• By Vincent Mpepo

    African countries have been called upon to work together instead of acting alone in the fight against poverty and exploitation. This cooperation would help fulfill the dreams of Africa’s founding leaders, such as Mwalimu Julius Nyerere and Nelson Mandela.

    The call was made during an academic forum held yesterday at Johari Rotana Hotel in Dar es Salaam which was attended by scholars, academics, government leaders, private sector representatives, and diplomats from across Africa and beyond.

    During the forum, Professor Senia Nhamo from the University of South Africa (UNISA) said African nations can gain a lot by joining hands and taking advantage of shared economic opportunities.

    “We can make better use of our resources and trade more with each other if we cut down bureaucracy and remove customs and tax barriers,” said Prof. Nhamo.

    She pointed out that challenges like lack of a single African currency and customs duties need to be addressed. She also encouraged African governments to invest in useful research and urged universities to share research findings with the public instead of keeping them in libraries.

    Dr. Dunlop Ochieng, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences at the Open University of Tanzania said some development projects and investments ignore local people which leads to poor cooperation.

    He said it’s important to include local communities in all development efforts so they are active participants, not just observers in their own land.

    Executive Director of the Mwalimu Julius Nyerere Foundation, Joseph Butiku, said Africa needs strong and continuous leadership to reach its development goals.

    “Africa is falling behind because there is no consistency in planning and following through with priorities when leadership changes,” said Butiku.

    He noted that new leaders often bring in their own priorities and ignore those of past leaders.

    Butiku also thanked former South African President Thabo Mbeki for choosing Tanzania to host the forum, which helped assess the importance of the blue economy adding that the relationship between Tanzania and South Africa goes back to the time of the struggle for independence.

    A researcher from Tanzania’s National Defence College, Dr. Lucy Shule, said African countries must work together at regional and continental levels to drive economic growth.

    She said working in unity brings more strength than working alone.

    On the topic of the blue economy, she stressed the need for African governments to raise awareness about the concept and create policies to protect local communities so they benefit from marine resources.

  • By Vincent Mpepo

    Academics and researchers in African higher learning institutions have been urged to conduct studies that provide practical solutions for the sustainable use of marine resources in order to effectively implement the Blue Economy concept and drive Africa’s economic and social development.

    A group photo of academics from the Faculty of Arts and Social Sciences of the Open University of Tanzania and lecturers from the University of South Africa (UNISA), taken shortly after a brief meeting focused on exploring potential collaboration in teaching, research, and exchange programs for students and faculty.

    The call was made during a high-level academic dialogue held yesterday at Johari Rotana Hotel in Dar es Salaam and attended by scholars, academics, government officials, private sector representatives, and diplomats from across Africa and beyond.

    Contributing to the discussions, former South African President and current Chancellor of the University of South Africa (UNISA), Dr. Thabo Mbeki, said the concept of the Blue Economy remains poorly understood at a practical level.

    “A large percentage of our people still lack proper knowledge of what the Blue Economy entails. We must therefore prioritize public awareness and education if we want this concept to be well understood and implemented,” Dr. Mbeki emphasized.

    Dr. Dunlop Ochieng, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences at the Open University of Tanzania, stressed that any form of development must take into account how ordinary citizens will benefit.

    “How do we ensure their safety and inclusion? Too often we’ve seen economic initiatives, including foreign investments, where local communities are left to pick up the scraps while the best resources are exported,” he said.

    He also highlighted the strategic importance of resources such as the Nile River to countries like Egypt, questioning whether the Blue Economy is sometimes used more as a buzzword than a development reality.

    Joseph Butiku, Executive Director of the Mwalimu Julius Nyerere Foundation, said Africa needs courageous and visionary leaders who will spearhead efforts to achieve self-reliance in thought and confidence in development pursuits.

    “The Organization of African Unity (OAU) helped liberate African nations from colonial rule. Today, the African Union (AU) must champion economic, political, and social liberation,” Butiku stated.

    He also thanked Dr. Mbeki for choosing Tanzania to host the dialogue that has provided a valuable platform to assess the potential of the Blue Economy and explore strategic ways to harness marine resources for the continent’s economic emancipation.

    Dr. Narriman Jiddawi, a Senior Researcher on marine resources, spoke about the cultural and mindset shifts occurring in Zanzibar, where women are increasingly participating in income-generating activities linked to marine resources, reflecting a growing inclusivity in the Blue Economy.

    The dialogue emphasized the critical role of research, policy integration, and grassroots involvement in ensuring that Africa’s Blue Economy is not just a theoretical concept but a real driver of inclusive growth and sustainable development.

  • Na Annamaria John

    Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji na Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) zimesaini mkataba ili kutekeleza Mradi wa Uhifadhi wa Maeneo Oevu na Baioanuwai ya Kidakio cha Katuma, Mpanda.

    Mradi wa IKI Katuma utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitatu kwa gharama ya kiasi cha Euro 4,000,000.00 zitakazotolewa na Serikali ya Ujerumani.

    Lengo la mradi IKI Katuma ni kuzijengea uwezo taasisi mtambuka za Sekta ya Maji katika kuimarisha ushirikiano na kubadilishana maarifa ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za maji ili kuhakikisha huduma za mifumo ya ikolojia zinatumika kwa maendeleo endelevu.

  • Na Gloria Maganza, Dodoma

    Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amesema katika Kipindi cha miaka minne ya serikali   imefanikiwa kupunguza mrundikano wa wafungwa na mahabusu kwenye magereza hapa nchini ambapo amesema magereza hapa nchini zina uwezo wa kuchukua wafungwa na mahabusu 28,000 nchi nzima.

    Waziri Dkt. Ndumbaro ametoa taarifa hiyo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Wizara yake katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita Jijini Dodoma.

    Alisema kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC) jumla ya halmashauri 180, kata 1,907 na vijiji/mitaa 5,702 zilifikiwa na jumla ya wananchi milioni 2,698,908 walifikiwa na kupata elimu na huduma za kisheria kupitia mikutano ya ana kwa ana.

     Lalisema Wizara kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekamilisha uhakiki wa mwisho wa Sheria Kuu 300 kati ya 446 zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili.

    “Hii ni sehemu ya jitahada za serikali katika kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria na kuimarisha misingi ya utoaji haki” alisema Dkt. Ndumbaro.

    Alisema mashauri yenye umri mrefu mahakamani ni 2,780 sawa na asilimia 4 ya mashauri yote yaliyobaki mahakamani hivyo, Tanzania ni miongoni mwa nchi chache barani Afrika zenye mrundikano mdogo wa mashauri mahakamani.

    Sanjari na hayo, Waziri Dkt. Ndumbaro amesema mahakama inafanya utaratibu wa  kutumia mfumo wa kutafsiri katika mahakama zote zenye miundombinu ya mtandao (intaneti) nchini ili kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati na gharama nafuu.

  • Na Vincent Mpepo

    Wanataaluma na watafiti katika taasisi za elimu ya juu barani Afrika wametakiwa kufanya tafiti zitakazotoa majawabu ya matumizi endelevu ya rasilimali za bahari barani humo ili kutekeleza  dhana ya uchumi wa bluu kwa vitendo na tija katika kuchochea uchumi na maendeleo ya Afrika.

    Wito huo umetolewa na washiriki katika mjadala wa kitaaluma uliofanyika leo katika ukumbi wa Hotel ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wasomi, wanataaluma viongozi wa serikali, taasisi binafsi na wanadiplomasia wa ndani na nje ya Afrika.

    Akizungumza wakati akichangia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mjadala huo, Rais Mstaafu na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afrika Kusini (UNISA), Dr. Thabo Mbeki alisema bado kuna changamoto ya kueleweka kwa dhana ya uchumi wa bluu kivitendo.

    “Asilimia kubwa ya watu wetu bado hawana maarifa sahihi kuhusu uchumi wa bluu na kwamba hatuna budi kuwaelimisha ili uchumi wa bluu ufahamike”, alsiema Rais Mstaafu Mbeki.

    Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt.Dunlop Ochieng alisema kutokana na mjadala huo mojawapo ya vitu vya msingi ambavyo utekelezaji wa aina yoyote ya maendeleo unapaswa kuzingatia ni kuwaangalia wananchi wa kawaida watafaidikaje.

    “Tunawekaje mazingira ya usalama wao kwani tumeona mara kadhaa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi ikiwemo uwekezaji wananchi wamekuwa ni walaji wa mabaki na vinono vikisafirishwa kwenda nje”, alisema Dkt.Ochieng.

    Alisema tunafamu umuhimu wa Mto Nille kwa nchi ya Misri na kwamba dhana ya uchumi wa bluu wakati mwingine ni msamiati tu.

    Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku alisema Afrika inahitaji vinara watakaofanya kazi mstari wa mbele ili kuhakikisha malengo ya kujikomboa kifikra na kujiamini yanatimia.

    “OAU imesaidia nchi za Afrika kupata Uhuru wake lakini kwa sasa AU na Afrika ya sasa ni kulikomboa Bara hilo katika nyanya zote za kiuchumi, kisiasa na kijamii”, alisema Butiku.

    Aidha alimshukuru Rais Thabo Mbeki kwa kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa mjadala huo uliosaidia kufanya tathimini ya thamani ya uchumi wa bluu katika bara la Afrika na kuanisha mikakati ya kutumia rasilimali za bahari kujikomboa kiuchumi.

    Kwa upande wake, Mtafiti Mwandamizi wa masuala ya rasilimali za bahari, Dkt. Narriman Jiddawi alielezea mabadiliko ya kiutamaduni na kifikra yanayoonesha kukua kwa ushiriki wa wanawake wa Zanzibar kwenye uchumi wa bluu na kwamba wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kujipatia kipato zinazoambatana na rasilimali za bahari.

  • Na Gloria Maganza, Dodoma

    Madereva wa magari ya serikali mkaoni Dodoma wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa kwa ajili ya usalama barabarani wanapokuwa wakiendesha magari hayo.

    Rai hiyo imetolewa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), George Katabazi wakati akizungumza na madereva hao kwenye kikao maalumu alichokiitisha katika ukumbi wa Polisi jamii Jijini Dodoma kilicholenga  kuzungumza nao juu ya utii wa sheria za usalama barabarani kwani baadhi yao wamekuwa wakilalamikiwa kukiuka sheria hizo.

    “Kikubwa ni kuwataka madereva wa serikali kuzingatia sheria na taratibu zinazohusiana na usalama barabarani”, alisema Kamanda Katabazi.

    Alisema Jeshi lake limekusudia kuwakumbusha na kuwaelimisha kuhussu sheria hizo, taratibu na kanuni lakini pia kuwaonya baadhi yao ambao hawazingatii sheria hizo kwa makusudi hivyo kuhatarisha usalama wao na wengine.

    Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Serikali, Issa Kisebengo alisema elimu waliyoipata kwenye kikao hicho imewasaidia kutambua majukumu na wajibu wao kwenye utumishi wa umma na kutoa wito kwa madereva wenzake kuzingatia yale yote waliyofundishwa.

    “Sisi ni vioo kwa madereva wengine lakini pia tunabeba watumishi wa serikali na kuna watumiaji wengine wa barabara na wote hao wanatutegemea sisi kwa usalama wao hivyo, mafunzo tuliyoyapata tutaenda kuyafanyia kazi”, alisema Kisebengo.

    Sanjali na kukumbushwa sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani kikao hicho pia kiliambatana na mafunzo mbalimbali yaliyotolewa kwa madereva hao ili kuendelea kuwakumbusha sharia hizo kwani kuwa madereva wa magari ya serikali si kigezo cha kuvunja sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa.

  • Na Vincent Mpepo

    Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dkt. Mwatumai Mwanjota amewataka wanaume kutokwepa wajibu kwa familia zao katika masuala mbalimbali ya kiimani ikiwemo kuhudhuria na waume zao kwenye huduma na sakramenti muhimu.

    Hayo ameyasema leo baada ya ubatizo wa watoto katika Mtaa wa Kwembe na kwamba anakerwa na baadhi ya wanaume kuwaacha wake zao kwenda ibadani kwa ajili ya ubatizo wa watoto wao huku akihoji umuhimu wa shughuli walizoenda kufanya ambazo ni zaidi ya tukio kama ubatizo.

    “Ubatizo ni kitu chenye thamani sana na alihoji kwa nini wapange safari siku ya ubatizo?”, alihoji Mchungaji Dkt. Mwanjota.

    Alisema ikiwa kuna matatizo ya kuumwa mpaka kulazwa walao hapo wataeleweka vinginevyo wanakwepa wajibu wao kama wazazi na viongozi wa familia.

    Aidha aliwataka akina mama hao wakaombe msamaha na kutengeneza na waume zao ikiwa kuna hitilafu ili mambo yawe mazuri kwa wakati ujao.

    Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava akihubiri kwa kutumia maandiko kutoka kitabu Zaburi alisema ni kitabu chenye hazina kubwa ndani yake kwa kuwa unaweza kutunga nyimbo ukaimba, ukasifu na kushangilia ukuu wa Mungu.

    Alisema kila kiumbe hakina budi kumsifu Mungu kwa kuwa ndiye aliyekipa uhai na uwepo wake hapa duniani.

    “Kila kiumbe kina namna ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya uumbaji wake ndio maana vitu kama Jua na Mwezi vinamsifu Mungu”, alisema Mwinjilisti Mzava.

    Alisema mwadamu anapaswa kuimba wimbo mpya kila siku kwa kuwa ndiye aliyempa uhai na kwamba kuimba ni sehemu ya kushukuru na moyo unaoweza kushukuru ni ule uliojaa shukrani.

    “Kama unaweza kumsifu mwanadamu ikiwa amekufanyia jambo fulani jema, je Mungu si zaidi ya mwanadamu?”, alisema Mwinjilisti Mzava.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Ujenzi Mtaani hapo, Exaud Mchome akitoa mwendelezo wa kazi ya ujenzi wa kanisa alisema kazi ya uwekaji bati inaendelea licha ya kusimama kutokana na hali ya hewa.

    Aliwakumbusha washarika kuendelea kumtolea Mungu ili kufikia malengo kwa awamu ya kwanza ya January hadi Juni kwa kiasi walichokubaliana.

    “Roho ya kupenda ikusukume ufanye jambo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Bwana”, alisema Mchome.

    Ibada ya leo siku ya nne baada ya Pasaka kiliturujua ni maalumu kwa ajili ya uimbaji ikitambulika kwa jina na la ‘Domino Kantate’ na mtaani Kwembe ilipamwa na kwaya mbalimbali za mtaani hapo lakini pia uwepo wa Kwaya Kuu ya Umoja kutoka Mtaa wa Malamba Mawili ulinogesha na kufanya iwe siku ya Baraka tele.

    Kwaya Kuu ya Umoja kutoka Mtaa wa Malamba Mawili ikihudumu katika ibada ya Leo, Siku ya nne baada Pasaka katika Mtaa wa Kwembe.

    Sanjali na hilo huduma mbalimbali za kichungaji ikiwemo ubatizo, meza ya bwana na kuweka wakfu kwa vifaa vilivyoletwa kanisani kwa ajili ya kazi ya Mungu zilifanyika.

  • Na Cartace Ngajiro

    Umoja wa Wanawake Wanaofanya kazi Sekta ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) wametembelea Bandari ya Tanga na kuridhishwa  na utendaji kazi katika bandari hiyo baada ya kukamilika kwa mradi wa maboresho ya bandari.

    Akiongea wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Umoja huo Mhandisi Fortunata Makoye Kakwaya alisema maboresho hayo yameleta mapinduzi makubwa katika bandari hiyo ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo meli kubwa zilikuwa haziwezi kufunga gatini kutokana na changamoto ya kina cha maji kuwa kifupi.

    “Kama wadau katika sekta ya bahari tunapongeza kwa maboresho haya kwa kuwa yameleta mapinduzi makubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kuifanya bandari hii ikidhi viwango vya kimataifa katika kuhudumia meli na mizigo”, alisema Mhandisi Kakwaya.

    Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Bandari, Afisa Mkuu anayeshughulikia utekelezaji Gwakisa Mwaibuji aliwataka wadau hao kuwa mabalozi wazuri wa Bandari ya Tanga ili bandari hiyo iendelee kupokea shehena kubwa zaidi na mapato makubwa.