• Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Thomas Apson akiongea na waandishi wa habari katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo la ofisi za madini Mkoa wa Singida Mei 15, 2024

    Na Sylvester Richard-Singida

    Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Thomas  Apson amesema serikali itaendelea kushirikiana na waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida ili kulinda na kukuza demokrasia nchini ikiwa ni namna ya kuhakikksha kuwa  wananchi watapata taarifa kuhusu nini serikali yao ili kuharakisha maendeleo kupitia vyombo vya habari.

    Apson  aliyasema hayo Mei 15, 2024 wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari kwa Mkoa wa Singida yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano jengo la ofisi za madini Mkoani hapo.

    Alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa wanahabari katika kukuza uchumi wa Taifa na wa Mtu mmoja mmoja na ndiyo maana imetoa uhuru kwa wanahabari kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya kazi za pamoja na sheria zilizowekwa.

    Alisema  uhuru huo wa vyombo vya habari umeenda sambamba na uhuru wa kufanyika kwa mikutano ya hadhara, vikao na maandamano kwa vyama vyote vya siasa ambapo wanahabari wamekuwa wakiandika habari juu ya mikutano hiyo yenye lengo la kuikosoa na kuishauri serikali iliyopo madarakani.

    Mwenyekiti wa Klabu ya wanahabari Mkoa wa Singida (SINGPRESS, Elisante John akitoa taarifa ya Klabu kwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari Mkoa wa Singida.

    Mwenyekiti wa Klabu ya wanahabari Mkoa wa Singida ( SINGPRESS) Elisante John alisema Klabu hiyo ilianzishwa Julai 16, 2023 kwa lengo la kuwaunganisha wanahabri  wa Mkao  huo ili kufanya kazi chini ya mwamvuli mmoja unaoongozwa na katiba ya Klabu.

    Alisema Klabu hiyo ina malengo ya kukuza demokrasia katika jamii kupitia fursa sawa zinazotolewa na vyombo vya habari kwa kutoa taarifa sahihi katika masuala ya elimu kwa makundi mbalimbali ikiwemo wanawake, watoto, vijana, wazee na wenye ulemavu.

    Kwa upande wake, Mkurugenzi  Mtendaji  wa Shirika la Research and Development organization (ReDO),Hudson Kazonta aliwataka waandishi wa habari kuandika habari mazingira ili kutoa elimu ya utunzaji mazingira kwa Wananchi na utambuzi wa mabadiliko ya tabia nchi.

    Maadhimisho hayo yalifanyika kimkoa baada ya kufanyika kimataifa Mei 3, 2024 Jijini Accra Ghana na kitaifa jijini Dodoma yalibebwa na kauli mbiu isemayo ” Uandishi wa Habari na Changamoto za Mabadiliko ya Tabia Nchi” na yamefanyika mara 31 tangu kuanziahwa kwake mwaka 1993.

  • Na Sylvester Richard- Singida

    Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga akihutubia wananchi wa Mkoa wa Singida waliofika katika ukumbi wa RC Mission Manispaa ya Singida kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo DCP Stella A. Mutabihirwa aliyehamishiwa Makao Makuu ya Polisi na kumkaribisha Kamanda SACP Amon Daudi Kakwale.

    Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga amewataka askari wa Mkoa wa Singida kukataa rushwa kila mahali wanapokutana na watu wasio waaaminifu wanaotaka kuwahadaa na  kuwapa rushwa ili wafanye udanganyifu wa kesi mbalimbali.

    Mganga amesema hayo Mei 3, 2024 katika hotuba yake aliyoitoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida aliyealikwa kuwa Mgeni Rasmi kwenye hafla ya kumuaga aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida DCP Stella Alchard Mutabihirwa iliyofanyika kwenye ukumbi wa RC Mission Manispaa ya Singida.

    Aidha, Dkt. Mganga amewasisitiza askari kutosheka na mishahara yao na kuepuka kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa ambavyo vinarudisha nyuma maendeleo ya nchi na ya mtu mmoja mmoja.

    Kwa upande mwingine, amewaomba viongozi wa dini kuendelea kuiombea Nchi ili iendelee kuwa na amani na wananchi wake waishi katika maadili.

    Akiwaaga askari wa Mkoa wa Singida, DCP Mutabihirwa amewashukuru askari na wananchi wa Mkoa wa Singida kwa ushirikiano waliompa katika kipindi alichokuwa Mkoani humo akiwa na cheo kidogo hadi alipoondoka na cheo cha Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) huku akiuacha Mkoa ukiwa shwari.

    DCP Stella A. Mutabihirwa akiwaaga askari na wananchi wa Mkoa wa Singida kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa RC Mission baada ya kuhamishiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma.

    Naye Kamanda wa Polisi wa sasa wa Mkoa wa Singida SACP Amon Daudi Kakwale ambaye pia amepokelewa rasmi katika hafla hiyo ameahidi kuendeleza mazuri aliyoyafanya DCP Mutabihirwa wakati akiwa Kamanda wa Mkoa huo.

    Hata hivyo, Kakwale amewaomba askari na wananchi wa Mkoa wa Singida kumpa ushirikiano katika kubaini, kupambana na uhalifu ili Mkoa wa Singida uendelee kuwa shwari.

  • Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP Amon Daudi Kakwale akiongea na makundi ya watu katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida.

    Na Sylvester Richard- Singida

    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida SACP Amon Daud Kakwale amewataka viongozi wa Serikali za Mitaa kuwatumia Polisi Kata katika kuimarisha ulinzi na usalama wa maeneo yao kwa kutoa taarifa za wahalifu kwa usahihi na kwa wakati.

    Alisema hayo Mei 3, 2024 wakati akizungumza na makundi mbalimbali ya watu wa Manispaa ya Singida wakiwemo viongozi wa Serikali za Mitaa, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini, wazee wa kimila na wamiliki wa makampuni ya ulinzi binafsi kwenye kikao  kilichofanyika ukumbi wa mikutano uliopo katika jengo la Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida.

    Aidha aliwataka viongozi hao kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa sahihi za viashiria vya changamoto za kiusalama ili zifanyiwe kazi.

    Kikao hicho ambacho pia Kamanda Kakwale amekitumia kujitambulisha, kilikuwa huru na wazi ambapo wajumbe walipata nafasi ya kutoa kero na kuchangia hoja mbalimbali zilizolenga kuimarisha ulinzi na usalama wa Mkoa wa Singida.

    Kwa upande wake, Mstahiki  Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu ambaye pia alihudhuria kikao hicho,  alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kupeleka huduma ya Polisi kwenye Kata na kusema kuwa Polisi kata wamekuwa msaada mkubwa kwa jamii kwakuwa uhalifu umekuwa ukipungua siku hadi siku.

    Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu akichangia hoja katika kikao cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida na makundi mbalimbali ya wakazi  wa Manispaa ya Singida.

    Aaliliomba Jeshi la Polisi lishirikiane na Mshauri wa Mgambo Wilaya katika kuwafundisha vijana wenye sifa juu ya ulinzi shirikishi ili vijana wafanye kazi ya ulinzi kwa uelewa zaidi.

    Katibu wa CHADEMA Jimbo la Singida Mjini, Mtta Anselemi  Adrian akichangia hoja kuhusu ulinzi na usalama.

  • Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Halima Dendego akiongea na watumishi wa umma Mkoa wa Singida katika kituo cha mabasi Ikungi kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani.

    Na Sylvester Richard-Singida

    Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amewataka watumishi wa umma Mkoa wa Singida kuisikiliza na kuielewa hotuba Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani iliyowasilishwa kwa niaba yake na Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kwenye maadhimisho ya Mei Mosi 2024 yaliyofanyika kitaifa Mkoani Arusha.

    Dendego amebainisha hayo jana Mei 1, 2024 wakati akizungumza na watumishi wa umma kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani  yaliyofanyika  kimkoa kwenye kituo cha mabasi Wilayani Ikungi.

    Baadhi ya mambo yaliyoahidiwa na serikali kwa wafanyakazi kupitia hotuba hiyo ni pamoja na kuhuisha viwango vya mishahara kwa kuzingatia uwezo wa kiuchumi na kibajeti pamoja na ujuzi na utendaji wa waajiriwa misingi ambayo imetajwa kuwa ni muhimu ili kuepuka mfumuko wa bei na uhimilivu wa deni la taifa na athari nyiningine za kichumi.

    Aidha, Dendego amewakumbusha watumishi kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni  na maadili ya kazi ili kuongeza ufanisi katika kazi. Maadhimisho hayo yalibebwa na kaulimbiu isemayo “Nyongeza ya mshahara ni msingi wa mafao bora na kinga dhidi ya hali ngumu ya maisha” na yaliambatana na utoaji wa zawadi ambapo Dendegu alikabidhi zawadi mbalimba kwa wafanyakazi wa Mkoa wa Singida waliofanya vizuri mwaka 2024.

  • Na Vincent Mpepo, OUT

    Imeelezwa kuwa ujio wa teknolojia mpya unapaswa kuchukuliwa kwa mapokeo chanya ili isadie katika mifumo ya ujifunzaji na usomaji katika ngazi zote za elimu badala ya kuweka vizuizi vingi katika utekelezaji wake.

    Hayo yamebainishwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Profesa Elifas Bisanda wakati wa kusaini makubaliano kati ya Chuo Kikuu Huriacha Tanzania na Chuo Kikuu cha Masafa cha Sayansi Tumizi  cha Uswisi yaliyofanyika hivi karibuni katika ukumbi wa chuo hicho Kinondoni jijini Dar es salaam.

     Akizungumzia masharti na vizuizi vya wanafunzi kutumia teknolojia mpya ikiwemo ya AI na ChatGPT katika ujifunzaji alisema wakati umefika kwa walimu na wahadhiri kuuliza maswali ambayo yatasaidia kuwashughulisha wanafunzi badala ya yale yaliyozoeleka.

    “Muulize maswali yatakayomfanya atafute majibu nje ya AI na ChatGPT, siyo yale ya kujadili au kutoa fasili ya dhana fulani”, alisema Profesa Bisanda.

    Profesa Bisanda alisema kwa sasa ufundishaji na ujifunzaji katika elimu ngazi zote unapaswa kuhusisha teknolojia ili kuwafikia wahitaji wengi na kwa muda mfupi lakini pia kurahisisha mchakato wa elimu tofauti ilivyokuwa hapo awali.

    “Watu wanaanza kuwa na woga na AI na ChatGPT  sawa na kwa waliosoma zamani kidogo ambapo ilikuwa ni kosa la jinai kutumia kikokotoo au kompyuta lakini kwa sasa vimekuwa vitu vya kawaida”, alisema Profesa Bisanda.

    Alisema mazingira ya kazi yanapaswa kuendana na mazingira ya kusoma yanayotawaliwa na simu janja na kompyuta badala yake tuwafundishe wanafunzi ili wapate maarifa, ujuzi na stadi za kazi au taaluma wanazosomea.

    Afisa Mwandamizi, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt.Evaristo Mtitu alipongeza jitihanda za chuo hicho katika uwekezaji kwenye Tehama na teknolojia nyingine wezeshi katika masuala ya ujifunzaji na ufundishaji.

    “Vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu zinapoingia kwenye mkataba wa maelewano ya kushirikiana kwenye maeneo ya makubaliano inasaidia  kubadilishana uzoefu kwenye maeneo ya ushirikiano”, alisema Dkt.Mtitu.

    Alisema vyuo vyote vinatakiwa kuwekeza kwenye matumizi ya teknolojia ili kurahisha mchakato wa kujifunza na kufundishia.

    Aliongeza kuwa wizara inaamini kuwa teknolojia zinasaidia kuwa na rasimali watu inayoweza kutumika kuwafikia walengwa wengi kwa muda mfupi mfano walimu wa sayansi.

    “Teknolojia ikitumika vizuri inatoa nafasi kwa mwanafunzi kushiriki vizuri kwenye kipengele cha ujifunzaji mwenyewe”, alisema Dtk.Mtitu. 

  • Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego akiongea na wananchi wa Mkoa wa Singida katika maadhimisho ya miaka 60 ya kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mji Mdogo wa Kiomboi, Wilaya ya Iramba, Mkoani Singida.

    Na Sylvester Richard, Singida

    Watanzania wamekumbushwa kuuenzi muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya kazi kwa maarifa na juhudi ili kujiletea maendeleo.

    Wito huo umetolewa na  Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego wakati wa maadhimisho ya miaka 60 ya muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika yaliyofanyika leo maeneo ya kituo cha mabasi kilichopo katika Mji Mdogo wa Kiomboi, Wilaya ya Iramba Mkoani Singida huku wito wake ukiwa ni kufanya kazi zaidi.

    Dendego aliwapongeza wasanii waliosherehesha katika maadhimisho hayo zikiwemo kwaya, ngoma za asili, mziki wa kizazi kipya na wachoraji na kuwataka kudumisha utamadini, mila na desturi za mtanzania.

    “Sanaa ni furaha, ni afya, ni kazi na ni ajira”, alisema Dendego.

    Aidha, katika maadhimisho hayo Dendego alipokea zawadi zilizoandaliwa na baadhi ya wasanii huku pia yeye akikabidhi zawadi kwa makundi mbalimbali kama zilivyoandaliwa na kamati ya maadhimisho hayo.

    Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga ambaye alihudhuria maadhimisho hayo aliwaasa wananchi wa mkoa huo kuendeleza mshikamono walionao katika nyanja zote ili kujijenga na kukua kiuchumi kama muungano unavyotaka kwa maendeleo yao na mkoa kwa ujumla.

    Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga akiongea na
    wananchi katika maadhimisho ya miaka 60 ya kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika katika Mji Mdogo wa Kiomboi, Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

    Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa na kwa ngazi za mikoa na wilaya kwa namna mbalimbali huku yakiongozwa na kauli mbiu isemayo,”Tumeshikamana  na tumeimarika, kwa maendeleo ya taifa letu”.

  • By Vincent Mpepo, OUT

    The Vice Chancellor of the Open University of Tanzania, Professor Elifas Bisanda exchanging partnership agreements with Professor Egon Werlen of Swiss Distance University of Applied Sciences during the MoU signing held today in Kinondoni, Dar es Salaam (Photo by Vincent Mpepo).

    The Open University of Tanzania and Swiss Distance University of Applied Sciences have signed a five year Memorandum of Understanding which will help the two to collaborate in various academic activities for the betterment of two universities and countries at large.

    Speaking during the official signing of the MoU between the two universities, the Vice Chancellor of the Open University of Tanzania, Professor Elifas Bisanda said the collaboration will involve a number of areas of agreement which involves students and lectures exchange, fellowships, scholarship and collaborative research.

    He welcomed and thanked the Swiss Distance University of Applied Sciences for having an interest to collaborate with the Open University of Tanzania and assured that his university will keep on cherishing the good things for the benefit of two universities.

    Dean Faculty of Arts and Social Sciences, Dr.Dunlop Ochieng said the collaboration has been a very fruitful because it has brought a number of benefits for both universities.

    “FASS is very grateful and proud for this collaboration that started with the faculty and has now extended to university wide”, said Dr.Ochieng.

    He said his faculty is committed to encouraging faculty members to actively participate in future research stemming from the present study under the auspices of the OUT UNESCO Chair on curriculum development.

    A researcher from the Open University of Tanzania, Dr.Christopher Awinia shared the findings of a research which was part and parcel of the collaboration between two universities where it has been found that technological challenges hamper learning and teaching environment in Tanzania.

    He identified some of the challenges as stemming from internet cost and unreliable internet something which makes learning and teaching in Tanzania and most of African countries to face some difficulties hence legging behind in education.

    Senior Education Officer from the Ministry of Education, Science, and Technology, Dr. Evaristo Mtitu addressing the public during the signing ceremony between the Open University of Tanzania and Swiss Distance University of Applied Sciences held today in Kinondoni, Dar es Salaam (Photo by Vincent Mpepo).

  • Na Mwandishi wetu, Dar es salaam

    Kanisa la DPA la jijini Dar es salaam litafanya maadhimisho ya miaka minne tangu kuanzishwa kwake kama sehemu tathimini na shukrani kwa Mungu.

    Hayo yamebainishwa na Mchungaji muasisi wa kanisa hilo, Hanington Kabuta wakati wa mahojiano na mwandishi wetu huku akitanabaisha kuwa madhabahu hiyo ya DPA imekuwa baraka kwa mtu mojamoja na jamii kwa ujumla na kwamba Mungu amewatendea mengi.

    “Mwezi huu wa nne mwaka 2024 kanisa letu la DPA limefikisha miaka 4 tangu lianzishwe hapa Goba, Tegeta A, Mtaa wa Msabila”, alisema Mchungaji Kabuta.

    Alisema uongozi wa kanisa hilo umeamua kufanya maadhimisho ndani ya wiki hii, ambapo kilele chake ni Jumapili jioni.

    Tuna maombi ya mfungo wiki hii pamoja na Semina ya Historia ya Kanisa Kiulimwengu, Afrika, Tanzania, na Hatimaye DPA, alibanisha Mchungaji Kabuta.

    Aliongeza kuwa semina ni Jumatano tarehe 24 hadi Junapili tarehe 28/04/2024 na  Muda ni kuanzia saa 10:00 Jioni hadi 12:30 Jioni kwa siku hizo tano huku agenda kuu ni ‘Fundisho la Kanisa, Maombi na Maombezi.

    Aliwataka watu wote wenye mapenzi mema kuhudhuria na kuwaalika wengine huku akiwakumbusha kushirikisha taarifa hii kwenye mitandao ya kijamii ili wengi waokolewe.

  • RC Dendegu Kuimarisha Ushirikiano na TCCIA

    Na Sylvester Richard, Singida

    Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendegu akiongea na wajumbe kutoka Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Singida kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwake leo.

    Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendegu ameuhakikishia uongozi wa Jumuiya ya wafanyabiashara (TCCIA) Mkoa wa Singida kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi ikiwemo wafanyabiashara   ili kuinua uchumi wa Mkoa wa Singida kwakuwa Serikali ya Mkoa ipo imara katika suala zima la ulinzi na usalama.

    Dendegu alitoa kauli hiyo Aprili 24, 2024 ofisini kwake wakati wa mazungumzo na kati yake na uongozi wa chama cha wafanyabiashara, wakulima na wamiliki wa viwanda Tanzania (TCCIA) waliopo Mkoani Singida.

    Alisema Jumuiya hiyo ni muhimu na muhimili katika kuinua uchumi wa Singida hivyo kuwaomba kuendeleza ushirikiano huo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa mkoa huo.

     ambao Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani amedhamiria kuboresha maisha ya mtu mmoja mmoja na ndiyo maana miradi mbalimbali inatekelezwa.

    Akiongea kwa niaba ya TCCIA, Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Elly Kitila Mkumbo alisema walifika  ofisini hapo kwa lengo la kukitambulisha chama hicho cha wafanyabiashara kwa Mkuu wa Mkoa aliyehamia hivi karibuni akitokea Mkoa wa Iringa ambapo wajumbe walipata nafasi ya kujadili masuala  mbalimbali kuhusu kukuza uchumi kupitia  sekta binafsi ikiwemo biashara.

    Alisema chama hicho kitaendeleza na kudumisha ushirikiano kati yake na serikali kwa madhumuni ya kumkomboa na kumhakikishia mfanyabiashara mazingira wezeshi katika shughuli zake kwa maslahi ya taifa pamoja na kulitangazo soko la kimataifa la vitunguu lililopo Mkoani Singida.

    Mwenyekiti wa Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Singida Bw. Elly Kitila Mkumbo, akizungumza kwenye kikao baina ya Mkuu wa Mkoa wa Singida na TCCIA kilichofanyika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huo.

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT amewakumbusha wanawake kuvaa mavazi ya heshima kanisani ili kuendelea kuwa walezi wazuri kwa watoto na jamii.

    Mchungaji Dkt.Mwatumai Mwanjota aliyasema hayo wakati akihubiri katika ibada ya Jumapili Mtaani hapo na kuwataka wajijengee heshima kwa mwenendo mwema ikiwemo mavazi.

    “Wakati mwingine akina mama tunajishushia heshima yetu wenyewe kwa aina ya mavazi tuyavaayo”, alisema Mchungaji Dkt.Mwanjota

    Aidha, alisema tabia hiyo ni sehemu ya mwenendo mbaya katika jamii na kwamba kwa kufanya hivyo wanakiuka majukumu waliyopewa kwa jamii japo pia alibainisha kuwa wapo wanaume ambao pia huvaa vibaya.

    “Utakuta mwanaume mzima anavaa suruari chini ya kiuno”, alisema Mchungaji Dtk. Mwanjota.

    Aidha aliwakumbusha wanawake kutambua nafasi ya mwanume katika familia kwa kuwa wapo baadhi ambao wakijaaliwa kuwa na nafasi nzuri kiuchumi au madaraka huwadharau waume zao.

    Hata kama una madaraka na nafasi nzuri zaidi ya mume wako tambua nafasi yake kuwa ni kichwa, alisema Mchungaji Dkt.Mwanjota.

    Kwa upande wake, Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava aliwakumbusha washarika wa mtaa huo kupitia jumuiya zao kufanya usafi katika maeneo yao kanisani hapo ili kuweka mazingira ya kanisa hilo katika hali ya usafi.

    Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi Mtaani hapo, Exaud Mchome amewakumbusha washarika kutimiza ahadi zao ili kazi ya ujenzi iendelee bila kukwama.

    Aliwaomba washarika kuendelea kumtolea Mungu ili kufanikisha kazi ya ujenzi na kwamba kiuhalisia hakuna ambaye anaweza kutamka hana cha kumpa Mungu kwa kuwa wema wake umeendelea kuwa katika maisha yao.

    “Hata pumzi na uhai tulivyonavyo vinadhirisha upendo wa Mungu kwetu na tunapaswa kumshukuru”, alisema Mzee Mchome.

    Katika ibada hiyo huduma kadhaa zilitolewa ikiwemo sakramenti ya ubatizo na meza ya bwana huku pia familia mbili zikimshukuru Mungu kwa makuu aliyowatendea katika nyakati mbalimbali.

    Matukio mbalimbali katika picha ikiwemo ubatizo, jengo la Kanisa linaloendelea kujengwa na familia ya Wasiwasi Mwabulambo mara baada ya ubatizo wa mtoto wao. (Picha na Vincent Mpepo)

    Kwaya ya vijana ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe ikihudumu wakati wa ibada Siku ya Jumapili. (Picha na Vincent Mpepo)