Jamii imetakiwa kuasili watoto wanaoishi na kutunzwa kwenye vituo mbalimbali ili wawe sehemu ya familia hivyo kupata malezi na uangalizi unaostahili kama wanajamii wengine.
Wito huo umtolewa na Afisa Ustawi wa Jamii, Malezi na Familia wa Jiji la Arusha, Nivoneia Kikaho wakati wa uzinduzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake mkoa wa Arusha ‘ARUSHA WOMEN IN MEDIA’ uliofanyika mwishoni mwa wiki na kuhudhuliwa na wanawake waandishi wa mkoa huo, wanafunzi wanawake wa tasnia hiyo na wadao mbalimbali wa maendeleo.
Alisema baadhi ya vigezo vinavyotumika ili anayekusudia kuasili mtoto kupata kibali cha mtoto wa kulea ni pamoja na utayari, maadili, usafi na mapenzi kwa watoto na kuwa utaratibu huo ni wakisheria na una taratibu za kufuata.
“Wanadoa wanakaribishwa kuasili watoto kwa kuwa kuna mazingira rafiki tofauti na wasio kwenye ndoa”, alisema Kikaho.
Alisema uwezo na vigezo vivyokusudiwa ni vya msingi na vya kawaida ambavyo vitamuwezesha mtoto anayeasiliwa kupata mahitaji yake muhimu.
Hatahivyo, alisema bado kuna mwamko mdogo wa jamii kuasili watoto jambo ambalo linahitaji uhamasishaji.
Mwenyekiti Arusha Women in Media Jamillah Omar kuasili mtoto ni kama sadaka hivyo anayeasili hapaswi kuchagua mtoto kati wengi kwenye mahali wanapoishi ili kuzuia unyanyapaa na kuwafanya wanakosa kuasiliwa kujisikia vibaya.
Hatahivyo, kwa uzoefu wa miaka ya hivi karibuni suala la kuasili watoto halijapata kipaumbele na jamii bado kunahitajika juhudi za makusudi kuhamasisha jamii ili ione umuhimu wa jambo hilo.
Viongozi wa serikali za mitaa ikiwemo watendaji na wenyeviti wa vijiji, kata na mitaa wametakiwa kutoa ushirikiano kwa shirika la UCRT linalotekeleza mradi wa mpango wa matumizi bora ya ardhi vijinini.
Hayo yalisemwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbulu, Paulo Bura kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Veronica Kessy wakati akifungua kikao cha uzinduzi wa awamu ya pili ya mradi wa mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa vijiji sita chini ya Ujamaa Community Resource Team (UCRT), uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu Machi 19, 2024.
Alisema viongozi hao wanatakiwa kutoa ushirikiano watekelezaji wa mradi huo ili kile walichokuja nacho kiweze kuwanufaisha wananchi wa wilaya hiyo na kutimiza malengo hayo yenye nia njema.
“Lakini sisi tulioingia kwenye awamu hii vijiji hivi sita, pia tujue sisi ni wa mfano na tunatakiwa tufanye vizuri ili kuwapa moyo wafadhili kuendelea na mradi huu kwa vijiji vingine”, alisema Bura.
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Mbulu, Petro Tarimo aliwaomba wanufaika wa mradi wa zamani na wapya waendelee kutoa ushirikiano kwa UCRT na kutoa elimu kwa wanchi wengine ili kuepuka migogoro ya mipaka.
Mratibu wa Ujamaa Community Resource Team (UCRT), Dismas Meitaya ameushukuru uongozi wa Wilaya Mbulu kwa ujumla kwa ushirikiano wanaoutoa kwa takribani miaka 20 hivyo kuwawezesha kutekeleza mradi huo kwa ufaninsi.
Malengo ya UCRT ni kuwezesha jamii ya asili kumiliki, kusimamia na kunufaika na ardhi, alisema Meitaya
Alisema wamelenga aidi kwenye jamii ya wakusanya matunda, ambao ni wa hadzabe na waakie, wamaasai, wadatoga pamoja na wafugaji , wakulima wabatemi na wa iraqw.
“Huu mpango ni shirikishi sana, akina mama wanapewa kipaumbele ili washiriki kikamilifu na zaidi kuona jamii na akina mama kupitia vikundi vyao wakiwa mstari wa mbele.
Alibainisha vijiji lengwa sita vya mradi katika bonde la Yaeda na Ziwa Eyasi ni Garbabi, Yaedakati, Dirim, Endalat, Murkuchida na Endamilay.
Sehemu ya washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Mkoani Arusha ‘Arusha Women in Media’ katika picha za pamoja katika ukumbi na viwanja vya Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyofanyika hivi karibuni.
Waandishi wa habari wanawake mkoa wa Arusha wametakiwa kuchangamkia fursa kwa kujiunga na chama cha waandishi wananawake mkoani humo ili kuwa na umoja wenye nguvu na sauti moja katika kujikomboa kiuchumi.
Mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Off we Go safaris Ltd Genevive Mollel ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake mkoa wa Arusha kijulikanacho kwa jina la ‘ARUSHA WOMEN IN MEDIA’ ulifanyika jijini Arusha na kuhudhuliwa na wanawake waandishi wa mkoa huo, wanafunzi wanawake wa tasnia hiyo na wadao mbalimbali.
Alisema uandishi wa habari ni tasnia mtambuka ambayo yenye fursa nyingi zikiwemo za kiuchumi na kijamii hivyo waandishi wa habari waache kujifungia sehemu moja ili kuona fursa katika maeneo mengine ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuacha utegemezi.
Mwenyekiti Arusha Women in Media Jamillah Omar amesema lengo umoja huo ni kutumia fursa mbalimbali zitolewazo na serikali, wakala wa serikali, makampuni na taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa ajili ya wanawake ikiwemo mikopo yenye masharti nafuu na isiyo na riba.
Alisema waandishi wa habari wanawake kama walivyo wanawake wengine wanakabiliwa na changamoto ya kipato kutokana na majukukumu ya familia hivyo umoja huo utawasaidia kuzifikia fursa hizo kwa pamoja na hatimae kujikwamua kimaisha.
“Waandishi wenzangu hasa wanawake mnatambua namna ambavyo mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amejipambanua kuwawezesha wanawake kiuchumi hivyo na sisi tujiongeze tutumie fursa hizo tuwe na vyanzo mbadala vya kujiongezea kipato”alisema Jamillah.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha Cloud Gwandu aliwataka waandishi wa habari wanawake kujiunga na umoja huo ili wawe na sauti moja itakayosaidia kufikia malengo yao.
Alisema waandishi wa habari wengi sasa hivi wanapitia changamoto ya ajira ambapo asilimia kubwa hawana ajira wala mikataba ya kazi jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa maisha yao.
“Tasnia ya habari kwa sasa inapitia wakati mgumu kwa kuwa kazi nyingi za serikali zimekuwa zikifanywa na maafisa habari wa serikali badala ya kutumia waandishi wa habari”, alisema Gwandu.
Wakati huo huo Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Vincent Mpepo aliwakumbusha waandishi kuzingtia maadili na weledi katika kazi zao na kwa kuzingatia mabadiliko ya teknolojia amabyo yana changamoto kadha wa kadha.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Arusha, Amulikiwa Massawe alisema uzinduzi wa umoja huo umekuja wakati mwafaka ambapo benki ya CRDB imetenga fedha nyingi kwa ajili ya kuwakopesha wanawake kwa masharti nafuu .
“Habari njema kwa sasa ni kwamba CRDB ina akaunti maalum kwa ajili ya wanawake ikiwemo akaunti za Malkia na Imbeju ambazo zina masharti nafuu”, alisema Massawe.
Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanyika barani Afrika na nchini Tanzania zinabainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili tasnia ya habari ikiwemo kuyumba kiuchumi kwa vyombo vingi vya habari hivyo kushindwa kuwapa waandishi wa habari stahiki zao kwa muda muafaka ikiwemo mishahara na mikataba ya ajira za uhakika hivyo kuwafanya waendelee kuwa tegemezi jambo linaothiri pia misingi ya uandishi wa habari ambapo kuna wakati waandhi wa habari wanakuwa wasemaji wa watu badala ya umma.
Waandishi wa Habari wanawake wameshauriwa kuungana na kutumia fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali ili waweze kujikwamua kiuchumi jambo ambalo litawasaidia kuwa na kipato mbadala na kuondokana na utegemezi wa kazi moja.
Mwenyekiti wa umoja wa waandishi wa Habari mkoa wa Arusha Jamillah Omar ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa chama hicho cha ARUSHA WOMEN IN MEDIA ulioenda sambamba na semina elekezi iliyohusisha masuala ya ujasiriamali na fursa za mikopo zitolewazo na benki ya CRDB,Usalama wa mitandaoni kwa wanawake mada iliyotolewa na TCRA,maadili ya uandishi wa Habari na malezi bora ya Watoto.
Jamilah amesema serikali chini ya mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imetoa Fursa nyingi za kuwawezesha wanawake ikiwemo mikopo isiyokuwa na riba hivyo imefika wakati sasa kwa waandishi wa Habari wanawake nao kutumia fursa hiyo kujiingiza katika ujasiriamali ili waweze kuwa na chanzo kingine cha mapato.
Amesema kutokana na kupanda kwa gharama za Maisha na mara nyingi wanawake ndio wamekuwa kukabiliwa na majukumu mengi ya malezi ya familia wamekuwa wakikumbana na changamoto ya kipato hivyo wakati mwingine kusababisha kuzidiwa na majukumu ambapo kwa kutumia fursa ya umoja huo itawasaidia kuungana na kunufaika na fursa mbalimbali.
“Siku zote sisi kama waandishi wa Habari tumekuwa vianara wa kuripoti matukio mbaimbali ikiwemo hizi fursa za mikopo kama ya Halmashauri inayotolewa kwa ajili ya wanawake vijana na watu wenye ulemavu lakini sisi kama waandishi wa Habari wanawake tumetumia vipi fursa hiyo?alihoji Jamillah
“Imefika wakati sasa waandishi wa Habari wanawake tubadilike kwanza tumechelewa sana kila mtu anatushangaa tulikuwa wapi hadi leo hatuna umoja wa kama huu”alisema
Mgeni Rasmi katika hafla hiyo mfanyabiashara mjasiriamali wa sekta ya utalii Genevive Mollel amewapongeza waandishi wa Habari wanawake mkoa wa Arusha kwa kuanzisha umoja huo ambapo amewatoa hofu kuwa ujasiriamali si kitu kigumu na kusisitiza kuwa wanaweza kutokana na tasnia na uwanda mpana katika kila sekta.
“katika sekta yenu ya Media inafursa nyingi sana mnakutana na watu wengi sana kila siku kila mahali kwa mfano kwenye sekta ya utalii hatuwezi kupanda bila media kuna vivutio vingi ambavyo vinatanganzwa kwa kupitia media hii ni fursa”alisema Genevive
Awali mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa Habari mkoa wa Arusha Cloud Gwandu akizungumza katika hafla hiyo amewapongeza waandishi wa Habari wanawake kwa kuungana na kusema kuwa dunia ya sasa bila kuungana huwezi kufanya kitu chochote kikubwa hata kama unakili au uwezo kama nani.
“Ninawaomba waandishi wa Habari ambao hawajajiunga kujiunga na chama hicho ili kiwe na nguvu ili wawe na sauti moja itakayosikika itakayowasaidia kuwafikisha mbali”alisema Gwandu
Amesema hivi sasa tasnia ya uandishi wa Habari inakabiliwa na changamoto kubwa ya kazi zao nyingi kufanywa na maafisa Habari wa serikali jambo ambalo limepunguza wigo wa waandishi kupata kazi za kufanya hivyo kwa umoja huo itawasaidia kubadilishana Mawazo na kutumia vyema fursa mbadala kujikwamua kiuchumi.
Gwandu amesema waandishi wengi wa Habari hawana ajira hivyo uhakika wa kipato chao ni mdogo hali inayowazalimu wakati mwingine kuwa omba omba kwa wadau hali ambayo amesema imekuwa ikiwadhalilisha.
The Eastern Africa Regional Early Childhood Conference will start on 11th to 14th Mach, 2024 at Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam and will involve participants from Tanzania and outside Tanzania.
According to the information from the organizers’ website, this years’ conference theme is ‘Investing in Early Childhood: Building Human Capital along the Life Course’ and it will be open to multisectoral stakeholders interested in improving early childhood outcomes.
“Policy Makers, CSOs/FBOs/CBOs, Grassroots Advocacy Organizations including Women and Youth Groups, Academia and Development Partner Organizations”, says part of the information from the website.
The conference will provide an opportunity for stakeholders and participants to take stock of the status of early childhood in the sub region, showcase innovative programs in the sub-region, foster dialogue that promotes knowledge exchange and learning and build consensus around key advocacy issues.
The conference presentations will be an in-person with different sessions to ensure wide and active participation and provide avenues for generating insights that will be taken up in the conference recommendations, final communication and plans for action.
The conference will employ plenary sessions where keynote presentations will be made along with panel sessions that spotlight country experiences, oral paper presentations in thematic break-out parallel sessions, round table discussions for smaller groups that allow for in-depth engagement and learning sessions.
Moreover, other presentation modalities are not limited to side events to support capacity building and joint planning for various interest groups.
These presentation modalities will enable groups to engage, network and build pathways for collaboration and partnerships that would take Early Childhood forward in the region and lastly exhibition of partner initiatives and sharing of materials and resources.
According to Dr. Evangeline Nderu, the conference is expected to receive participants from Kenya, Uganda, Rwanda, South Sudan, Mozambique; South Africa and from outside Africa.
Group photos of rapporteurs which include students and a lecturer from the Aga Khan University during the orientation before the start of the conference. (Picture by Vincent Mpepo).
IMEELEZWA kuwa baadhi ya sheria, taratibu na kanuni za manunuzi nchini ni kikwazo kinachokwamisha utelekezaji wa miradi kwa muda uliopangwa na kusababisha wananchi kutopata huduma kwa muda uliopangwa.
Hayo yamebainishwa na Mratibu Mkuu wa Mradi wa Mageuzi ya kiuchumi, Profesa Deus Ngaruko katika siku ya pili ya kikao kazi cha siku tatu kinachoendelea Mkoani Pwani Wilaya ya Bagamoyo na kuhusisha waratibu wa mradi katika idara zote na wakurugenzi wa vituo vya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambao mradi huo unatekelezwa katika vituo vya mikoa wanavyovisimamia.
Alisema taratibu, kanuni na sheria za manunuzi zinaleta ugumu katika kutekeleza masuala mbalimbali ikiwemo miradi wa mageuzi ya kiuchumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.
“Fedha zipo lakini tunashindwa kuzitumia kutekeleza mradi kwa wakati kwa sababu kuna taratibu ambazo zinatumia muda mrefu kukamilika, kuna haja kuangaliwa kwa taratibu hizi,”alisema Profesa Ngaruko.
Mratibu wa uhuishaji mitaala, Dkt. Halima Kilungu alisema utekelezaji wa miradi kama huu wa mageuzi ya kiuchumi unahitaji wafanyakazi wa taasisi husika kutoka idara na vitengo vyote kushirikiana ili kuhakikisha kuwa changamoto za ndani zinatatuliwa ili kwa pamoja kuhakiksha mradi unatekelezeka kwa faida ya taasisi na taifa kwa ujumla.
“Ni muhimu kwa wafanyakazi wa idara zote ndani ya taasisi kushirikiana ili kuhakikisha kuwa mradi unafanikiwa kwani ukifeli ni taasisi na taifa limefeli”, alisema Dkt.Kilungu.
Kwa upande wake, Mratibu wa Manunuzi wa Mageuzi ya kiuchumi chuoni hapo, Daudi Sospeter alisema ni muhimu kufuata taratibu, sheria na kanuni za manunuzi ili kuondokana na changamoto za kiuhasibu na mahesabu.
“Sheria za manunuzi zinaweza kuwa na tasfiri tofauti na ilivyokusudiwa”, alisema Sospeter.
Alisema lengo la kusimamia sheria, kanuni na taratibu za manunuzi ili yaende kwenye mamlaka husika
Mradi wa mageuzi ya kiuchumi wa miaka mitano kupitia ufadhili wa Benki ya Dunia una lengo la kukuza elimu ya juu kama chachu ya uchumi mpya wa Tanzania ikihusisha kupanua uwezo wa vyuo vikuu katika maeneo muhimu ya uvumbuzi, kuongeza soko la ajira na kwa kuwekeza katika miundombinu inayohitajika kwa ufundishaji na utafiti wa kisasa.
Mratibu Mkuu wa Mradi wa Mageuzi ya kiuchumi, Profesa Deus Ngaruko akifafanua jambo wakati wa kikao kazi kilichofanyika Bagamoyo hivi karibuni
Mratibu wa Manunuzi, Daudi Sospeter akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha tatu cha tathimini ya maendeleo ya mradi wa magezi ya kiuchumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kilichoanza leo Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. (Picha na Vincent Mpepo, OUT).
Wanataaluma wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania wametakiwa kufikiri namna bora ya matumizi ya rasilimali majengo yatakayopatikana kupitia mradi wa mageuzi ya kiuchumi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia ili kuwa na uhusiano wa moja kwa moja kati ya taaluma na maendeleo ya kiuchumi nchini..
Wito huo umetolewa leo na Mratibu Mkuu wa Mradi huo wa chuo hicho Profesa Deus Ngaruko katika siku ya kwanza ya kikao kazi cha siku tatu kinachoendelea Mkoani Pwani Wilaya ya Bagamoyo na kuwahusisha waratibu wa mradi katika idara zote na wakurugenzi wa vituo vya chuo hicho ambao mradi huo utafanyika katika vituo vya mikoa wavyoviongoza.
Alisema wanataaluma kwa ujumla wao wanapaswa kufikiria miradi endelevu yenye tija kwa kuongeza thamani na kuzalisha bidhaa na hudumua endelevu ambazo zitasaidia kuwa na progamu za kitaaluma zenye uhusiano wa moja kwa moja na ajira ili kuwa na wahitimu watakaoweza kujiajiri mara baada ya kuhitimu.
“Vyuo vikuu vinatakiwa kuwa chachu ya maendeleo kupitia programu mbalimbali ambazo zitasaidia kuandaa wahitimu wenye ujuzi wa vitendo”, alisema Profesa Ngaruko.
Mratibu wa Kituo cha Mkoa cha Chuo Kikuu HurIa cha Tanzania cha Mtwara, Mhadhiri Msafiri Njoroge alisema wamepokea mawazo hayo na kubainisha kuwa mazingira na muktadha wa kila mkoa unaweza kutoa fursa tofauti na mikoa mingine.
“Kwa asili ya muktadha wa maeneo ya vituo hivyo tunaweza kubuni miradi midogomidogo itakayotumia taaluma kupata pesa”, alsima Dkt.Njoroge.
Aidha alishauri kuwepo kwa mwendelezo wa majadiliano na ushirikishwaji na mahusiano mazuri kati ya wakurugenzi wa vituo vya chuo hicho na timu ya watekelezaji ili kupata matokeo mazuri zaidi kiutekelezaji.
Mratibu Msaidizi wa Mradi huo chuoni hapo, Mhandisi, Dkt. Timothy Lyanga alisema katika utoaji wa kandarasi za mradi huo masuala ya kisheria yamezingatiwa ikiwemo kuwa na makubaliano ambayo yanaweka bayana majukumu ya watekelezaji mradi huo katika kila hatua.
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni moja ya taasisi za elimu ya juu kinachotekeleza mradi wa miaka mitano wa magaeuzi ya kiuchumi kupitia ufadhili wa Benki ya Dunia wenye lengo la kukuza elimu ya juu, kukuza uchumi na kujenga uwezo wa vyuo vikuu ili kuchangia katika maeneo muhimu ya uvumbuzi, maendeleo ya kiuchumi ikiwemo uwekezaji katika uimarishaji wa miundombinu ya ufundishaji, utafiti na kuendeleza wahadhiri kitaaluma.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Pius Lutumo Leo 17 Februari 2024 ameshiriki kutoa elimu ya haki jinai katika Kanisa la Pentekoste Kibaha ikiwa ni sehemu ya elimu kwa jamii (ushirikishwaji jamii) katika kutatua uhalifu na wahalifu.
Kongamano hilo lililoandaliwa na Pwani Pastors Network na Pastors Fellowship Kibaha maili moja, kamanda Lutumo alisema kuwa jukumu la viongozi wa dini ni kuhakikisha jamii inaishi kwa kufuata sheria na maadili mema yanayofundishwa na wachungaji katika nyumba za ibada ambapo wao ndio viongozi.
Akifafanua juu ya mada hiyo kamanda alisema ni vema zaidi kushukuru kwa Mungu juu ya uumbaji wetu kuliko kuomba kila siku huku akisema chanzo cha uhalifu na wahalifu ni jamii kukosa maaadili yanayochochea vijana kuwa wezi, vibaka, majambazi au hata wauaji katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kujinufaisha na kujipatia kipato kwa njia zisizo halali.
Alisema viongozi wa dini wanapaswa kukemea jamii kutofanya vitendo vya kihakifu kupitia mahubiri huku wakisisitiza matendo mema.
Kamanda Lutumo alisema serikali kupitia Kamati ya Haki Jinai iliyoundwa mwaka 2023 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Daktari Samia Suluhu Hassan ikiongozwa na Jaji Mstaafu Chande Othman ilikusudia kusaidia jamii kupitia Jeshi la polisi kwa kuboresha utendaji wa kazi kwa kuongeza vitendea kazi, kuboresha hali ya maisha kwa kujenga nyumba za askari na kuwapandisha vyeo.
Sanjali na hayo kamati ilitoa maelekezo juu ya utolewaji wa dhamana kwa kila mtuhumiwa anapofikishwa kituo cha Polisi.
“Ubambikiaji kesi uishe maana unawakosesha haki wananchi”, alisema Kamanda Lutumo.
Kamati ilielekeza ilisema dhamana ni haki ya kila mtuhumiwa na itolewe pasipo masharti magumu na vikwazo, maana imekuwa tabia ya watu kupelekana Polisi kwa makosa ya kawaida yanayoweza kusuluhishwa na viongozi wa kijamii pasipo kufika Polisi.
Alisema utolewaji wa dhamana utapunguza mlundikano wa mahabusu walio na makosa yenye dhamana katika vituo vya Polisi
Wakristo wametakiwa kuacha wivu kwa kuwa una matokeo mabaya yanayoweza kuleta atahari hasi na uharibufu katika jamii hivyo kutenda dhambi.
Wito huo umetolewa na Padre Guntram Hongo wakati wa mahubiri siku ya Jumamosi katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Nambehe Parokia ya Msalaba Mkuu Jimbo Kuu la Songea wakati wa ibada ya kumwombea Marehemu Thobias Komba.
Alisema wivu mbaya hurudisha nyuma maendeleo ya jamii kwa mtu mmoja mmoja, hufarakanisha na ni dhambi.
“Wivu mbaya huleta matokeo mabaya na athahari zake daima ni hasi”, alisema Padre Hongo.
Alisema wivu ni dhambi ambayo inaweza kutendwa na mtu yeyote awe Askofu, Padre, Mtawa au muumini na hivyo kuwataka wakristo kuishi maisha yenye kumpendeza Mungu.
Kwa upande wake, Wilhem Komba alisema wivu una tabia ya kuwafanya watu kuchukia mafanikio ya wengine au kufurahia kushindwa kwa wengine kitu ambacho wakati mwingine ni kikwazo cha maendeleo siyo tu kwa mwenye mafanikio hata mwenye wivu.
“Wivu ni kuzuizi cha maendeleo na mafaniko ya mwenye wivu na wengine”, alisema Komba.
Alisema baadhi ya athari za wivu ni pamoja na mtu kushindwa kujifunza mambo mema kwa waliofanikiwa badala yake kuishia kufurahia anguko au kushindwa kwa wengine kitu ambacho hakina faida chanya.
Msemaji wa Familia Jordan Komba aliwashukuru ndugu, jamaa na marafiki walioshiriki katika ibada ya kumwombea Marehemu na kwamba wamekuwa faraja wakati wote tangu wakati wa homa mpaka alipopatwa na umauti.
Matukio katika picha: Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wlioshiriki katika ibada ya kumuombea Marehemu Thobias Komba siku ya Jumamosi katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Nambehe, Parokia ya Msalaba Mkuu, Jimbo Kuu la Songea(Picha na Vincent Mpepo).