• Na Vincent Mpepo, OUT

    Watanzania wametakiwa kujenga utaratibu wa kupima afya mara kwa mara ili kuwa na uhakika wa maendeleo kiafya badala ya kusubiri  vipimo wakati wa homa.

    Wito huo ulitolewa na Daktari Julius Mchelele kutoka Kliniki ya Path Labs wakati wa tukio la ufunguzi wa mbio za Marathoni lilioandaliwa na Umoja wa Vijana wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wakazi wengi wao vijana.

    “Watu walijitokeza kwa wingi na wamepima afya zao”, alisema Dkt.Mchele

    Aliushukuru uongozi Uongozi wa vijana wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa kuwaalika katika tukio hilo na kuwataka kuendelea na ushirikiano huo kwa matukio mengine kwa wakati ujao.

    Alisema chagamoto kubwa kwa baadhi ya washiriki wa mbio hizo baada ya vipimo ni shinikizo la damu la juu na la chini ambalo linatokana na mtindo wa maisha na masuala ya ulaji.

    Kwa upande wake, Mtaalamu wa Damu, Kitengo cha Damu-Muhimbili, Richard Massam alisema mwitikio siyo mbaya kwa kuwa wapo minongoni mwa washiriki waliojitokeza kutoa damu huku akiwakumbusha watanzania kuendelea kuchangia damu kutokana na mahitaji makubwa.

     “Ili kuokoa wagonjwa wenye uhitaji wa damu ni lazima binadamu mwingine akubali kuchangia damu”, alisema Massam.

    Alisema kitengo chake huwa kina matukio ya kukutanisha watu ya mara kwa mara ili wanaokubali wachangie damu kutokana na ukweli kuwa hakuna kiwanda cha kuzalisha damu.

    “Ninaomba ambao wapotayari waungane nasi kwa siku zote mitaani, shuleni na nyumba za ibada ili tuendelee kuokoa uhai wa wahitaji wa damu”, alisema Massam

    Mwenyekiti wa Taasisi ya Eduthon Elite Suuport, Anwari Said alisema dhima ya taasisi yake ni kuhakikisha inatengeza na kushirikisha vijana fursa mbalimbali za kuchumi, kijamii na kisiasa ili waweze kujikwamua.

    Mshauri katika masuala ya uongozi na utawala ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Emmanuel Mallya alisema vijana wanatakiwa kuwekeza katika afya zao kwa kuwa ndio mtaji wa kwanza kabla ya vitu vingine.

    “Usifikirie cheo kwanza kwa kuwa utachanganyikiwa na kupata msongo wa mawazo na kuhisi wanapendeleana”, alisema Dkt.Mallya.

    Ufunguzi wa mbio hizo za Marathoni ni maandalizi ya uzinduzi wa mbio zitakazofanyika 04 May, 2024 zenye lengo la kukusanya pesa ili kusaidia wanafunzi wa chuo hicho ambao wanashindwa kuendelea na masomo kutokana na kukosa ada.

  • Na Vincent Mpepo, Morogoro

    Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania amewashukuru wafanyakazi wawakilishi wa idara za kitivo hicho na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya idara, kitivo na chuo kwa ujumla.

    Mtiva, Dunlop Ochieng alitoa kauli hiyo juzi Mjini Morogoro wakati akifungua kikao kazi kwa wawakilishi wa idara mbalimbali za kitivo hicho huku wito wake ni kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.

     “Nawashukuru kwa kuja na kuendelea kufanya kazi licha ya changamoto mbalimbali”, alisema Mtiva Ochieng.

    Aidha alisema kumekuwa na changamoto katika nyaraka za kitivo na chuo ambazo zina maelekezo na gharama ambazo zinatofatiana kitu ambacho inabidi wawakilishi hao wakifanyie kazi ili kuwa na taarifa sahihi na za uhakika.

    Mratibu wa Uwasilishaji tafiti wa Kitivo hicho, Dkt. Ladisalus Batinoluho alimshukuru Mtiva kwa kuwaamini na kuwapa jukumu hilo na kwamba hawatamuangusha ili kuhakikisha kazi hiyo inafanyika kwa weledi.

    “Hata kama kutakuwa na marekebisho tupo tayari kuyafanya ili mwisho wa siku malengo ya kazi hii yafikiwe”, alisema Dtk.Batinoluho.

    Mwakilishi wa Kitengo cha Udhibiti Ubora cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Mhadhiri Msaidizi Janeth Gwimile aliema anashukuru kitivo hicho kwa kuonesha njia ya kuhakikisha kunakuwa na taarifa za uhakika na kwamba kitengo chake kushirikishwa ni jambo muhimu kwa kuwa kimekuwa kikisisitiza masuala ubora kama sehemu ya majukumu yake.

    Kwa upande wake, Mhadhiri Emmanuel Msangi alimshukuru Mtiva kwa uamuzi wake na kwamba wapo tayari kuendelea kujifunza ili kuhakikisha kila kitu kinafanyika kwa ubora.

    Mtaalamu wa Usanifu wa maandishi na machapisho, Thomas Kilumbi alisema kitivo hicho kimeonseha njia kwa kumshirikisha katika hatua za awali ambapo anaweza kufanya kazi hizo kwa kushirikiana na wahusika na kujua mahaitaji yao na wakati mwingine kushauri namna bora zaidi.

  • Na Vincent Mpepo, Morogoro

    Washarika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ) Usharika wa Mji Mpya Jimbo la Morogoro wametakiwa kuwa makini na wahubiri wanaojulikana kwa majina ya mitume na manabii kwa kuwa wakati mwingine siyo wote wana karama za uponyaji kama wanavyojinasibu.

    Tahadahari hiyo ilitolewa na Mchungaji wa KKKT Usharika wa Mji Mpya Jimbo la Morogoro, Sifu Dunia wakati wa mahubiri katika ibada ya kwanza katika usharika huo leo na kuwataka kusoma na kulielewa neno la Mungu.

    Alisema neno la Mungu halihitaji msaada wowote kwa kuwa linajitosheleza hivyo wakisoma na kuelewa itakuwa siyo rahisi kurubuniwa na mahubiri ya mitume na manabii ambao wakati mwingine huwapotosha wakristo.

    “Tusiwe wavivu kusoma neno la Mungu vinginevyo tutapokea vitu vya ajabu kwa kutegemea uponyaji na kufunguliwa”, alisema Mchungaji Sifu.

    Aliwataka washarika kutofanya mzaha na neno la Mungu kwa kuwa lina nguvu ambayo huleta matokeo kwa kadiri ya maombi na mapenzi yake.

    “Tuache mzaha na neno la Mungu kwani kufanya hivyo ni utani na Mungu mwenyewe”, alisema Mchungaji Sifu.

    Aidha aliwakumbusha washarika kumalizia ahadi za mwaka 2023 na kwamba kila mmoja ashiriki kwenye sadaka ya fungu la kumi ambayo itafanyika kila Jumapili ya mwisho wa Mwezi.

    “Kama Mungu hajakubariki usitoe kitu”, alisema Mchungaji Sifu.

    whatsapp-image-2024-02-04-at-10.35.37-am
  • Na Vincent Mpepo, CKHT

    Wafanyakazi  wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania wamekumbushwa kukamilsha ujazaji wa mfumo wa upimaji na ufuatiliaji wa malengo na shabaha ujulikanao kwa jina la PEPMIS leo 27/01/2024.

    Wito huo ulitolewa jana na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa chuo hicho, Francis Badundwa wakati wa mafunzo ya mafunzo ya uingizaji wa malengo ndani ya mfumo wa PEPMISulifanyika jana katika ukumbi wa chuo kikuu huria cha Tanzania kwa ana kwa ana na njia ya mtandao kwa wafanyakazi walio nje ya Dar es salaam.

    Alisema ni muhimu kila mfanayakazi ahakikishe amejaza taarifa zake kwenye mfumo huo ili kutoenda kinyume na maagizo ya serikali amabyo inamtaka kufanya hivyo.

    Akitoa mafunzo kwa wakuu wa vitivo, wakurugenzi na wakuu wa idara mbalimbali za chuo hicho Ramadhan Kauzen alisema mfumo huo una tofati na OPRAS kwa kuwa una vitu vya ziada ambavyo havikuwepo kwenye OPRAS.

    Alisema alisema mfumo wa PEPMIS ni tofauti na OPRAS kwa kuwa unatoa fursa na mawanda mapana kwa mwajiriwa kuweka malengo na shabaha zinazopimika tofauti na mfumo wa OPRAS.

    “Kwenye mfumo wa PEPMIS hata sehemu ya majukumu mengine utakayopangiwa na viongozi unaweza kuyaweka na yakapimika”, alisema Kauzen.

    Alisisitiza wakuu wa vitivo, wakurugenzi, wakuu wa iadara na viongozi wengine kuwakumbusha wanaowasimamia kujisajikli na kujaza taarifa zao ili wasikose mshahara Mwezi February.

  • Na Vincent Mpepo, OUT

    Chuo kikuu Huria cha Tanzania kitaendelea kushirikiana na taasisi za elimu ya juu za ndani na nje ya nchi katika kuhakikisha kuwa kinaendeleza majukumu yake ya msingi ya ufundishaji,kufanya utafiti na huduma kwa jamii kwa maslahi ya pande zote na jamii kwa ujumla.

    Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii cha chuo hicho Dkt. Dunlop Ochieng wakati akihutubia jopo la wanafunzi na wahadhiri wa Chuo kikuu Huria cha Tanzania na wageni kutoka vyuo vikuu viwili kutoka Norway iliyofanyika jana katika ukumbi wa chuo hicho jijini Dar salaam.

    Alisema chuo chake kinathamini sana uhusiano na taasisi za elimu ya juu kutoka nje kwa sababu ushirikiano huo una faida ikiwemo kudumisha na kuendeleza maarifa na ujuzi katika ufundishaji hususani mafunzo kwa vitendo kupitia huduma kwa jamii kitu ambacho kinadhihirisha mchango wa taasisi za elimu ya juu kwa jamii.

    ‘Watoto wenye mahitaji maalumu na wenye ulemavu wana mahitaji maalumu na maafisa ustawi wa jamii wanafanya kila wazezalo ili kuhakikisha watoto hao wanapata haki zao ambazo wakati mwingine hukiukwa”, alisema Dkt. Ochieng

    Alisema ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizo umesaidia kuwapa wahadhiri na wanafunzi wa kitanzania na Norway jukwaa la kutekeleza kwa vitendo wakifundisha na kusoma darasani katika mazingira halisi ya jamii.

    Mwanafunzi Mtanzania ambaye ni mkufunzi katika idara ya ustawi wa jamii ya Chuo kikuu Huria cha Tanzania, Fauzia Kitenge alisema akiwa nchini Norway alifunza vitu vingi ikiwemo suala la ustaarabu na zaidi namna ya kuishi na watu wa tamaduni za tofauti huku wito wake uikwa ni kueleza au kusimamia ukweli kwa jambo ambalo anaamini ni kweli.

    Alisema licha ya utofauti mkubwa wa kimaendeleo kati ya Norway na Tanzania bado misingi ya ubinadamu ya kujali wengine imekuwa nguzo kuu katika nchi zote mbili kama sehemu ya kuthamini ubinadamu.

    Aidha alisifu mtindo wa matibabu Norway ambao umejikita katika kuangalia tatizo la mgonjwa katika huduma za kitabibu za kibingwa na ubobevu katika maeneo mbalimbali ya afya tofauti na Tanzania ambapo wakati mwingine masuala ya matibabu huchukuliwa kwa ni kwa ujumlaujumla.

    Mwakilishi wa wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Himolde, Karoline Lie alisema uwepo wao nchini Tanzania wamejifunza vitu vingi ikiwemo tafsiri na matumizi ya nguvu katika ufundishaji au utoaji wa adhabu kwa watoto kitu ambacho ni tofauti katika utekelezaji wa sera na sheria za ufundishaji katika nchi hizo mbili.

    Alisema nchini Norway, kuna sera na mifumo thabiti ambayo imeanisha ya aina ya huduma ambazo kila raia anastahili kuzipata kama haki yake katika maeneo ya afya, elimu na huduma za ustawi jamii ambazo ni tofauti na Tanzania.

    “Kwa mfumo wa Norway, kila darasa la wanafunzi wa shule za awali na msingi linapaswa kuwa na idadi ya wanafunzi kati ya 20 na 30 na walimu zaidi ya mmoja katika kipindi kimoja”, alisema Karoline.

    Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Ustawi wa Jamii ya Chuo kikuu Huria cha Tanzania, Dtk.Mariana Makuu ushirikiano kati ya taasisi hizo unahusisha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo cha Patandi kwa Tanzania wakati kwa Norway  ni Chuo Kikuu cha Molde na Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi Shirikishi cha Western.

  • Na Vincent Mpepo, OUT

    Serikali imetakiwa kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi zake ili kuwa namna nzuri ya kutekeleza majukumu kwa taasisi, wakala na mashirika yake ili kuepusha changamoto za mafunzo ya zimatoto katika mambo yake na kufanya vitu vyenye tija kwa maslahi ya umma.

    Wito huo umetolewa na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kufutia mafunzo ya Mafunzo ya uingizaji wa malengo ndani ya mfumo wa PEPMIS jana ambayo makataa yake yakiwa ni leo 27/01/2024.

    Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mafunzo hayo baadhi ya watumishi wamesema uanzishwaji wa mambo mapya au programu mpya lazima uangalie muda na ratiba za taasisi pamoja na mafunzo ili kufanya utekelezaji uwe mwepesi kwa watumishi.