Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa mvua zitaendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali ya nchi, hasa katika kanda ya Ziwa Victoria, magharibi mwa nchi, na nyanda za juu kusini-magharibi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa, mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zinatarajiwa katika maeneo machache ya kanda ya Ziwa Victoria, magharibi mwa nchi, na nyanda za juu kusini-magharibi.
Taarifa hiyo inatoa muhtasari wa mwenendo wa mvua kati ya Novemba 21 na 30 mwaka huu na matarajio ya mvua kwa Disemba 01 mpaka 10 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, na Mara inatarajiwa kupata mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika kipindi cha siku tano za mwisho za tarehe tajwa.
Pia, mikoa ya Kigoma, Katavi, na Tabora inatarajiwa kupata mvua zinazoambatana na ngurumo za radi katika kipindi cha siku tano za mwisho.
Hali ya ukavu inatarajiwa katika mikoa ya Arusha, Manyara, na Kilimanjaro, pamoja na kanda ya kati (Dodoma na Singida).
Mamlaka ya Hali ya Hewa imetoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari na kufuatilia taarifa za hali ya hewa ili kujiandaa na mabadiliko ya hali ya hewa
Bandari ya Tanga kwa mara ya kwanza imeandika historia baada ya kupokea Meli ya MV PARNIA yenye Makontena 463 kutoka Iran.
Akiongea mara baada ya kupokea meli hiyo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Balozi Batilda Burian, alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika bandari hiyo na matunda yake kuonekana.
Alisema ujio wa meli hiyo katika Bandari ya Tanga kutoka Iran ni fursa kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Tanga na Mikoa mingine kufungua fursa za kibiashara baina ya Tanzania na Iran kwa kupitishia mizigo yao katika Bandari ya Tanga.
“Nampongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono makubwa ya kuwekeza katika Bandari ya Tanga na leo hii tumeandika historia kwa kupokea meli yenye makontena mengi jambo ambalo halikuwahi kutokea huko nyuma kabla ya maboresho”, alisema Balozi Burian.
Katika hatua nyingine Balozi Burian aliahidi kuendelea kujenga ushirikiano wa kibiashara na Iran kwa kutumia bandari ya Tanga ili kuhudumia nchi za Afrika Mashariki na nchi za Ukanda wa SADC.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Dadi Kolimba alisema ujio wa meli hiyo katika Bandari ya Tanga ni fahari kwa wananchi kwani uchumi wa Tanzania utazidi kukua na fursa za kibiashara zitazidi kufunguka zaidi.
Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa, Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Bw. Peter Millanzi alisema kwa muda mrefu Bandari ya Tanga imekuwa ikipokea meli ndogo ndogo ‘Feeder ‘ kutoka Bandari za na nchi jirani kwa sababu sababu ya uwezo mdogo wa kupokea meli kubwa za makontena.
Alisema kutokana na maboresho makubwa yaliyofanyika kwa sasa Bandari hiyo ina uwezo wa kupokea meli kubwa na matokeo yake ni hitoria kuandikwa kutokana na kupokea meli kubwa ya makontena kutoka moja kwa moja nchini Iran.
Meli hiyo yenye urefu wa mita 174 na kina cha mita 10.3 imetia nanga katika Bandari ya Tanga ikiwa na makontena 463 ambapo makontena 261 ni ya Tanzania na makontena 182 yanakwenda katika nchi za za Rwanda, Zambia, Malawi na Uganda.
Wanakikundi wa PMO LEYD wametembelea na kutoa misaada mbalimbali kwa wazee wa Kambi ya wazee Sukamahela Wilayani Manyoni, Singida.
Msaada hiyo ilitolewa na wanakikundi hao hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya taratibu na utamaduni wa kikindi hicho ili kuyafikia makundi yenye uhitaji na kwamba watumishi, mashirika na watu binafsi wajenge utaratibu wa kuwatembelea wahitaji ili kuwapa faraja na kuondoa upweke.
Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi wenzake, Makamu Mwenyekiti wa kikundi hicho Venerose Mtenga alisema kikundi chao kina utaratibu wa kutoa kwa jamii wenye uhitaji mbalimbali kama sehemu ya malengo ya kikundi hicho.
“Ninawashukuru sana watumishi wa kituo hiki kwa huduma zenu, rai yangu kwenu endeleeni kufanya kazi kwa weledi na upendo kwani pamoja na yote mnafanya pia kazi ya kumtukuza Mungu kupitia wazee hawa”, alisema Bi Venerose.
Aidha Afisa Ustawi wa Jamii katika kituo hicho, Lilian Bujiba alisema serikali inafanya kazi kubwa ya kuwahudumia wazee hao ambao wengi wao ni waliokimbiwa na familia na kuishi mazingira hatarishi na waliokua na ulemavu wa kudumu ikiwemo ukoma upofu na viungo.
“Ninawashukuru wanakikundi cha PMO LEYD kwa msaada wao na ninawaomba wanajamii, mashirika ya umma na serikali kuhjitokeza kuwasaidia wazee hao kwa kadri watakavyoguswa, alisema.
Mwenyekiti wa wazee hao, Andrea Mkung’huni alisema wamefurahi sana kutembelewa na wanakikundi hao na wamejisikia faraja sana na kujiona fahari kua kuna watu wanawakumbuka na kuwajali.
Kituo hicho kipo Mkoa wa Singida Wilaya ya Manyoni Kata ya Solya kijiji cha Sukamahela kina wazee 16 wanaume 9 na wanawake 7 na ni moja ya kambi inayohudumiwa na serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.
Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuandika na kuripoti habari zinazohamasisha amani ili kuwa na taifa endelevu katika sekta mbalimbali kwa ujenzi wa nchi.
Akizungunza na waandishi wa habari zaidi ya 100 kutoka mikoa mbalimbali nchini wakati wa mafunzo maalumu kuhusu uandishi wa habari wa amani Jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Denis Londo amewataka wanahabari kuwa mstari wa mbele katika kulinda amani kupitia kazi zao za uandishi ili kupunguza au kuondoa kabisa mogogoro isiyo ya lazima.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Denis Londo
Alisema tasnia ya habari ni wadau muhimu katika kuuhabarisha umma kuhusu masuala ya umuhimu wa jamii kupendana na kulinda amani katika kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi ili kuepusha migogoro na chuki.
Tunapaswa kuhamasisha amani na upendo miongoni mwa jamii zetu ili tuendelee kuwa wamoja kwa maslahi ya ulinzi na usalama wa taifa letu, alisema Londo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kanda ya Kusini mwa Afrika upande wa Tanzania (Media Institute of Southern Africa-MISA) Ndugu Edwin Soko, alisema vyombo vya habari nchini havitakubali kuchonganishwa na wananchi bali vitaendelea kusimamia maadili, uzalendo na weledi katika kutekeleza majukumu yao ya msingi ya kila siku.
Mwenyekiti wa MISA-TAN, Edwin Soko
“Jukumu letu kama wanahabari ni kutafuta, kuchakata na kusambaza habari sahihi kwa jamii”, alisema Soko.
Alisema sekta ya habari nchini imekuwa imara na inazidi kukua siku hadi siku na MISA-TANZANIA itaendelea kutoa mafunzo hayo ili kuimarisha msingi wa upatikanaji na utoaji wa taarifa sahihi kwa walaji (Jamii).
Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, DCP David Misime aliwapongeza wanahabari nchini kwa namna wanavyoshirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kutafuta na kuripoti matukio mbalimbali kwa usahihi na kuwaasa waandishi kuachana na habari za uchochezi.
Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi, DCP David Misime
Kwa upande wao, waandishi wa habari Keneth Ngelesi na Elizabeth Kilindi walisema mafunzo hayo ni mwendelezo mzuri wa kujenga uelewa na kuwakumbusha misingi ya taaluma yao kwa kuzingatia sheria na maadili.
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo ambao ni waandishi wa habari na viongozi wa taasisi mbalimbali za kidini nchini
Mafunzo hayo ya siku moja kwa waandishi wa habari yalifanyika katika Hoteli ya Morena Jijini Dodoma na kuhusisha wataalamu kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), wakufunzi wa vyuo vikuu, waandishi wa habari waandamizi na viongozi wa dini na yalipambwa na kaulimbiu isemayo “Sasa ni wakati wa kulijenga Taifa letu”.
The Office Management Secretary of the Open University of Tanzania’s Dodoma Regional Centre, Gracehilda Urassa, provides clarification on admission matters to newly admitted and continuing students. To her right is the Centre Director, Dr. Mohamed Msoroka. (By Vincent Mpepo).
By Ummy Kondo, Dodoma
New and continuing students of the Open University of Tanzania (OUT) have been urged to take their studies seriously and uphold discipline in order to learn effectively and complete their programs on time.
The call was made by the university’s Vice-Chancellor, Prof. Alex Makulilo, during his welcome address to new and continuing students for the 2025/2026 academic year.
He emphasized students must remain attentive to their studies at all times and follow ongoing teaching programs, especially online lectures conducted via the Zoom application.
“I would like to remind you that studying at the Open University of Tanzania requires self-discipline and commitment,” Prof. Makulilo said.
He added that the university will continue providing teaching timetables regularly so that students can follow along and avoid falling behind in their coursework.
For his part, the Director of the Dodoma Regional Centre of the Open University of Tanzania, Dr. Mohamed Msoroka, said that academic success is possible for everyone, but especially for those who are dedicated and use their time wisely.
“Be fully engaged in online and face-to-face sessions, and do not hesitate to seek help whenever you need it. Our doors are always open,” Dr. Msoroka said.
He noted that since many admitted students are adults with families, jobs, and other responsibilities, the Open University was established to offer them flexibility, freedom, and the opportunity to pursue higher education without disrupting their daily obligations.
“Success in open and distance learning requires self-discipline, commitment, and strong time-management skills,” added Dr. Msoroka.
A third-year student at the Dodoma Regional Centre, Sabina Mpigauzi, who is pursuing a bachelor degree in education, said she decided to attend the orientation sessions to gain additional information about her studies, particularly in areas she was not familiar with, to help her progress smoothly.
She also encouraged public servants and private-sector employees to advance their professional qualifications through the Open University of Tanzania, noting that the system allows them to study without interfering with other responsibilities such as employment, childcare, and family care.
A section of newly admitted students and continuing certificate, diploma, and undergraduate learners at the Open University of Tanzania’s Regional Centre follow an orientation session on Saturday. (Photo by Vincent Mpepo).
The Open University of Tanzania is a public institution that offers education through open and distance learning in accordance with its establishing legislation, and provides this service both within and outside the country.
Wanafunzi wapya na wanaoendelea wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania wametakiwa kuwajibika katika masomo na kuwa na nidhamu ili wasome na kuhitimu kwa wakati.
Wito huo ulitolewa na Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Alex Makulio katika hotuba yake ya ukaribisho kwa wanafunzi wapya na wanaoendelea kwa Mwaka wa masomo wa 2025/2026.
Alisema wanapaswa kuwa makini na masomo yao kila wakati na kufuatilia programu zinazoendelea za ufundishaji, hususani mihadhara ya inayofundishwa kwa njia ya mtanadao kupitia programu tumizi ya Zoom.
“Napenda kuwakumbusha kwamba kusoma Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kunahitaji nidhamu binafsi na kujituma”, alisema Profesa Makulilo.
Aidha alisema chuo kitakuwa kinatoa ratiba ya ufundishaji mara kwa mara ili wanafaunzi wafuatilie hivyo kutoachwa katika masomo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Mkoa cha Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dodoma, Dr.Mohamed Msoroka alisema kusoma kwa mafanikio kunawezekana kwa kila mtu lakini zaidi ni kwa wale wanaojituma huku akisisitiza watumie muda wao vizuri.
“Jihusishe kikamilifu katika vipindi na mihadhara ya mtandaoni na vile vya ana kwa ana na usisite kutafuta msaada unapouhitaji kwa kuwa milango yetu iko wazi wakati wote”, alisema Dkt.Msoroka.
Alisema kwa kuwa wadahiliwa wengi ni watu wazima, wenye familia, ajira, na majukumu mengine ndiyo maana Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilianzishwa ili kuwapatia urahisi, uhuru, na fursa ya kuendelea na elimu ya juu bila kuathiri majukumu yao.
“Mafanikio katika ujifunzaji kwa njia ya elimu huria na ya masafa yanahitaji nidhamu binafsi, kujitolea, na uwezo mzuri wa kusimamia muda”, alisema Dkt. Msoroka.
Mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Kituo cha Mkoa cha Dodoma, Sabina Mpigauzi anayesomea ualimu alisema aliamua kuhudhuria mafunzo elekezi ili kupata taarifa za ziada kuhusu masomo ili kwenye sehemu ambazo hana ufahamu nazo ili kuendelea vyema na masomo yake.
Aidha, alitoa wito kwa watumishi wa umma na sekta binafsi kujiendeleza kitaaluma kupitia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwani kinawawezesha kuendelea na masomo bila kuathiri majukumu yao mengine kama ajira. malezi na uangalizi wa familia zao.
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni chuo kikuu cha umma kinachotoa elimu kupitia mfumo wa masafa na huria kwa mujibu wa sheria ya kuanzishwa kwake na kwamba kinatoa huduma hiyo ndani na nje ya nchi.