
Na Cosmas Msuha
Serikali imezindua mradi maalum wa kuboresha huduma za dharura na usalama barabarani katika jiji la Dar es salaam kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kutoka nchini Japan wenye lengo la kupunguza madhara kwa wahanga wa ajali za barabarani.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma hizo jana jijini Dar es salaam, Mganga Mfawidhi Dkt. Bryceson Kiwelu al;isema Hospital ya Amana ni Iitakuwa ni kitovu cha uboreshaji wa huduma za dharura Katika mradi huo kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2025/2028.
Alisema serikali imeandaa mfumo wa ulinzi na sheria za barabarani kupitia taarifa za jeshi la polisi, wizara ya ujenzi na hospitali ziweze kusomana.
Alisema serikali kwa kushirikiana na wadau wa mfumo wanapaswa kutoa elimu ya matumizi sahihi ya barabara kwa wanafunzi wa shule za msingi ili kujenga uelewa na utamaduni wa usalama barabarani katika jamii.
“Hospitali ya Amana imechaguliwa kuwa kitovu cha mradi huo, ambapo huduma zitatolewa ndani ya kipenyo cha Kilomita tano kuzunguka hospitali hiyo,”alisema Dkt.Kiwelu.
Mratibu wa operesheni kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Dar es salaam, Michael Bachubila, amewataka wananchi kutumia namba ya dharura 114 wakati wowote wanaposhuhudia ajali au tukio la dharura Katika maeneombali mbali ya makazi yao.
Bachubila alisema Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limejiandaa kikamilifu kwa vifaa vya kisasa pamoja na wataalamu waliopata mafunzo maalum ya uokoaji na huduma za awali za dharura.
Aidha serikali imesema mradi huo utaanza kwa majaribio katika jiji la Dar es salaam na ikiwa utafanikiwa unatarajiwa kupanuliwa katika mikoa mingine nchini.




















