Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba amewapongeza watumishi wa Bandari ya Tanga na kuwataka waendelee kufanya kazi kwa bidii ili kuunga mkono juhudi za serikali katika uwekezaji mkubwa uliofanyika katika bandari hiyo.
Kolimba alitoa pongezi hizo baada ya kutembelea na kukagua banda la Bandari ya Tanga kwenye maonesho ya 12 ya Biashara na Utalii (Tanga Trade Fair) yanayofanyika katika viwanja vya Mwahako kuanzia tarehe 28 Mei hadi 6 Juni 2025.
“Serikali imewekeza kiasi cha Shilingi za Kitanzania Billioni 429.1 hivyo endeleeni kuwajibika ipasavyo ili uwekezaji huo uweze kuzaa matunda sabamba na uhudumiaji wa shehena na ukusanyaji wa mapato uzidi kuongezeka” alisema Kolimba
Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya huyo, Kaimu Mkuu wa Idara ya Usaidizi wa Biashara Bi. Rose Tandiko kwa niaba ya Meneja wa Bandari, alisema Bandari ya Tanga imeshiriki katika maonesho hayo kwa utoaji wa elimu kwa umma juu ya faida itakayopatikana baada ya mradi huo kukamilika.
Bi. Rose alitoa rai kwa wafanyabiashara kuitumia Bandari ya Tanga kwani huduma zake zimeboreshwa na hakuna msongamano kutokana na utendaji kazi wenye ufanisi na wafanyakazi wenye ari kubwa.
Alisema uwekezaji uliofanywa na serikali umekusudia kuijengea uwezo bandari hiyo ili iweze kuhudumia shehena kutoka tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka.
Maonesho ya 12 ya Biashara na Utalii ambayo husimamiwa na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) ambapo kauli mbiu mwaka huu ni “Mwonekano wa Wadau Sekta ya Umma na Binafsi Kwenye Uwekezaji, Ukuaji na Uendelevu wa Biashara”.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Umeme Tanzania -Tanesco Mkoani Ruvuma imeanza kulipa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa gridi ya taifa ya Msongo wa 220KV kutoka Songea hadi Tunduru ambapo zaidi ya wananchi 200 watanufaika na fidia hiyo.
Wanufaika wa fidia hiyo ni wale wanaoishi kijiji cha Mlete, Kata ya Shule ya Tanga Manispaa ya Songea na kwamba kukamilika kwa mradi huo kutachochea shughuli za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja hivyo kukuza pato la taifa.
Akizungumza na wananci wa maeneo yaliyolipiwa fidia, Afisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja Tanesco Mkoa wa Ruvuma, Alan Njiro aliwataka wakazi wa maeneo hayo kutorejea tena ili kupisha utekelezaji wa mradi huo.
“Nishati ya umeme imewafikia wananchi wa Mlete hivyo ni jukumu la kila mmoja wenu kuwa mlinzi wa miundombinu hii ili kuendelea kunufaika nayo kwa muda mrefu”, alisema Njiro.
Aidha alisema serikali itaendelea kuboresha huduma ya umeme na kuwaasa wananchi hao kutoa taarifa kwa kupiga simu bure kupitia namba 180 kwa maulizo, dharura na uhitaji wa huduma nyingine.
Mtumishi wa Tanesco kutoka Makao Makuu, Phlasida Lalika aliwaasa wananchi kutumia vizuri fedha za fidia kwa kuanzisha miradi na shughuli za ujasiriamali ili kujiongezea kipato.
Mtumishi Mwingine wa Tanesco, Winifrida Masuka alisema wameenda kijijini hapo ili kuwahakikishia kuwa serikali kupitia Tanesco itawalipa fidia hizo kwa wakati ili watafute maeneo mbadala.
Kwa Upande wao wanufaika wa fidia hiyo wameishukuru Tanesco pamoja na Serikali kwa kuwa malipo hayo yamekuja wakati muafaka na kwamba pesa hiyo itasaidia katika shughuli mbalimbali ikiwemo kutafuta maeneo mbadala na kulipa ada za watoto.
Afisa Tarafa Songea Mjini Mashariki, Dismas Komba ni alishukuru serikali kwa kazi kubwa na nzuri ya kuwaletea maendeleo wananchi na kwamba mchakato wa uthaminishaji wa maeneo ya wananchi ulianza Mwezi Mei 2023.
“Ofisi yangu na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Songea zinawashauri kutumia vyema pesa za fidia kwa ajili ya ujenzi wa makazi badala ya kufanya vitu visivyofaa ikiwemo kuoa wanawake”, alisema Komba.
Licha ya kuipongeza serikali kwa kusogeza huduma muhimu kwa wananchi alisema umeme utakaopatikana katika mradi huo utachochea kasi ya maenedeleo na kuvutia wawekezaji kupitia viwanda na shughuli nyingine zinazotegemea nishati ya umeme.
Maafisa wa Tanesco Kutoka Mkoa wa Ruvuma na waandishi wa habari walifika kijiji cha Mlete ilipo ofisi ya Mtaa ambako zoezi la kukabidhi hundi na kuwafungulia akaunti wananchi linaendelea huku kiasi cha shilingi bilioni 2.5 zinaendelea kulipwa kwa wananchi waliopisha maeneo yao kuruhusu mradi huo.
African countries have been called upon to work together instead of acting alone in the fight against poverty and exploitation. This cooperation would help fulfill the dreams of Africa’s founding leaders, such as Mwalimu Julius Nyerere and Nelson Mandela.
This call was made during an academic forum held yesterday at Johari Rotana Hotel in Dar es Salaam which was attended by scholars, academics, government leaders, private sector representatives, and diplomats from across Africa and beyond.
During the forum, Professor Senia Nhamo from the University of South Africa (UNISA) said African nations can gain a lot by joining hands and taking advantage of shared economic opportunities.
“We can make better use of our resources and trade more with each other if we cut down bureaucracy and remove customs and tax barriers,” said Prof. Nhamo.
She pointed out that challenges like lack of a single African currency and customs duties need to be addressed. She also encouraged African governments to invest in useful research and urged universities to share research findings with the public instead of keeping them in libraries.
Dr. Dunlop Ochieng, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences at the Open University of Tanzania said some development projects and investments ignore local people which leads to poor cooperation.
He said it’s important to include local communities in all development efforts so they are active participants, not just observers in their own land.
Executive Director of the Mwalimu Julius Nyerere Foundation, Joseph Butiku, said Africa needs strong and continuous leadership to reach its development goals.
“Africa is falling behind because there is no consistency in planning and following through with priorities when leadership changes,” said Butiku.
He noted that new leaders often bring in their own priorities and ignore those of past leaders.
Butiku also thanked former South African President Thabo Mbeki for choosing Tanzania to host the forum, which helped assess the importance of the blue economy adding that the relationship between Tanzania and South Africa goes back to the time of the struggle for independence.
A researcher from Tanzania’s National Defence College, Dr. Lucy Shule, said African countries must work together at regional and continental levels to drive economic growth.
She said working in unity brings more strength than working alone.
On the topic of the blue economy, she stressed the need for African governments to raise awareness about the concept and create policies to protect local communities so they benefit from marine resources.
Madereva wanaosafirisha abiria na mizigo kwenda sehemu mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Songwe wametakiwa kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za madereva wenzao wazembe ili hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Songwe, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), Charles Bukombe baada ya kufanya oparesheni ya ukaguzi wa magari ya abiria na mizigo katika Kituo cha Ukaguzi wa Magari Mkoani humo eneo la Chimbuya Wilaya ya Mbozi.
SSP Bukombe alisema lengo la operesheni hiyo pamoja na ukaguzi huo ni kuangalia ubovu wa magari hasa ukaguzi wa mataili, kukagua madeni ya magari ambayo bado hayajalipwa, ukaguzi wa leseni, ujazaji wa abria kupita uwezo wa chombo pamoja na ukaguzi wa tiketi mtandao ili kuepusha ajali zinazoweza.
“Niwaombe madereva na abiria kutofumbia macho vitendo vya ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani na badala yake mnatakiwa kukemea na kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ili hatua za haraka zichukuliwe” alisema SSP Bukombe.
Kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Mbozi Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba alisema jeshi la polisi linaendelea kutoa elimu kwa abiria juu ya umuhimu wa kufichua taarifa za madereva wazembe wasiofuata sheria za usalama barabarani.
Alisema Jeshi la Polisi nchini linaendelea na operesheni za ukaguzi wa vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na utoaji elimu kwa jamii kuhusu masuala ya usalama barabarani ili kutokomeza ajali za barabarani kwa watumiaji wa vyombo vya moto na watembea kwa miguu na kupunguza ajali ambazo zinaepukika.
Katika operesheni hiyo jumla ya magari 54 yalikaguliwa na kati ya hayo magari 8 yalikutwa na changamoto ambazo zinaweza kusababisha ajali ikiwa ni pamoja na kasoro katika leseni 17 za madereva.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akizungumza na wadau wa kemikali bashirifu zaidi ya 40 wakati akifungua kikao cha wadau wa Kemikali Bashirifu na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kilichofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Dar es Salaam, Mei 28, 2025.
Na Okello Thomas
Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imewakumbusha wadau wanaojihusisha na shughuli za kemikali kuhakikisha wanazingatia matumizi salama ya kemikali na kutojihusisha na uchepushwaji wa kemikali bashirifu kwa ajili ya utengenezaji wa dawa za kulevya.
Akizungumza wakati akifungua kikao kilichofanyika katika Hotelk ya Golden Tulip jijin Dar es salaam, Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko amewataka wadau wa kemikali kushirikiana na Mamlaka za Udhibiti ili kutokomeza uchepushwaji wa kemikali bashirifu kwa ajili ya matengenezo ya dawa za kelevya kwani dawa za kulevya huleta athari za kiuchumi, nguvu kazi na kuporomoka kwa maadili.
“Nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa inatokomeza uingiaji, utengenezaji na matumizi ya dawa za kulevya nchini”, alisema Dkt. Mafumiko.
Alisema ili malengo hayo yatimie ni lazima kuziba mianya yote inayochangia masuala hayo kufanyika kila mmoja wetu katika jamii awajibike.
Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Daniel Ndiyo, akiwasilisha mada kuhusu udhibiti wa kemikali bashirifu kwa wadau wa hao wakati wa kikao kilichofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Dar es Salaam, Mei 28, 2025.
Kamishna wa Ukaguzi na Sayansi Jinai kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Domician Mutayoba alisema kupitia Mamlaka za Udhibiti wanahakikisha wanatengeneza ushirikiano imara na wadau ili kuzuia na kudhibiti uchepushwaji wa kemikali bashirifu zisitumike katika utengenezaji wa dawa za kulevya na silaa.
Kwa upande wake Meneja wa Total Med-Lab Solutions, Shaphii Miraji ameishauri Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wadau wa kemikali kwani teknolojia inabadilika hivyo elimu endelee kutolewa ili kuboresha masuala ya kemikali nchini.
Wadau wa Kemikali bashirifu kutoka kampuni mbalimbali wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa katika kikao baina ya Mamlaka na wadau hao kilichofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Dar es Salaam, Mei 28, 2025.
The Open University of Tanzania (OUT) will launch a Bachelor’s programme in Records and Archives Management starting from the 2025/2026 academic year after fulfilling the requirements set by the Tanzania Commission for Universities (TCU).
Speaking during a stakeholders’ engagement workshop held today on the programme in Kinondoni- Dar es salaam, Assistant Lecturer Chausiku Mwinyimbegu said the programme is designed to provide training for individuals without prior academic backgrounds in records, archives, library and information studies who are interested in pursuing careers in the profession.
“The programme aims to offer excellent preparation for training professionals in records and archives management,” said Mwinyimbegu.
She said the programme will be delivered through the Open and Distance Learning (ODL) mode and the university expects to enroll students who are aspiring to build careers in the field.
Contributing to the discussion on behalf of her group, a lecturer from Dar es Salaam Tumaini University (DarTU), Dr. Getrude Ntulo, said the team had thoroughly reviewed the programme including its title, content, relevance, and compliance with the framework set by the Tanzania Commission for Universities.
She also noted that the programme aligns with the current Education and Training Policy and addresses the ministry’s emphasis on competence-based education during curriculum reviews and development of new programmes.
Dr. Ntulo commended the department for their efforts in developing the programme.
A senior lecturer from the University of Dar es Salaam Dr. Esther Ndenje, emphasized the need to rearrange certain topics to ensure a coherent and logical flow of teaching materials throughout the curriculum.
“Sometimes it’s easy to list sub-topics in a curriculum, but the real challenge comes during actual teaching,” noted Dr. Ndenje.
A Bachelor’s student in Records and Archives Management from the Tanzania Public Service College (TPSC), Martha Mohamed, stressed the importance of involving stakeholders in the development of new academic programmes.
She said an inclusive approach ensures diverse perspectives are considered and ultimately leading to a more comprehensive and effective curriculum.
“Involving stakeholders from the field helps universities and colleges design well-informed and relevant content in records and archives management,” said Martha.
Wadau wa Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu katika picha ya pamoja leo wakati wa warsha ya mapitio ya Mtaala wa Shahada ya Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu iliyifanyika leo jijini Dar es salaam na kuhusisha wanataaluma, waanafunzi, wahitimu, waajiri, vyama vya kitaaluma na wafanyakazi katika kada hiyo katika sekta za umma na binafsi.
Na Vincent Mpepo
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) kitaanza kutoa programu ya Shahada ya Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu kuanzia mwaka wa masomo wa 2025/2026 baada ya kutimiza vigezo na masharti ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).
Akizungumza wakati wa warsha ya wadau kuhusu programu hiyo leo Kinondoni, jijini Dar es salaam, Mhadhiri Msaidizi wa chuo hicho, Chausiku Mwinyimbegu alisema programu hiyo imelenga kutoa mafunzo kwa watu wenye msingi na wasio na msingi wa kitaaluma katika fani za utunzanji wa nyaraka, kumbukumbu, ukutubi na masomo ya taarifa ambao wana nia ya kufuata taaluma hiyo.
“Lengo la programu hii ni kutoa mafunzo bora na kufundisha wataalamu wa usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu,” alisema Mwinyimbegu.
Alisema programu hiyo itafundishwa kupitia mfumo wa elimu huria na masafa na kwamba chuo kinatarajia kudahili wanafunzi wanaotamani kujijenga kitaaluma katika eneo hilo.
Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es Salaam (DarTU), Dkt. Getrude Ntulo alisema wamepitia programu hiyo kwa kina katika maeneo mbalimbali ikiwemo jina, maudhui, uhalisia wa programu na namna ilivyozingatia vigezo na masharti ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.
“Masuala mengine yaliyoshughulikiwa ni pamoja na kuhakikisha programu hiyo inaendana na Sera ya Elimu na Mafunzo ya sasa pamoja na mahitaji ya mapitio ya mitaala kama yanavyoelekezwa na wizara inayohusika ambayo yanasisitiza elimu inayozingatia umahiri”, alisema Dkt. Ntulo.
Aidha aliipongeza Idara ya Masomo ya Habari na Ukutubi chuoni hapo kwa kazi nzuri waliyofanya katika uandaaji mtaala wa programu hiyo kwani anatambua siyo kitu rahisi kwa kuwa kinahusisha juhudi na kujitoa.
Kwa upande wake, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt. Esther Ndenje alisema wamependekeza mpangilio mpya wa wa mada mbalimbali ili kuhakikisha mpangilio wa kufundishia unafuata mtiririko wa mantiki na uelekevu wa kitaaluma.
“Mara nyingine ni rahisi kuweka mada ndogo kwenye mtaala lakini changamoto hujitokeza wakati wa kufundisha darasani,” alisema Dkt. Ndenje.
Mwanafunzi wa Shahada ya Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu kutoka Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Martha Mohamed, alisema ni muhimu kwa taasisi za elimu ya juu kuwashirikisha wadau katika mchakato wa kuanzisha programu mpya ili kupata maoni kuhusu maudhui ya programu ili kuoata kuunda mtaala bora.
“Kuwashirikisha wadau mbalimbali wa taaluma husika kutasaidia vyuo na taasisi za elimu ya juu kupata maudhui bora katika usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu,” alisema Martha.
Mhadhiri Msaidizi na Mratibu wa programu hiyo, Ntimi Kasumo aliwashukuru wadau wa ndani na nje walioudhuria kwa michango yao ambayo itasaidia kuboresha mtaala wa programu hiyo ili kupata wahitimu watakaokidhi vigezo na kukubalika katika soko la ajira ambalo msingi wake ni umahiri.
Wadau wa Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu katika picha za Makundi namba 1, 2 na 3 wakati wa mijadala iliyofanyika leo wakati wa warsha ya mapitio ya Mtaala wa Shahada ya Utunzaji wa Nyaraka na Kumbukumbu jijini Dar es salaam ikihusisha wanataaluma, waanafunzi, wahitimu, waajiri, vyama vya kitaaluma na wafanyakazi katika kada hiyo katika sekta za umma na binafsi.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele ametoa wito kwa vijana wote waliohitimu kidato cha sita mwaka 2025 kutoka shule zote Tanzania Bara kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2025.
Akiwasilisha wito huo jana kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kijenga Taifa JKT Jijini Dodoma, Kaimu Mkuu wa Utawala wa JKT, Kanali Juma Mrai amesema vijana hao wanatakiwa kuripoti kwenye kambi mbalimbali kuanzia Mei 28 hadi Juni 08, 2025.
Alitaja kambi ambazo wahitimu hao watakwenda kuripoti kuwa ni JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu na JKT Kibiti – Pwani, JKT Mpwapwa na JKT Makutupora – Dodoma, JKT Mafinga -Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba -Tanga, JKT Makuyuni na JKT Orjolo – Arusha.
‘Kambi nyingine ni JKT Bulombora, JKT Kanembwa na JKT Mtabila – Kigoma, JKT Itaka – Songwe, JKT Luwa na JKT Milundikwa – Rukwa pamoja na JKT Nachingwea – Lindi”, alisema Kanali Mlai.
Alisema wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (Physical Disabilities) watatakiwa kuripoti katika Kambi ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia watu wa aina hiyo.
Aidha aliwahimiza wazazi na walezi kuwapa ruhusa vijana wao kuhudhuria mafunzo hayo muhimu kwa maendeleo na kwa maisha yao ya baadae.
Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria yanalenga kuwajenga vijana katika ujasiri, nidhamu na kuimarisha maadili ya kizalendo.
Serikali imetangaza utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Teknolojia za Kidijitali katika elimu ikijumuisha miongozo ya matumizi ya teknolojia katika shule, Vyuo vya Ualimu, Vyuo vya Ufundi na Vyuo Vikuu, pamoja na matumizi ya akili bandia (Artificial Intelligence) kwa mwaka 2025.
Kauli ya utekelezaji mkakati huo ilitolewa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Jijini Dodoma wakati akielezea mafanikio ya serikali ya wamu ya sita na kubainisha maeneo kadhaa ya maboresho yatakayoongeza tija katika sekta ya elimu.
Alisema katika sekta ya elimu ya juu serikali imeanza ujenzi wa majengo ya madarasa, maabara na mabweni katika kampasi kuu na za pembezoni katika mikoa 16 ambayo haikuwa na taasisi za elimu ya juu.
Ujenzi huo unatokana na Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) wenye thamani ya shilingi bilioni 972 na utaongeza uwezo wa taasisi za elimu ya juu nchini kudahili wanafunzi zaidi na kupunguza uhaba wa wahadhiri kwa asilimia 20.
“Tunahakikisha kwamba elimu yetu inazalisha wataalamu wenye ujuzi na stadi zinazohitajiwa katika soko la ajira ili kuchangia maendeleo ya Taifa letu,” alisema Profesa Mkenda.
Alisema pamoja na mafanikio hayo serikali imeandaa Mfumo wa Kielektroniki wa Tathmini ya Ujifunzaji unaolenga kurahisisha upimaji wa wanafunzi katika shule za msingi na kuimarisha huduma kwa walimu na wanafunzi wenye mahitaji Maalumu na maboresho ya mitaala katika ngazi zote za elimu.
“Serikali inaendelea kuimarisha mfumo wa elimu kupitia maboresho makubwa ya mitaala katika ngazi zote za elimu nchini ili kuongeza ujuzi, maarifa, tina na stadi za wanafunzi wanaohitimu”, alisema Profesa Mkenda.
Alisema serikali imeweka mfumo wa elimu nyumbufu ili kuhakikisha wanafunzi wanapokea ujuzi na maarifa yanayozingatia mahitaji halisi ya taifa na soko la ajira.
“Tumeweka somo la lazima la elimu ya biashara na historia ya Tanzania huku tukiboresha mifumo ya ufundishaji lugha ili kuongeza ufanisi wa ujifunzaji,” alisema Profesa Mkenda.
Alisema mitaala 389 katika elimu ya ufundi na mitaala 563 katika elimu ya juu imeboreshwa ili kuendana na Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, Toleo la 2023 pamoja na kuzingatia stadi za karne ya ishirini na mahitaji ya kitaifa, Kikanda na Kimataifa.
“Serikali inaendelea kufanya mapitio ya Sheria ya Elimu (Sura 353) ili kuendana na mabadiliko haya ya sera na mitaala”, alisema Profesa Mkenda.
Alisema wizara yake inaendelea kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu ili kuhakikisha sheria husika inakidhi mahitaji ya sasa ikiwemo ushirikishwaji wa umma.
Aliongeza kuwa serikali imehuisha miongozo mbalimbali ikiwemo Mwongozo wa Taifa wa Tuzo na Sifa Linganifu za Kitaaluma (TQF), Mwongozo wa Uanzishaji na Usajili wa Shule, Mwongozo wa Utambuzi wa Vipawa na Vipaji, pamoja na Mwongozo wa Mafunzo Endelevu ya Walimu Kazini.
Aidha, Waziri Mkenda amewataka wananchi na wadau wa elimu kuendelea kushirikiana na serikali katika kuimarisha mfumo wa elimu nchini ili kuhakikisha elimu inakuwa chachu ya maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.