• Washiriki wa tathimini ya mafunzo kwa vitendo unaohusisha wahadhiri, wakufunzi na wanafunzi wa Tanzania na Norway uliofanyika jana katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Picha na Vincent Mpepo, OUT).

    Na Vincent Mpepo, OUT

    Utekelezaji wa mradi wa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Chuo cha Ualimu Elimu Maalumu Patandi na vyuo vikuu vya Norway umeonesha mafanikio chanya ya namna watoto wenye mahitahji maalumu wanavyoweza kusaidiwa ili kuboresha maisha yao.

    Hayo yamebainishwa na washiriki wa mjadala wa tathimini ya mafunzo kwa vitendo unaohusisha wahadhiri, wakufunzi na wanafunzi wa Tanzania na Norway uliofanyika leo katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania huku mafaniko na changamoto kadhaa zikiainishwa ili kufikia malengo ya mradi huo.

    Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Dunlop Ochieng alisema ushirikano huo umeleta mafaniko chanya na kwamba chuo chake kinathamini juhudi na mchango wa ushirkiano huo unaolenga kuboresha maarifa na ujuzi wa namna ya kuwadumia watoto wenye mahitaji maalumu.

    “Ninatambua kazi nzuri inayofanyika katika shule za Uhuru Mchanganyiko na Sinza Maalumu”, alisema Dtk.Ochieng.

    Alisema utekelezaji wa makubaliano ya mradi huo yanaenda sambamba na matakwa ya mikataba ya kimataifa na sheria za nchi kuhusu haki za watoto na watu wenye ulemavu.

    Alisema ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizo umesaidia kuwapa wahadhiri na wanafunzi wa kitanzania na Norway jukwaa la kutekeleza kwa vitendo wakifundishacho na kusoma darasani katika mazingira halisi ya jamii kwa pande zote mbili.

    Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Mariana Makuu alisema ushirikano huo unasaidia kupatikana kwa suluhu za changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wa kuwahudumia watoto wenye mahitaji maalumu kwa kubadilishana uzoefu kati ya wageni na wenyeji.

    “Kwa kawaida huwa tunafanya tathimini ili kuona kama wahusika wameweza kutekeleza malengo ya mradi na ikiwa kuna changamoto tuone namna ya kutatua ili malengo ya mradi yafanikiwe”, alisema Dkt.Makuu.

    Aidha alisema bado kuna umuhimu wa uwepo wa maafisa ustawi wa jamii kwenye shule za msingi na sekondari ili wasaidiektika utoaji huduma kwa watoto kwa kuwa walimu wana majukumu ya kutekeleza mtaala na hawezi kuangalia ustawi wa watoto kwa undani.

    Mkufunzi wa Chuo cha Ualimu Elimu Maalumu Patandi, Leah Makundi alisema kutokana na ushiriki wake kwenye mradi huo amejifunza vitu vingi ikiwemo mbinu mbadala za kuwafundisha walimu wanafunzi bila kuwaadhibu watoto.

    “Wametusaidia namna mbalimbali mbadala za kuepuka matumizi ya fimbo kama njia pekee ya kumuonya na kumuelekeza mtoto”, alisema Bi Makundi.

    Alisema wao wanatamani na wanajitahidi sana sisi tufundishe walimu waache kuwachapa watoto na tutumie mbinu mbadala katika kufundisha.

    Mwakilishi wa wanafunzi kutoka Norway, Erlend Hoibo alisema uwepo wao nchini Tanzania wamejifunza vitu vingi ikiwemo namna walimu wanavyotumia rasilimali kidogo walizonazo ili kufundisha watoto wenye mahitaji maalumu kitu ambacho kinaonesha upendo na kujali.

    “Nafikiri wanahitaji kupata usaidizi na serikali iajiri maofisa ustawi wa jamii ili kurahisha kazi za walimu za kutoa huduma stahiki kwa watoto hao”, alisema Hoibo.

    Aidha, alisema amefurahishwa na namna watoto wenye mahitaji maalumu na wasio na mahitaji  maalumu wanavyosaidiana bila ya kujali aina ya ulemavu walionao kitu kinachodhihirisha upendo, kujali na uwajibikaji wa kila mmoja kwa mwenzie.

    Kwa mujibu Mkufunzi katika Idara ya Ustawi wa Jamii ya Chuo kikuu Huria cha Tanzania, Fauzia Kitenge tathimini hiyo inahusisha wanafunzi waliopo Tanzania kutoka Norway wanaotoa mrejesho wa shughuli za mafunzo kwa vitendo katika shule tano za Dar es salaam na Arusha.

    “Kwa Dar es salaam ni shule za Uhuru Mchanganyiko na Sinza Maalumu wakati kwa Mkoa wa Arusha ni Shule za Msingi na Sekondari za Patandi na Kiloleni”, alisema Bi Fauzia.

    Alisema shughuli za mafunzo kwa vitendo zitahusisha makongamano katika shule hizo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo ulinzi wa watoto, haki za watoto na mengine ambayo yenye msalahi kwa ustawi wa watoto.

  • Participants of NOREC Project involving lecturers, trainers, and students from Tanzania and Norway held today at the Open University of Tanzania. During the discussion, successes and challenges were outlined in order to achieve the goals of the project. (Photo by Vincent Mpepo, OUT)

    By Vincent Mpepo, OUT

    The implementation of a partnership project between the Open University of Tanzania, Patandi Special Education Teachers College and universities from Norway has demonstrated positive outcomes in assisting children with special needs to improve their wellbeing.

    This was highlighted during a practical training assessment discussion involving lecturers, trainers, and students from Tanzania and Norway which took place today at the Open University of Tanzania whereby achievements and challenges in achieving the project goals were identified.

    Speaking during the official opening of a two days practical training assessment workshop, Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences of the Open University of Tanzania, Dr. Dunlop Ochieng said the collaboration has yielded positive results as it is aiming in enhancing knowledge and skills in supporting children with special needs.

    “I acknowledge the good work being done at Uhuru Mchanganyiko and Sinza Maalumu schools, said Dr.Ochieng.

    He said the project’s execution aligns with international agreements and national laws with regard to the rights of children and people with disabilities.

    He said the partnership between the institutions has helped provide Tanzanian and Norwegian lecturers and students with practical opportunities to apply what they are teaching and learning in real-world community settings on both sides.

    Head of the Department of Sociology and Social Work of the Open University of Tanzania, Dr. Mariana Makuu, said the collaboration has helped in identifying solutions to challenges in serving children with special needs by exchanging experiences between local and foreign participants.

    “We usually conduct assessments to see if the project’s goals have been met and to identify challenges so that we can find ways to resolve them to ensure the project succeeds,” said Dr. Makuu.

    She also highlighted the importance of having social workers in primary and secondary schools that will assist in children’s welfare services as teachers have the responsibility to implement the curriculum and cannot fully address children’s well-being.

    A tutor from Patandi Special Education Teachers College Leah Makundi, said the partnership has helped her gain experiences and skills towards the use of alternative teaching methods and guiding students without resorting to corporal punishment.

    “They have helped us find alternative ways to guide and direct children without using a stick,” said Makundi.

    She said as tutors they are trying their best to teach teachers to stop beating children instead they are suggesting the use of alternative methods that will help them understand their mistakes and learn trough those mistakes.

    A student from Norway, Erlend Hoibo, said their presence in Tanzania for the time they have served has provided many learning experiences including how teachers make the best use of limited resources to educate children with special needs something which demonstrates care and compassion.

    “I believe they need more support and the government should employ social workers to facilitate teachers’ work in providing appropriate services to the children,” said Hoibo.

    He also admired the cooperation between children with and without special needs and how they assist each other regardless of their disabilities reflecting a sense of love and mutual responsibility.

    According to a trainer in the Department of Sociology and Social Work from the Open University of Tanzania, Fauzia Kitenge, the assessment involves receiving feedback from Norwegian students conducting their practical training activities in five schools located in Dar es Salaam and Arusha.

    “The involved schools are Uhuru Mchanganyiko and Sinza Maalumu in Dar es Salaam while in Arusha, we have Patandi Primary and Secondary schools with and Kiloleni,” said Kitenge.

    She said their practical training activities will include workshops on various topics in the selected schools including child protection, children’s rights and any other issues beneficial to child welfare.

    Assistant lecturers from the Department of Sociology and Social Work of the Open University of Tanzania, Robert Makungu and Asia Namamba, presenting a topic on the importance of Ubuntu philosophy which emphasizes the principles of humanity, compassion, and love among members of the community during a debate on the evaluation of practical training involving lecturers, trainers, and students from Tanzania and Norway, held today at the Open University of Tanzania in Dar es Salaam. (Photo by Vincent Mpepo, OUT).

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe
    Serikali ya Mtaa wa Kwembe imeishukuru serikali kwa namna inavyojali wananchi kupitia uboreshaji wa miundombinu na huduma za afya.
    Hayo yamebainishwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kwembe Rajabu Koba wakati wa mkutano wa wa Kwanza na wa wananchi wa Mtaa huo uliofanyika hivi karibuni katika ofisi za mtaa huo ambapo masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwemo pongezi kwa serikali.
    Koba alisema serikali imetoa pesa ili kufanikisha shughuli mbalimbali za maendeleo katika Mtaa wake na kupitia wataalamu wa sekta mbalimbali mtaani kwake.
    Kwa mujibu wa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Amani, Dkt.Nikodemus Ngwembe alibainisha maboresho mbalimbali yaliyofanyika na yanaendelea kufanyika katika Kituo hicho cha Afya ambayo yanafanya kipandishwe hadhi kutoka Zahanati ili kuendana na hadhi hiyo.
    “Kwa sasa kituo chetu kimejenga jengo la wazazi kwa gharama ya Tsh milioni 300 ambalo lina vitanda 30 huku vitanda vya chumba cha wazazi ni 10 na tunatoa huduma masaa 24”, alisema Dkt. Ngwembe.
    Alisema kwa sasa kituo hicho kinaendelea na ujenzi wa wodi ya upasuaji na kwamba kitahudumia kata ya Kwembe na Kibamba huku mashine na mitambo mingine ikiwemo Utra-Sound ikiwa mbioni kuletwa katika kituo hicho ambayo imegharimu Tsh milioni 22.
    Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kwembe, Lwitiko Mwakisole alisema changamoto kubwa inayoikabili shule yake ni uhaba wa madarasa ya kusomea na madawati ambao hauendani na idadi ya wanafunzi waliopo matokeo yake badhi ya wanafunzi kulazimika kusomea nje na kukaa chini.

    “Shule ya Msingi Kwembe ina wanafunzi zaidi ya 2000 huku miundombinu ya madarasa tuliyonayo ni 12 tu”, alisema Mwalimu Mwakisole.
    Aliwaasa wazazi kutembelea shule yao ili kujionea uhalisia wa kinachosemwa ili waweze kufanya maamuzi sahihi katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo kwa maslahi ya kizazi cha wanakwembe.
    Akizungumzia malezi, Mwakisole alisema kumekuwa na changamoto za malezi katika jamii na familia kutokana na baadhi ya walezi na wazazi kutokubali watoto wao kuadhibiwa suala ambalo linaleta mustakabali mbaya kwa jamii na kizazi cha sasa.
    “Kimsingi, tukubali kuna changamoto za malezi zinazotokana na malezi mabovu katika familia zetu hivyo kusababisha watoto wenye tabia mbaya”, alisema Mwalimu Mwakisole.
    Aliwataka wazazi na walezi wa mtaa huo kushirikiana na walimu ili kuendelea kuboresha tabia na maadili ya watoto kwa faida ya kizazi kijacho na taifa kwa ujumla.
    Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kwembe, Bi Ramla Mustafa aliwakumbusha wananchi wa mtaa huo kuhusu fursa za mikopo asilimia kumi (10%) ambayo hutolewa na serikali kupitia Halmashauri ya Ubungo kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu.
    “Vigezo vya kuapata mikopo hiyo ni mtu mwenye umri wa miaka 18 hadi 45 na mwenye uwezo wa kufanya kazi na kujiingizia kipato”, alisema Bi Ramla.
    Aidha aliwataka Wananchi kutosikiliza maneno ya mtaani badala yake waende ofisini kwa maelezo na maelekezo sahihi.

  • Na Vincent Mpepo, OUT

    Imeelezwa kuwa utekelezaji wa malipo ya mafao sanjali na kikokotoo kwa wastaafu ni matokeo ya tafiti mbalimbali ambazo zilionesha ya ulipaji kidogokidogo badala ya kulipa kwa mkupuo unaweza kusaidia zaidi wastaafu tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

    Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Elimu ya Juu Taifa, Elia Kasalile wakati wa Mkutano Mkuu wa Tawi la chama hicho la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania uliofanyika leo katika ukumbi wa chuo hicho jijini Dar es salaam.

    Alisema matokeo ya tafiti na mapendekezo yalionesha kuwa sehemu kubwa ya wastaafu hawakuwa na uwezo wa kuzitawala pesa zao walizolipwa kwa mkupuo badala yake wengi wao haikuzidi miaka mitatu walimaliza na kuzalisha matatizo mengine ikiwemo kifo.

    Alianisha changamoto nyingine zinazowakabili wastaafu ikiwa ni pamoja na kupungua kwa kiasi cha kipato na idadi ya marafiki hivyo kuwabadilishia mfumo wa mfumo wa maisha ambapo mstaafu asipojiandaa inakuwa janga.

    “Nawakumbusha wanachama kuunga mkono juhudi za chama chetu kupitia programu mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa viwanja vya ujenzi kama njia mojawapo ya dhidi ya majanga ikiwemo kutegemea malipo ya kustaafu kustaafu kujenga”, alisema Kasalile.

    Alisema matokeo ya tafiti yalizingatia vigezo vya kitaifa na kimataifa kupitia shirika la kazi (ILO) yalipendekeza kiwango cha mafao kwa mkupuo kipunguzwe na badala yake pesa hiyo ilipwe kwenye nyongeza ya kila Mwezi.

    Aidha aliukumbusha uongozi wa chama hicho chuoni hapo kuingia makubaliano na menejimenti ili kupata ada ya uwakala kupitia wafanyakazi wasio wanachama wa chama hicho kwa kuwa ni wanufaika wa juhudu za kulinda na kutetea maslahi mbalimbali.

    Mwenyekiti wa Chama hicho chuoni hapo, Salatiel Chaula alisema chama chake kimeendelea kulinda na kutetea maslahi ya wanachama wake licha ya changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa fedha katika uendeshaji wa chama hicho.

    Kwa upande mwingine, aliushukuru uongozi wa chuo hicho kwa ushirikiano ambao umesaidia katika ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za kulinda na kutetea a ya wafanyakazi.  

    Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Rasilimali watu chuoni hapo, Bi Joyce Kimati aliwakumbusha wafanyakazi kufuata sheria, taratibu na kanuni za kazi ikiwemo kujaza taarifa za kazi na majukumu yao katika mfumo wa Usimamizi na Utendaji kazi katika utumishi wa Umma (PEPMIS) kwani kutokufanya hivyo ni kujiletea matatizo.

  • Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa wa Kwembe, Emeline Mzava na Mtendakazi Anna Mauki pamoja na wanakwaya wa kwaya hiyo wakifurahia jambo wakati wa uzinduzi wa Albamu ya kwanza ya Kwaya Kuu ya Mtaa huo Siku ya Jumapili, (Picha na Vincent Mpepo).

    Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Viongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe wamewashukuru washarika wa Mtaa huo kwa namna wanavyojitoa katika kazi ya Mungu.

    Shukrani hizo zimetolewa na viongozi hao wakati wa ibada ya Jumapili katika vipindi mbalimbali huku wakitanabaisha kwamba wanajisikia amani kufanya kazi katika Mtaa huo.

    Akizungumza wakati wa ahadi za changizo za ujenzi wa kanisa unaoendelea Mtaani hapo, Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava alisema anawiwa kumshukuru Mungu kwa ajili ya washarika hao kwa namna wanavyojitoa katika shughuli mbalimbali kanisani hapo na zaidi anawaombea ili utumishi wao uendelee.

    “Sina cha kusema zaidi ya kumshukuru Mungu kwa ajili yenu,” alisema Mwinjilisti Mzava.

    Aidha aliwakumbusha washarika wa mtaa huo kuhusu changizo la ujenzi wa nyumba ya watoto wenye mahitaji maalumu huko Kitopeni-Bagamoyo ambayo inahamishwa kutoka Mtoni kijichi.

    Akiongezea uzito wa kauli hiyo, Mtendakazi wa Mtaa huo Anna Mauki alisema anaguswa na namna washarika wanavyowajibika.

    Aidha katika mahubiri yake alizungumzia umuhimu wa neno la Mungu sawa na silaha ambayo hutumika kujilinda dhidi ya adui akisimamia kichwa kisemacho ‘Neno ni Silaha Imara’ na kwamba neno la Mungu ni pumzi inayoishi na imeandikwa kwa watu ambao wamepewa uwezo na Mungu.

    “Tuanze kuliishi neno katika familia zetu kwa kusali pamoja asubuhi, mchana na usiku,” alisema Mtendakazi Anna.

    Alisema kuwafundisha watoto neno Mungu ni urithi mkubwa zaidi ya aina ya urithi mwingine kwakuwa mtu akijawa na wingi wa neno la Mungyu atapata kibali na kukubalika katika mazingira ambayo kibinadamu asingeweza.

    “Wakati mwingine tumekuwa na mashaka kuhusu utendaji wetu kwa baadhi ya vitu jambo muhimu ni kuamini kuwa aliyetupa uhai ndiye anayetuwezesha,” alisema Bi Anna.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Mtaa huo, Exaud Mchome aliwashukuru washarika kwa kuendelea na michango kwa ajili ya ujenzi na alitangaza kuanza kwa awamu ya uchangiaji kwa kwanza ambayo ni Februari mpaka Mei na awamu ya pili itaanza Mwezi Juni hadi Disemba 2025.

    Baadhi ya Wafadhiri wa Kwaya Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe wakiunga mkono kwa kununua albamu ya Kwanza ya Video ya kwaya hiyo Jumapili, (Picha na Vincent Mpepo).

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila kimewataka Wananchi wa Kwembe na maeneo jirani kuchangamkia fursa ya kambi maalumu ya kupima afya bure ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Elimu ya Juu kwa mageuzi ya kichumi (HEET).

    Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kwembe Rajabu Koba wakati wa mkutano wa wa kwanza na wa wananchi wa Mtaa huo uliofanyika jana katika ofisi za mtaa huo ambapo masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwemo suala la kambi hiyo maalumu itakayofanyika Tarehe 26-27 Februari 2025 kuanzia Saa 03:00 asubhi mpaka saa 10:00 alasiri.

    Koba alisema chuo hicho kimewajulisha kuhusu kambi hiyo na kuwataka wananchi kuitumia fursa hiyo ili kufanya uchunguzi wa afya zao.

    Kwa mujibu wa taarifa hiyo imetaja huduma kadhaa zitakazolewa ikiwemo uchunguzi wa awali wa magonjwa ya macho, masikio, pua na koo.

    “Huduma nyingine ni pamoja na uchunguzi wa kinywa na meno, saratani ya matiti na shingo ya kizazi, homa ya ini na tezi dume kwa kipimo cha damu”, imenukuliwa taarifa hiyo.

    Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa kutakuwa na elimu kwa umma kuhusu madhara yanayotokana na matumizi ya dawa na usugu wa dawa, magonjwa ya kuambukizwa, lishe na uchakataji wa taarifa kwa kutumia akili mnemba.

    “Wananchi watapata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wataalamu kutoka famasia na tiba asilia”, ilisema taarifa hiyo.

    Wakati huohuo, Koba aliwataka wananchi wa Mtaa huo kuchangamkia fursa za ujasiriamali katika mradi mkubwa unaotarajiwa kuanza hivi karibuni katika eneo la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.

    “Wanacnhi wa maeneo jirani wajiandae kwa kazi mbalimbali ikiwemo vibarua na ujasiriamali kama mama lishe katika mradi huo”, alisema Koba.

    Alisema fursa hizo ni matokeo ya utekelezaji wa Mradi wa Elimu ya juu kwa Mageuzi ya Kichumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unahusisha ujenzi wa majengo sita ambapo tayari kandarasi zimekwishatolewa kwa makampuni mawili na utagharimu kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 30.5.

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Wataalamu mbalimbali wanaoishi na kufanya kazi katika Mtaa wa Kwembe Ubungo Jijini Dar es salaam wamebainisha fursa na changamoto mbalimbali za kimaendeleo katika Mtaa huo huku huduma za jamii na miundombinu zikitajwa.

    Hayo yamejitokeza katika mkutano wa kwanza wa serikali ya Mtaa uliofanyika jana katika ofisi za mtaa huo jana huku fursa na changamoto mbalimbali zikitajwa katika kuchochoea au kurudisha nyuma maendeleo ya Mtaa huo.

    Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kwembe Rajabu Koba alisema ni wakati sasa Wananchi kuamka kuunganisha nguvu zao, kwa kuishauri serikali yao kwa hoja madhubuti ili kwa ushirikiano zifanyiwe kazi kwa manufaa ya Mtaa huo.

    Alitaja vipaumbele vya serikali yake kuwa ni pamoja na ujenzi wa Shule ya Msingi Kwembe ili kupunguza mrudikano wa watoto katika madara yaliyopo ambayo hayatoshi na Kituo cha polisi ili kuimarisha ulinzi na usalama.

    “Vipaumbele vingine ni pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama kupitia ulinzi shirikishi, kubadili matumizi ya eneo la soko kuwa machinjio na mnada wa mifugo”, alitaja Koba.

    Aliongeza vipaumbele vingine kuwa ni kukamilisha ujenzi wa ofisi ya serikali ya Mtaa huo na masuala ya urasimishaji ardhi katika Mtaa huo.

    Akizungumzia ajenda ya ulinzi na usalama aliwataka Wananchi kwenye mitaa na zone mbazo bado hazijaanzisha ulinzi shirikishi kufanya hivyo ili kutowapa wezi na wadokozi fursa ya kuwaibia.

    “Ulinzi shirikishi ni kwa ajili ya kuwanyima fursa wezi na wadokozi kujipatia kipato au faida kwa kazi isiyo halali”, alisema Koba.

    Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kwembe, Lwitiko Mwakisole alisema changamoto kubwa inayoikabili shule yake ni uhaba wa madarasa ya kusomea na madawati ambao hauendani na idadi ya wanafunzi waliopo matokeo yake bbadhi ya wanafunzi kulazimika kusomea nje na kukaa chini.

    “Shule ya Msingi Kwembe ina wanafunzi zaidi ya 2000 huku miundombinu ya madarasa tuliyonayo ni 12 tu”, alisema Mwalimu Mwakisole.

    Aliwaasa wazazi kutembelea shule yao ili kujionea uhalisia wa kinachosemwa ili waweze kufanya maamuzi sahihi katika kuboresha miundombinu ya shule hiyo kwa maslahi ya kizazi cha wanakwembe.

    Akizungumzia malezi, Mwakisole alisema kumekuwa na changamoto za malezi katika jamii na familia kutokana na baadhi ya walezi na wazazi kutokubali watoto wao kuadhibiwa suala ambalo linaleta mustakabali mbaya kwa jamii na kizazi cha sasa.

    “Kimsingi, tukubali kuna changamoto za malezi zinazotokana na malezi mabovu katika familia zetu hivyo kusababisha watoto wenye tabia mbaya”, alisema Mwalimu Mwakisole.

    Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Amani, Dkt.Nikodemus Ngwembe aliwataka Wananchi wa mtaa huo na mitaa ya jirani kukitumia kituo hicho ambacho kinapandishwa hadhi na kuwa Kituo cha Afya kutoka Zahanati kwa kuwa mindombinu inaboreshwa ili kuendana na hadhi hiyo.

    “Kwa sasa kituo chetu kimejenga jengo la wazazi kwa gharama ya Tsh milioni 300 ambalo lina vitanda 30 huku vitanda vya chumba cha wazazi ni 10inatoa huduma masaa 24 na ina vitanda 10”, alisema Dkt. Ngwembe.

    Alisema kwa sasa kituo hicho kinaendelea na ujenzi wa wodi ya upasuaji na kwamba kitahudumia kata ya Kwembe na Kibamba huku mashine na mitambo mingine ikiwemo Utra-Sound ikiwa mbioni kuletwa katika kituo hicho ambayo imegharimu Tsh milini 22.

    Akizungumzia masuala ya urasimishaji ardhi katika Mtaa huo, Mkandarasi Demetrius Sangu alisema tangu zoezi hilo lianze tayari wameshatambua viwanja 4015 na viwanja vilivyopangwa kwa mujibu wa ramani ya mipango miji ni 6207 wakati viwanja vilivopata namba za ploti ni 2116 wakati ni viawanja 20 pekee ambavyo bado havijapandwa mawe.

    “Changamoto za kuendelea na zoezi hili ikiwemo upandaji wa mawe unatokana na uhaba wa fedha”, alisema Mkandarasi Sangu.

    Aidha, uchunguzi uliofanywa na mwandishi umebani kuwa kuchelewa kwa zoezi la urasimishaji kumetokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuzorota kwa uchangiaji wa fedha kwa wananchi kutokana na kukosa hamasa au matamko mbalimbali ya serikali kwa nyakati zilizopita.

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Eneo ambalo lililopangwa kutumika kama soko limebadilishwa matumizi na kuwa machinjio na mnada wa mifungo kitu kinachotajwa kitaongeza idadi ya wasafiri kuja na kutoka mtaani hapo na kuchochea maenedeleo ya Mtaa wa Kwembe Ubungo jijini Dar es salaam.

    Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Kwembe Rajabu Koba wakati wa mkutano wa wa kwanza wa wananchi uliofanyika jana katika ofisi za mtaa huo ambapo masuala mbalimbali yalijadiliwa huku kubadili matumizi kwa eneo la soko na urasimishaji ardhi zikiwa ni ajenda ambazo zilivuta makini ya wananchi wa mtaa huo.

    Koba alisema maamuzi ya kubadili matumizi ya eneo hilo kuwa machinjio na mnada limefikiwa kufuatia vikao na kamati mbalimbali za mtaa huo na limewasilishwa kwa diwani ili kwenda kwenye ngazi za juu kwa maamuzi zaidi na kwamba tangu lilipofanywa kama soko hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

    Alisema maamuzi ya kubadili eneo matumizi limezingatia vitu vingi ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ambayo itavutia wafanyabiashara ya usafirishaji kama daladala kuja na kutoka kutokana na abiria wakakaokuja kwa shughuli mbalimbali za kibiashara.

    “Ili kupata abiria wa kutosha lazima kuwe na eneo ambalo litavuta watu kuja na kutoka huku pia miundombinu yetu ikiwa imeboreshwa”, alisema Koba.

    Aidha aliwataka wananchi wa Mtaa huo kuchangamkia fursa za ujasiriamali katika mradi mkubwa unaotarajiwa kuanza hivi karibuni katika eneo la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) kampasi ya Mloganzila.

    “Wanacnhi wa maeneo jirani wajiandae kwa kazi mbalimbali ikiwemo vibarua na ujasiriamali kama mama lishe katika mradi huo”, alisema Koba.

    Alisema fursa hizo ni matokeo ya utekelezaji wa Mradi wa Elimu ya juu kwa Mageuzi ya Kichumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unahusisha ujenzi wa majengo sita ambapo tayari kandarasi zimekwishatolewa kwa makampuni mawili na utagharimu kiasi cha dola za kimarekani milioni 30.5.

    Mtendaji wa Mtaa huo, Kennedy Kuwendwa alisema Wananchi wa mtaa huo wajenge utaratibu wa kwenda ofisini ili kupata taarifa sahihi na kutoa taarifa mbalimbali kwa kero ili zifanyiwe kazi badala ya kupeana maneno mitaani ambayo wakati mwingine hayana uhakika.

    “Ninawashukuru Wananchi wa mtaa huu na nitoe rai ikiwa kuna jambo hulielewi njoo ofisini utasaidiwa kupata ufumbuzi”, alisema Kennedy.

    Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kwembe, Bi Ramla Mustafa aliwakumbusha wananchi wa mtaa huo kuhusu fursa za mikopo asilimia kumi (10%) ambayo hutolewa na serikali kupitia Halmashauri ya Ubungo kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu.

    Vigezo vya kuapata mikopo hiyo ni mtu mwenye umri wa miaka 18 hadi 45 na mwenye Uwezo wa kufanya kazi na kujiingizia kipato, alisema Bi Ramla.

    Mkutano huo ulikuwa na ajenda nyingine ikiwemo ujenzi wa Shule ya Msingi Kwembe, Ujenzi wa Kituo cha Polisi, Suala la Ulinzi Shirikishi na umaliziaji wa ofisi ya mtaa huo.

    Hata hivyo uchunguzi wa mwandishi umebaini kutokuwepo kwa hamasa ya kutosha ya Wananchi kushiriki katika mikutano ya mtaa huo suala linalotajwa limetokana na taarifa kutowafikia Wananchi.

  • Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni (kushoto). Kulia ni Katibu wa Baraza Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli ( PURA) Ebeneza Mollel wakati wa Kikao cha Baraza hilo kilichofanyika hivi karibuni mkoani Morogoro.

    Morogoro

    Serikali imeitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kuendelea kuvutia  uwekezaji katika vitalu vilivyo wazi vya mafuta na gesi asilia ili kuongeza kiasi cha nishati hiyo nchini.

    Kauli hiyo ilitolewa mwanzoni mwa wiki na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga wilayani Morogoro, Mkoa wa Morogoro wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) kilicholenga kujadili  mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa mwaka  wa fedha 2025/26.

    Alisema mamlaka hiyo ikifanikiwa kuvutia wawekezaji wa utafutaji wa mafuta na gesi nchi itaongeza ugunduzi wa rasilimali hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na kufikia futi za ujazo wa gesi  inayopatikana nchini.

    “Mkiendelea kuvutia uwekezaji kupitia Duru ya Tano ya kunadi vitalu itakayozinduliwa mwezi Machi mwaka huu pamoja na faida zilizopo mtakuwa mmeendeleza jitihada za serikali kuifungua Tanzania kiuchumi na kuvutia uwekezaji zaidi”, Alisema Kapinga.

    Alisema wizara inatambua umuhimu wa tukio la Duru ya Tano ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini pamoja na kutambua kazi kubwa ambayo imekwishafanyika kuelekea uzinduzi wa tukio hilo muhimu.

    “Kwa muda mrefu tumekuwa tukizungumzia ugunduzi wa futi za ujazo trilioni 57.54 pekee wakati umefika ili kuongeza ugunduzi wa rasilimali hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa”,Alisema Kapinga

    Aidha, aliupongeza uongozi wa uongozi wa PURA kwa kuendelea kuwashirikisha watumishi wake katika kujadili, kupanga na kupitisha mipango na bajeti ya taasisi hiyo kwa uwazi kupitia baraza hilo ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya Majadiliano ya Pamoja katika Utumishi wa Umma.

    Alisema kufanyika kwa vikao hivyo ni ishara tosha ya utawala bora mahala pa kazi kwa kuwa watumishi wanapata fursa ya kuchangia mawazo yao kuhusu uendeshaji wa taasisi hivyo kuendelea kuwa ni sehemu muhimu ya taasisi.

    Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni, alisema duru ya tano (5) ya kunadi vitalu vya utafutaji wa mafuta na

    gesi asilia nchini inatarajiwa kuzinduliwa mwezi Machi, 2025 Jijini Dares salaam wakati wa Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki (EAPCE’25).

    Alisema PURA itaendelea kusimamia na kudhibiti shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa gesi asilia katika vitalu mbalimbali nchini ili kuhakikisha watanzania wazawa wanashirikishwa kikamilfu kwenye miradi mbalimbali ya mkondo wa juu wa petroli nchini.

    Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga (katikati) katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli( PURA) wakati wa Kikao cha Baraza hilo kilichofanyika Tarehe 18 na 19 Februari 2025, mkoani Morogoro. Kushoto Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mhandisi. Charles Sangweni.