• CCT

    Na Vincent Mpepo

    Mwinjilisti Neema Mhilu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) amesema suala la wakristo kuishi pamoja ni suala la kibiblia na kusisitiza kuwa Umoja wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania unasawiri uhalisia huo.

    Mwinjilisti Mhilu aliyasema hayo jana wakati wa mahuburi katika ibada ya Siku ya 5 baada ya Pasaka katika Mtaa wa Kwembe ambapo kwa mujibu wa kalenda ya KKKT ni siku ya Umoja wa Jumuiya ya Kikristu Tanzania yaani (CCT).

    Alisema biblia inaagiza ndugu wakae pamoja kwa upendo akirejelea maneno kutoka kitabu cha Warumi 12:13-15 na kwamba kuishi pamoja kuna faida nyingi ikiwemo namna bora ya kujaliana na kuhudumiana tukiwa hapa duniani.

    “Suala la umoja ni suala la kibiblia na lilianzishwa na Yesu mwenyewe”, alisema Mwinjilisti Mhilu

    Alisema wakristo wanapaswa kuuenzi umoja huo kwa sababu kufanya hivyo ni kutekeleza maagizo ya Mungu na upendo ukitawala kuna faida nyingi ikiwemo kuishi kwa mshikamano na amani katika ngazi ya mtu na mtu lakini pia hata katika jamii na taifa na kuhusiana vyema na watu wengine wasio wakristo.

    “Umoja huu ulinzishwa Mwaka 1934 na una vyama na taasisi 24 kwa madhumuni ya kumhubiri kristo ndani na nje ya Tanzania”, alisema Mwinjilisti Mhilu.

    Aidha aliwataka wakristo kuuishi ukristo wao kwa matendo kwa kuwa matendo mema yanaendana na nguvu itakayowatambulisha kwa watu wasio wakristo ambao wanatambua nguvu na thamani ya ukristo na kuwaasa kubaki katika Imani zao badala ya kuhamahama kufuata miujiza.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Ujenzi Mtaani hapo, Exaud Mchome aliwataarifu washarika kuhusu kukamilika kwa kazi ya kuezeka jengo la kanisa na ambalo linaendelea kujengwa kwa sadaka za washarika mtaani hapo.

    “Sehemu zilizobaki zitafanyiwa kazi kwa ushauri wa Mchungaji na katika kikao chetu cha leo tutafanya maamuzi ili kufikia wiki ijayo kazi hiyo iwe imekamilika kabisa”, alisema Mzee Mchome ambaye kwa sasa anafahamika kwa jina la Hagai.

    Aliwakumbusha washarika kuendelea kukamilisha ahadi zao kwa awamu ya kwanza iliyoanza Januari mpaka Juni Mwaka 2025 huku akiwahakikishia kuwa taarifa ya mapato na matumizi ya pesa hizo zitaletwa kwa washarika ili waone.

    Mtendakazi wa Mtaa huo, Anna Mauki aliwakumbusha washarika mambo kadhaa ikiwemo kuhudhuria ibada ya siku ya kupaa kwa Bwana itakayofanyika siku ya Alhamisi na kuendelea kutoa sadaka ya ujenzi wa kituo cha kimataifa cha watoto wenye mahitaji maalumu ambacho kinahamishwa kutoka Kijichi kwenda Dar es salaam Kitopeni, Bagamoyo.

  • Na Vincent Mpepo

    Nchi za Afrika zimetakiwa kuunganisha nguvu na kufanya kazi kwa kushirikiana badala ya kila nchi peke yake ili kupiga vita umaskini na kujikwamua dhidi ya unyonyaji na kuenzi ndoto na maono ya waasisi wa bara la Afrika ikiwemo Mwalimu Julius Nyerere na Neslon Mandela.

    Hayo yalibainishwa na washiriki wa mjadala wa kitaaluma uliofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa Hotel ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wasomi, wanataaluma viongozi wa serikali, taasisi binafsi na wanadiplomasia wa ndani na nje ya Afrika.

    Akiwasilisha mada katika mjadala huo, Profesa Senia Nhamo kutoka Chuo Kikuu cha Afrika Kusini (UNISA) alisema bado kuna faida kuwa ya kuungana na kufanya kazi pamoja kutokana na fursa za kiuchumi zinazopatikana kati ya mataifa ya Afrika ambayo inaweza kuwapa nguvu ya kiuchumi.

    “Tunaweza kutumia rasilimali zetu na kufanya biashara kati yetu ikiwa tutapunguza urasimu na vikwazo katika kodi na ushuru wa forodha”, alisema Profesa Nhamo.

    Alibainisha baadhi ya changamoto ambazo zikifanyiwa kazi zinaweza kusaidia katika kuboresha uchumi wa Afrika ikiwemo matumizi ya fedha moja pamoja na kundoa vikwazo vya ushuru wa forodha.

    Aidha alizitaka serikali barani Afrika kuwekeza kwenye tafiti zenye tija na kwamba taasisi za elimu ya juu zisifungie tafiti kwenye maktaba badala yake matokeo ya tafiti yawe wazi kwa wananchi na yasaidie utatuzi wa chngamoto za jamii husika.

    Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku alisema Afrika inahitaji kuwa na mwendelezo wa mipango endelevu kiuongozi ili kufikia maendeleo inayoyakusudia.

    “Kuna shida ya kutokuwepo kwa mwendelezo wa mipango na utekelezaji wa vipaumbele vya kimaendeleo kutokana na mabadiliko ya uongozi hivyo kuendelea kubaki nyuma”, alisema Butiku.

    Alisema kila wakati na kila uongozi huja na vipaumbele vyake vya kiutekelezaji ambavyo wakati mwingine huwa ni vipya badala ya kuendeleza walivyovikuta ambavyo vilianzishwa na watangulizi wao.

    Aidha alimshukuru Rais Thabo Mbeki kwa kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa mjadala huo uliosaidia kufanya tathimini ya thamani ya uchumi wa bluu na kwamba uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini ni wa kihistoria tangu nyakati harakati za kupigania Uhuru.

    Kwa upande wake, Mtafiti kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi-Tanznia, Dkt. Lucy Shule alisema ushirikiano kati ya nchi na nchi na kikanda barani Afrika ni mojawapo ya mikakati itakayosaidia kuivusha Afrika kiuchumi kwa kuwa ushirikiano huongeza nguvu katika kufanya jambo badala ya kila nchi kufanya peke yake.

    Aidha akizungumzia uchumi wa blue endelevu alisema bado kuna haja ya serikali za nchi za Afrika kutoa elimu ya dhana ya uchumi wa bluu na kuweka sera za ulinzi kwa wazawa ili wawe wanufaika wa mazao yanayotokana na rasilimali za bahari.

    Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt.Dunlop Ochieng alisema wakati mwingine mipango inayohusisha maendeleo ikiwemo uwekezaji imekuwa ikiwabagua wenyeji na matokeo yake ni kutopata ushirikiano mzuri.

    Alisema katika kila aina ya shughuli ya maendeleo inayopaswa kufanyika mahali popote ni muhimu kuzingatia wazawa ili wawe ni sehemu ya maendeleo hayo badala ya kuwa wasindikizaji kwenye ardhi yao.

  • Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa akielezea majukumu mbalimbali ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa madereva wanaosafirisha kemikali kutoka kampuni ya Golden Coach jijini Dar es Salaam.

    Na Okello Thomas

    Madereva wanaosafirisha kemikali hatarishi wametahadharishwa kutotumia dawa za kulevya wanaposafirisha kemikali hatarishi ili kujiepusha na ajali za barabarani zinazochangiwa na madhara ya dawa hizo.

    Tahadhari hiyo imetolewa leo na Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa wakati akifunga mafunzo kwa madereva wanaosafirisha kemikali kutoka kampuni ya Golden Coach ya Dar es Salaam hivi karibuni katika ukumbi wa mafunzo wa Golden Coach.

    “Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya kwa madereva wanaosafirisha kemikali hatarishi kwa kuwa wengi ni vijana na nguvu kazi ya taifa”, alisema Mkapa.

    Alisema madereva wote wanaosafirisha kemikali hatarishi wanapaswa kuepuka kuendesha vyombo vya moto wakiwa wametumia vilevi kwasababu ni hatari kwao na ukizingatia mzigo wanaobeba na mazingira wanayopita na kuhitaji umakini sana.

    Aidha, alisema matumizi ya madawa ya kulevya wakati wa usafirishaji, huathiri uwezo wa kufikiri, kutafakari na uwezo wa kuona jambo ambalo dereva anageweza kulifanyia maamuzi sahihi ili kuwa na thadahari za haraka bila kusabisha ajali ajali ambazo zingeweza kuzuilika.

    Mkapa ametoa rai kwa wamiliki wa kampuni za kusafirisha kemikali hatarishi kuendelea kutoa elimu kwa madereva wao kuhusu ufahamu wa makundi ya kemikali wanazosafirisha kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini.

    Dereva wa kampuni ya Golden Coach, Saidi Kisindula alisema baada ya kupata mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali itawasaidia kuwa makini katika kazi hiyo.

    Madereva kutoka kampuni ya Golden Coach wakifuatilia mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyotolewa na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

    Alisema wataendelea kuwa mabalozi kwa kuendelea kutoa elimu hiyo kwa madereva wenzao wanaofanya kazi hiyo ya usafirishaji wa kemikali katika makampuni mbambali nchini.

  • Na Gloria Maganza, Dodoma

    Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa pamoja na wananchi wa Kata ya Haubi wamefanikisha operesheni maalumu ya kutokomeza kilimo haramu cha bangi katika maeneo ya Hifadhi ya Milima ya Haubi, wilayani Kondoa, mkoani Dodoma.

    Akizungumza kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa DCEA, Naibu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wa Mamlaka hiyo, Daniel Kasokola, alisema operesheni hiyo iliyofanyika kuanzia Mwezi Mei 14 hadi 19,2025 na imefanikisha kuteketeza ekari 157 za mashamba ya bangi yaliyokuwa katika vijiji vya Ntomoko, Kinyasi na Haubi.

    Aidha, watuhumiwa saba wanashikiliwa kwa mahojiano huku pikipiki mbili zikikamatwa katika maeneo ya operesheni.

    “Operesheni hii ni ya pili kufanyika mwaka huu katika wilaya ya Kondoa ambapo mwezi  Januari tulibaini na kuteketeza zaidi ya ekari 500 za bangi”, alisema Kasokola.

    Alisema kupungua kwa mashamba hayo kutoka ekari 500 hadi 157 ni ushahidi kuwa wananchi wameanza kuelewa na kushiriki kikamilifu katika jitihada hizi na kwamba anapongeza kwa ushirikiano wao unaowezesha operesheni hiyo kufanikiwa.

    Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Fatuma Nyangasa amesisitiza kuwa serikali ya Wilaya ya Kondoa  itaendelea kushirikiana kwa karibu na mamlaka hiyo kuhakikisha kilimo cha bangi kinatokomezwa kabisa na kusisitiza kuwa elimu kwa wananchi itaendelea kutolewa ili waachane na kilimo haramu badala yake wajikite  katika uzalishaji wa mazao halali ya chakula na biashara kama vile tumbaku, ufuta na maharage.

    “Serikali ipo tayari kuwaongoza katika kilimo halali na chenye tija badala ya bangi, zaidi niwaombe wanachi washirikiane naserikali”, alisema Nyangasa.

    Aidha Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya itaendelea kuchukua hatua kali kwa yeyote atakayejihusisha na kilimo, biashara au usambazaji wa bangi na dawa nyingine za kulevya.

  • By Vincent Mpepo

    African countries have been called upon to work together instead of acting alone in the fight against poverty and exploitation. This cooperation would help fulfill the dreams of Africa’s founding leaders, such as Mwalimu Julius Nyerere and Nelson Mandela.

    The call was made during an academic forum held yesterday at Johari Rotana Hotel in Dar es Salaam which was attended by scholars, academics, government leaders, private sector representatives, and diplomats from across Africa and beyond.

    During the forum, Professor Senia Nhamo from the University of South Africa (UNISA) said African nations can gain a lot by joining hands and taking advantage of shared economic opportunities.

    “We can make better use of our resources and trade more with each other if we cut down bureaucracy and remove customs and tax barriers,” said Prof. Nhamo.

    She pointed out that challenges like lack of a single African currency and customs duties need to be addressed. She also encouraged African governments to invest in useful research and urged universities to share research findings with the public instead of keeping them in libraries.

    Dr. Dunlop Ochieng, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences at the Open University of Tanzania said some development projects and investments ignore local people which leads to poor cooperation.

    He said it’s important to include local communities in all development efforts so they are active participants, not just observers in their own land.

    Executive Director of the Mwalimu Julius Nyerere Foundation, Joseph Butiku, said Africa needs strong and continuous leadership to reach its development goals.

    “Africa is falling behind because there is no consistency in planning and following through with priorities when leadership changes,” said Butiku.

    He noted that new leaders often bring in their own priorities and ignore those of past leaders.

    Butiku also thanked former South African President Thabo Mbeki for choosing Tanzania to host the forum, which helped assess the importance of the blue economy adding that the relationship between Tanzania and South Africa goes back to the time of the struggle for independence.

    A researcher from Tanzania’s National Defence College, Dr. Lucy Shule, said African countries must work together at regional and continental levels to drive economic growth.

    She said working in unity brings more strength than working alone.

    On the topic of the blue economy, she stressed the need for African governments to raise awareness about the concept and create policies to protect local communities so they benefit from marine resources.

  • By Vincent Mpepo

    Academics and researchers in African higher learning institutions have been urged to conduct studies that provide practical solutions for the sustainable use of marine resources in order to effectively implement the Blue Economy concept and drive Africa’s economic and social development.

    A group photo of academics from the Faculty of Arts and Social Sciences of the Open University of Tanzania and lecturers from the University of South Africa (UNISA), taken shortly after a brief meeting focused on exploring potential collaboration in teaching, research, and exchange programs for students and faculty.

    The call was made during a high-level academic dialogue held yesterday at Johari Rotana Hotel in Dar es Salaam and attended by scholars, academics, government officials, private sector representatives, and diplomats from across Africa and beyond.

    Contributing to the discussions, former South African President and current Chancellor of the University of South Africa (UNISA), Dr. Thabo Mbeki, said the concept of the Blue Economy remains poorly understood at a practical level.

    “A large percentage of our people still lack proper knowledge of what the Blue Economy entails. We must therefore prioritize public awareness and education if we want this concept to be well understood and implemented,” Dr. Mbeki emphasized.

    Dr. Dunlop Ochieng, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences at the Open University of Tanzania, stressed that any form of development must take into account how ordinary citizens will benefit.

    “How do we ensure their safety and inclusion? Too often we’ve seen economic initiatives, including foreign investments, where local communities are left to pick up the scraps while the best resources are exported,” he said.

    He also highlighted the strategic importance of resources such as the Nile River to countries like Egypt, questioning whether the Blue Economy is sometimes used more as a buzzword than a development reality.

    Joseph Butiku, Executive Director of the Mwalimu Julius Nyerere Foundation, said Africa needs courageous and visionary leaders who will spearhead efforts to achieve self-reliance in thought and confidence in development pursuits.

    “The Organization of African Unity (OAU) helped liberate African nations from colonial rule. Today, the African Union (AU) must champion economic, political, and social liberation,” Butiku stated.

    He also thanked Dr. Mbeki for choosing Tanzania to host the dialogue that has provided a valuable platform to assess the potential of the Blue Economy and explore strategic ways to harness marine resources for the continent’s economic emancipation.

    Dr. Narriman Jiddawi, a Senior Researcher on marine resources, spoke about the cultural and mindset shifts occurring in Zanzibar, where women are increasingly participating in income-generating activities linked to marine resources, reflecting a growing inclusivity in the Blue Economy.

    The dialogue emphasized the critical role of research, policy integration, and grassroots involvement in ensuring that Africa’s Blue Economy is not just a theoretical concept but a real driver of inclusive growth and sustainable development.