meteorological Authority (TMA) has said.

    TMA Director General and Vice Chair of the Intergovernmental Panel on Climate Change, Dr Ladislaus Chang’a, said enhanced rainfall activity is likely in April, raising concerns over flooding, crop damage and outbreaks of water- and vector-borne diseases in vulnerable areas.

    He urged communities, authorities and sectors to take timely action and follow daily and ten-day forecasts for localized guidance.

    The Masika rains mainly affect the country’s bimodal rainfall zones, including the Lake Victoria Basin, Northern Coast, Northeastern Highlands and northern Kigoma. Normal to above-normal rainfall is expected over most parts of the Northern Coast, western Lake Victoria Basin—including Kagera and Geita—and northern Kigoma.

    These areas could experience periods of excessive soil moisture and localized flooding, which may disrupt farming, damage infrastructure and contaminate water sources.

    Normal to below-normal rainfall is forecast for the Northeastern Highlands, covering Arusha, Manyara and Kilimanjaro, and parts of the Lake Victoria Basin such as Mwanza, Shinyanga, Mara and Simiyu.

    Reduced river flows and declining reservoir levels may lead to water shortages for domestic use, livestock and irrigation.

    The rains are expected to start in late February to early March over the Lake Victoria Basin, early to mid-March along the Northern Coast, and mid-March in the Northeastern Highlands, before ending between late May and early June, depending on location.

    Health officials warn that heavy rains could increase malaria, cholera and other water-related diseases, particularly where flooding contaminates water sources and drier areas may also face health challenges linked to unsafe water.

    The outlook also highlights possible impacts on agriculture, livestock, transport, energy and water sectors whereas farmers in wetter areas may face waterlogging and crop losses, while drier zones risk reduced yields.

    Flooding could disrupt roads, railways and marine transport, and fluctuating water levels may affect hydropower generation and increase water treatment costs.

    TMA attributes the seasonal pattern to largely neutral sea surface temperatures in the Indian and Pacific Oceans, with weak westerly winds from the Congo Basin expected to enhance moisture inflow into parts of the western Lake Victoria Basin later in the season.

    Authorities, communities and the private sector are urged to use forecast in planning and preparedness measures, and to rely on official updates issued by TMA.

  • Na Alvar Mwakyusa

    Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza mwelekeo wa mvua za msimu wa Masika kwa mwaka 2026, ikieleza kuwa baadhi ya maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi juu ya wastani, huku maeneo mengine yakitarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Februari 5, 2026, mvua za Masika zinazotarajiwa kuanza mwezi Machi hadi Mei zitahusisha zaidi ukanda wa Ziwa Victoria, Nyanda za juu Kaskazini Mashariki, Pwani ya Kaskazini pamoja na Kaskazini mwa mkoa wa Kigoma.

    TMA imeeleza kuwa ongezeko la mvua linatarajiwa zaidi mwezi Aprili, hali inayoweza kuambatana na athari mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

    Akizungumza wakati wa kutangaza mwelekeo huo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), alisema ni muhimu kwa jamii kutumia taarifa za utabiri wa hali ya hewa katika kupanga na kutekeleza shughuli zao za kila siku.

    Alisema mvua hizo, pamoja na faida zake katika sekta mbalimbali, zinaweza pia kusababisha changamoto ikiwemo mafuriko, uharibifu wa miundombinu na uchafuzi wa vyanzo vya maji endapo tahadhari hazitazingatiwa kwa wakati.

    Alisisitiza umuhimu wa wananchi na wadau wa sekta mbalimbali kuendelea kufuatilia utabiri wa kila siku na tahadhari rasmi zinazotolewa na TMA.

    Katika ukanda wa Ziwa Victoria, mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa katika mikoa ya Kagera na Geita pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma, huku mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu ikitarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani.

    Kwa upande wa pwani ya kaskazini ikiwemo Dar es Salaam, Tanga, Pwani na visiwa vya Unguja na Pemba, mvua za wastani hadi juu ya wastani zinatarajiwa kuanza mapema mwezi Machi na kuisha mwishoni mwa Mei au mwanzoni mwa Juni.

    Nyanda za juu Kaskazini Mashariki zinazojumuisha mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro zinatarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani, huku mvua hizo zikitarajiwa kuanza katikati ya mwezi Machi na kuisha mwishoni mwa Mei.

    TMA imeonya kuwa, licha ya mwelekeo wa jumla wa mvua, matukio ya vipindi vya mvua kubwa yanaweza kujitokeza hata katika maeneo yanayotarajiwa kupata mvua chache, hali inayoweza kuongeza hatari ya mafuriko, uharibifu wa mali na kuibuka kwa magonjwa yanayotokana na uchafuzi wa maji.

    Wadau wa sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, mifugo, afya, usafiri, ujenzi na menejimenti za maafa wametakiwa kuzingatia taarifa hizi katika kupanga na kutekeleza shughuli zao, huku wananchi wakihimizwa kuendelea kufuatilia taarifa rasmi za hali ya hewa zinazotolewa na TMA.

  • Na Vincent Mpepo, Dodoma

    Watumishi wa Idara ya Masomo ya Habari na Ukutubi chini ya Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, wametakiwa kufanyia kazi changamoto mbalimbali za wanafunzi na masuala mengine kwa wakati.

    Hayo yalisemwa na Mkuu wa Idara, Dkt. Henry Mambo, wakati akifunga kikao kazi cha idara hiyo cha siku nne kilichofanyika katika kituo cha Mkoa cha chuo hicho cha Dodoma.

    Dkt. Mambo alisisitiza kuwa watumishi wa idara hiyo wanatakiwa kushughulikia majukumu yao ya msingi, ikiwemo kufundisha, kufanya tafiti na kazi nyingine zitazosaidia maendeleo ya idara, kitivo na chuo kwa ujumla.

    Mhadhiri Mwandamizi Athumani Samzugi aliwataka watumishi wa Idara hiyo kushikamana na kusaidiana kitaaluma, akisisitiza umuhimu wa kufanya tafiti za pamoja kutokana na masomo yanayofanana katika idara.

    Mratibu wa masomo ya Ukutubi katika Idara hiyo, Ntimi Kasumo, aliwakumbusha watumishi hao kuendana na mabadiliko ya kiutendaji, ikiwemo katika usahihishaji, uwekaji wa kumbukumbu za matokeo na uwasilishaji kwa wakati.

    Aidha, aliwashauri wahadhiri wanaofundisha programu za uzamili kutoa alama kwa wakati ili kuendana na utendajikazi wa menejimenti ya chuo hicho.

  • Na Farida Mkumba

    Wanafunzi wa Chuo cha Serikali za Mitaa Kampasi ya Shinyanga wametembelea Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga kuwaona wagonjwa, kufanya usafi eneo lote linalozunguka Hospitali hiyo, kujitolea damu na kutoa misaada mbalimbali za Kijamii.

    Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wangonjwa na wananchi mbalimbali wameeleza namna wanavyoridhishwa na uwepo wa Chuo cha Serikali za Mitaa Mkoani Shinyanga kwa kuwa uwepo wake unadhihirika katika mambo mbalimbali yanayohusu jamii.

    Pamoja na mambo mengine, wanafunzi hao wamechanga pesa na kwenda kuziona jamii zenye uhitaji na hii ni katika kuonesha kuwa pamoja na kujipatia elimu kama sehemu ya jamii wanashiriki shughuli mbalimbali za kijamii.

    Kwa upande wa Maneja Kampasi wa Chuo hicho Mkoani Shinyanga Dkt.John Kasubi amesema kuwa Chuo kitaendelea kujitolea kwa Jamii ya Shinyanga kila kinapopata fursa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo na kuwataka wananchi wakipe ushirikiano ili kuionesha Jamii kuwa mbali na utoaji wa elimu pia Chuo kinajitolea kuisaidia jamii inayokizunguka chuo hicho.

  • Na Mwandishi Wetu

    Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew, amemuagiza Mkandarasi Kampuni ya Afcons ya India kuzingatia maelekezo ya serikali kuhusu viwango vipya vya mishahara kwa wafanyakazi wa ngazi za chini, vinavyotaka kulipwa shilingi 16,500 kwa siku sawa na shilingi 515,000 kwa mwezi.

    Agizo hilo amelitoa leo wakati wa ukaguzi wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika mji wa Kayanga, wilayani Karagwe, baada ya kubaini kuwa mkandarasi huyo anawalipa vibarua shilingi 12,500 kwa siku, kinyume na maelekezo ya serikali.

    Alisema serikali ilielekeza viwango hivyo vipya vya mishahara kuanza kutumika Januari Mosi mwaka huu, na kusisitiza kuwa malipo hayo yaanze mara moja pamoja na kusainiwa kwa mikataba mipya inayoendana na mabadiliko hayo.

    “Nakuelekeza kuwasilisha nakala za mikataba hiyo mipya katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kwa viongozi wa sekta ya maji katika mkoa husika”, alisema Kundo.

    Sanjali na hilo, alionesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo, ambao awali ulipangwa kukamilika Desemba 2025 kabla ya kuongezewa muda hadi Septemba mwaka huu.

    Kutokana na hali hiyo, amemuagiza Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana na viongozi wa sekta ya maji mkoani kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini iwapo vifaa vya utekelezaji wa mradi vimeagizwa na kama mpango kazi uliopo unatekelezeka kwa muda uliopangwa.

    Alisema Wizara ya Maji haitavumilia uzembe wa mkandarasi wakati wananchi wakiendelea kupata changamoto ya huduma ya maji safi na salama.

    Mradi huo wa Maji wa Miji 28 wa Kayanga, unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 64.32 na unatarajiwa kuwanufaisha wakazi 352,790, na mpaka sasa umefikia asilimia 70 ya utekelezaji.

  • Na Mwandishi Wetu

    Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imekutana na kuzungumza na wananchi wa Mtaa wa Golani, Kata ya Kimara, Wilaya ya Ubungo kwa lengo la kutatua changamoto ya upatikanaji huduma ya maji katika mtaa huo.

    Akizungumza kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Bi. Everlasting Lyaro amewatoa hofu wananchi wa Golani kwamba Mamlaka inatambua changamoto ya maji katika mtaa huo na zipo hatua za muda mfupi na mrefu ambazo zinachukuliwa ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana.

    “Kwanza tuwaombe radhi wananchi wa hapa Golani kwa changamoto ya maji mnayoipitia, tunatambua maji ni haki ya kila mmoja wetu”, alisema Bi. Everlasting.

    Alisema kwa kuanza Mamlaka italeta matenki Matano (05) yenye ujazo wa Lita 10,000 kila moja na kuyajaza maji yatakayouzwa kwa bei elekezi zoezi na zoezi hilo litafanyika kuanzia 15.01.2025 ili kukabiliana na changamoto hiyo kama hatua za awali ambazo ni za muda mfupi.

    “Tutaratibu mgao wa maji katika eneo hili ambapo mtapata maji mara tatu kwa wiki, Alhamisi, Jumapili na Jumatatu”, alisema Bi. Evarlasting.

    Akizungumzia utatuzi wa changamoto hiyo kwa mpango wa muda mrefu alisema DAWASA itajenga kituo cha kusukuma maji eneo la kwa Mama Stela kitakachosaidia maji kufika sehemu mbalimbali zilizookua hazipati huduma hiyo hapo awali.

    Kwa upande wake, Meneja wa Mkoa wa kihuduma DAWASA Kinyerezi, Mhandisi Antony Budaga alisema watumishi hawatakaa ofisi badala yake watatoka kuwafikia wananchi na kuhakikisha yaliyopangwa katika kikao hicho yanatekelezwa.

    Mkazi wa Golani, Rajabu Said ameshukuru jitihada zinazofanyika kuhakikisha changamoto ya maji mtaani hapo inakwisha kwamba wananchi wanapata matumaini ya upatikanaji wa huduma ya maji amabayo itawaondolea kero ya ununuzi wa maji kwa watoa huduma binafsi inayowagharimu fedha nyingi.

  • Mwezeshaji kutoka Umoja wa Maabara Tanzania, Kezia Mbwambo akifafanua jambo kuhusu mifumo ya ubora kwa wataalam wa maabara kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye mafunzo yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam.

    Na Okello Thomas

    Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imetoa mafunzo ya utekelezaji wa ISO/IEC 17025:2017 kwa wataalamu wa maabara ili kuongeza umahiri katika utendaji wa kila siku katika maabara.

    Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki kwenye ukumbi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko amesema Kiwango cha ISO/IEC 17025:2017 kinaipa maabara uwezo wa kuonesha umahiri katika kufanya uchunguzi na kutoa matokeo yanayotambulika na kukubalika kitaifa na kimataifa

    “Utekelezaji wa kiwango hicho si hitaji la ithibati pekee, bali ni nyenzo muhimu ya kuimarisha ubora, uaminifu na ushindani wa huduma za maabara”, alisema Dkt. Mafumiko.

    Alisema maabara kupata ithibati na kuitekeleza kwa vitendo yatatoa sifa njema si tu kwa mamlaka bali pia kwa taifa kwa ujumla.

    “Nitumie fursa hii kusisitiza kwamba juhudi na uwajibikaji wenu ndiyo msingi wa mafanikio ya ithibati katika mamlaka”, alisema Dkt. Mafumiko.

    Alisema mamlaka itaendelea kutoa rasilimali zinazohitajika kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa ubora ulioanzishwa kulingana na mahitaji ya viwango vya ubora wa kimataifa (ISO).

    Mwezeshaji kutoka Umoja wa Maabara, Bi. Kezia Mbwambo alisema kuwa Kiwango cha ISO/IEC 17025:2017 ni mfumo wa usimamizi uliotengenezwa na Shirika la Viwango vya Kimataifa (ISO) linalolenga seti ya mahitaji ambayo taasisi au shirika linapaswa kufikia katika mfumo wa ubora ili kupata hati ya ISO.

    Naye Riphat Lusingo ameishukuru mamlaka kwa kuwezesha mafunzo hayo na kuahidi kwa niaba ya wataalamu wengine wa maabara kuendelea kujituma katika kutekeleza mifumo ya ubora kwa kuzingatia matakwa ya viwango vya kimataifa vya maabara kwa kufuata taratibu na miongozo husika.

    Wataalam wa Maabara kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) wakifuatilia mafunzo ya Mifumo ya Ubora ISO/IEC 17025:2017.

    Mtaalam wa Maabara, Judith Swai (kushoto) akimuuliza swali mwezeshaji wa mafunzo kutoka Umoja wa Maabara Tanzania, Kezia Mbwambo.

  • ← Back

    Thank you for your response. ✨

    Drag and drop or click to select a file.

  • Na Mwandishi Wetu, Nachingwea

    Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mohamedi Hassani Moyo amewataka madiwani wa Halmashauri za Ruangwa na Mtama kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi na kufuata kanununi na taratibu za uongozi.

    Moyo alisema hayo wakati akifungua mafunzo elekezi yenye lengo la kuwajengea uwezo katika Nyanja za uongozi, usimamizi na uwajibikaji katika kuwatumikia wananchi waliowachagua.

    Alisema mafanikio ya halmashauri hizo yanategemea ushirikiano wa madiwani, wataalamu na wananchi na kuwasihi kutoingiza maamuzi binafsi na badala yake kuhakikisha wanadhibiti mianya ya rushwa na kutanguliza mbele maslahi ya umma.

    “Jukumu lenu kubwa ni kudumisha amani, uzalendo, umoja, na uwajibikaji kwasababu ndio yanayochochea maendeleo”, alisema Moyo.

    Aidha, aliwataka madiwani  kutambua walichukua fomu na kugombea nafasi hizo kwa ajili ya kutumikia wananchi na si vinginevyo, hivyo aliwakumbusha kuacha alama katika uongozi wao ili wakumbukwe kwa mema.

    Aliwataka kuepuka chuki kati yao na wataalamu pamoja na wananchi na badala yake kwenda kusimamia fedha za serikali zinazoletwa katika halmashauri ili ziweze kuleta maendeleo kwa wananchi.