Kusini Kwetu
Habari za ndani na nje nchi
recent posts
- RUNALI, Wadau wa Usafirishaji Wakutana Kujiandaa na Msimu Mpya wa Mazao
- Vijana, Akina Mama Nachingwea Wanufaika Mikopo 10% ya Halmashauri
- e-GA Yatoa Msaada kwa Watoto Wenye Uhitaji
- Watumishi Wanawake Bandari ya Tanga Wasaidia Mashine za Upumuaji Bombo
- DC Moyo Apongeza Utendaji Kamati ya Lishe Wilaya
about
-

By George Mwamba, Songea
Chipole Orphanage and Special Needs Center, located in Magagura Ward, Songea Rural District, Ruvuma Region, has received a donation of 1.2 million Tanzanian shillings in cash, along with food, clothing, and other essential supplies. The contribution came from the Open University of Tanzania (OUT) community, including staff, alumni, current students, and other stakeholders.
Handing over the donation yesterday at the center, OUT Assistant Lecturer Vincent Mpepo commended the caregivers for their dedication to the children’s welfare. He urged them to remain steadfast, saying their service is noble both in the eyes of people and of God.
Mpepo explained that he was personally moved after seeing photographs and video clips shared by Inspector Dominic Msangi of the Ruvuma Regional Police, who had previously served as the Ward Police Officer for Magagura village. Inspector Msangi had been appealing to institutions and well-wishers to visit the center and support the children.
“This is just the beginning. On behalf of the university and our partners, we will continue to visit and assist these children as much as we can,” said Mpepo.
He further called on the wider community to join hands in supporting vulnerable groups instead of leaving the responsibility solely to caregivers. He also expressed gratitude to the Ruvuma Regional Police for partnering with OUT to make the initiative possible.
In addition to the donation, Mpepo pledged, in collaboration with OUT management, to sponsor health insurance coverage for 50 children at the center, to ensure they can access medical care whenever health challenges arise.
For his part, Inspector Dominic Msangi noted that the initiative aligns with the Police Community Outreach Strategy, which emphasizes building partnerships with institutions and stakeholders to give back to society.
“The Tanzania Police Force works closely with educational institutions and others to strengthen social cohesion and support vulnerable groups, including children in care centers such as Chipole,” he said.
Speaking on behalf of the center, Sister Maria Akwinata O.S.B of the Chipole Benedictine Sisters congregation explained that the facility cares for children of all ages—from newborns to secondary school students. She expressed heartfelt gratitude to OUT for their support, stressing that raising the children requires ongoing assistance to meet their diverse needs.
Richard Haule, representing the children, also thanked OUT and the Police for their generosity. He said the children felt encouraged and reassured that society had not forgotten them. He appealed to other institutions, both private and public, to continue extending support to help build brighter futures for the children.
-


Na Mack Francis-Arusha
Wananchi wa Mkoa wa Arusha jana Jumamosi Agosti 23, 2025 wamejumuika pamoja kushiriki kwenye Mbio za pamoja na mazoezi ya viungo, ikiwa ni siku ya Kilele cha Tukio la Tanzania Samia Connect, linalofanyika Mkoani Arusha kuelezea mafanikio yaliyopatikana Mkoani Arusha katika Kipindi cha Miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mbio hizo ziliratibiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Kihongosi na ziliambatana na huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo matibabu bure na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya Taifa.

Kwa mujibu wa taarifa ya aliyekuwa Katibu wa Itikadi, uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa CPA Amos Makalla Kihongosi ndiye atamrithi kwa nafasi hiyo.

-
Na Sylvester Richard
Afisa Polisi Jamii Mkoa wa Singida, ACP Richard Mwaisemba amewataka wananchi wa Kata ya Makanda, Wilaya ya Manyoni, kuitii sheria na kanuni za uchaguzi mkuu 2025 bila kushurutishwa ili kulinda amani na usalama katika maeneo yao.
Akihitimisha mafunzo ya Polisi Jamii kwa vijana 32 wa kijiji cha Magasai, ACP Mwaisemba amesisitiza umuhimu wa uadilifu, nidhamu na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuzuia uhalifu.
Viongozi wa jamii wamepongeza mafunzo hayo na kuomba yaendelezwe kwa kuwahusisha vijana zaidi.
-

Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watumishi wa Hazina ndogo mkoani Kigoma kufanya kazi kwa bidii, maarifa, weledi na kuzingatia kanuni katika majukumu yao.
Wito huo aliutoa wakati wa mazungumzo na watumishi hao alipotembelea Mkoa huo hivi karibuni ambapo alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Hazina ndogo.
Alisema kufuatia juhudi zinazofanywa na serikali katika kuboresha mazingira ya kazi na namna bora ya kuwahudumia wananchi wake watumishi hao wanatakiwa kufanya kazi kiueledi.
“Serikali inafanya kazi kubwa kwa kuweka mazingira wezeshi kwa watoa huduma na kuboresha miundombinu katika sekta zote ili wananchi wapate huduma bora kwa wakati na bila upendeleo” Dkt. Nchemba.

Mkuu wa Hazina Ndogo Mkoa wa Kigoma, Frank Msaki aliishukuru serikali kwa kazi kubwa katika Kanda ya Kigoma kuhakikisha huduma muhimu zinapatokana kwa wananchi na kwa wakati.
“Sisi wasaidizi wake, tutaendelea kutoa huduma kwa kufuata misingi ya haki na uwajibikaji”, alisema Msaki..
Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Kigoma, Beatus Nchota alisema usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato katika Mkoa wa Kigoma unatokana na mwitikio mkubwa wa walipa kodi kufuatia elimu ya mlipa kodi wanayoitoa mara kwa mara kwa wafanyabiashara wa Mkoa huo.

-

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tazania anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala, Profesa Josiah Katani ni miongoni mwa waliofika katika zoezi la upimaji afya mapema jana. Anayeonekana nyuma yake ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Francis Badundwa na Profesa Cosmas Mnyanyi. (Picha kwa hisani ya Dkt. Adamu Namamba).
Na Vincent Mpepo
Wafanayakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania wametakiwa kujali afya zao kwa kupima na kupata ushauri wa kitabibu ili kujua changamoto zinazowakabili mahali pa kazi na namna ya kukabiliana nazo.
Mkurugenzi wa Rasilimali watu na Utawala wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Francis Badundwa alitoa wito huo jana ofisini kwake Kinondoni jijini Dar es salaam wakati wa mahojiano na mwandishi wetu na kuwataka wafanyakazi hao kutumia fursa ya siku tano ya uwepo wa watumishi wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) kwa zoezi hilo la upimaji afya.
Alisema kumekuwa na mwitikio mdogo wa wafanyakazi katika zoezi hilo la upimaji licha ya kukiri kuwa masuala afya ni masuala binafsi.
“Natambua wengi huenda kipima hospitali moja kwa moja ambapo watapata vipimo, majibu na tiba”, alisema Badundwa.
Kwa upande wake, Dkt. Pricila Michael kutoka Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) alianisha majukumu ya taasisi yake kuwa ni ukaguzi wa afya unahusisha upimaji wa vipimo vya awali kwa mwajiriwa mpya, upimaji wa afya wa mara kwa mara na vipimo wakati mtumishi anapomaliza muda wake wa ajira kwa kustaafu, kuachishwa au kuhama.
“Madhumuni ya kufanya zoezi hili la ukaguzi wa afya ni kutaka kujua hali ya mtumishi kiafya”, alisema Dkt.Pricila.
Alibainisha aina ya vipimo wanavyohusika navyo kuwa ni pamoja na vya uzito, urefu, shikizo la damu, hali ya lishe na uwezo wa kuona mbali ili kujua hali ya afya ya mwajiriwa kwa ujumla na mazungumzo na Daktari.
Mkaguzi wa Afya wa Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), Peter Kilimuhano alisema watumishi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania walipe kipaumbele zoezi hili la upimaji wa afya kwa kuwa ni muh9mu kwa afya zao.
Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) ni chombo cha kusimamia usalama na afya mahala pa kazi kwa kuhakikisha kwamba waajiri wote nchini wanaweka miundo na mifumo inayohakikisha usalama na afya mahala pa kazi vinalindwa.

-

Na Mack Francis-Arusha
Mkuu wa mkoa Arusha Kenani Kihongosi mapema wiki hii aliwaongoza wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Arusha kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Arusha, kumdhamini Mgombea Urais wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wananchi walioambatana na Kihongosi ni kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wajasiriamali, mama lishe na baba lishe, vijana wanaojishughulisha na usafiri wa bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na wananchi wengine,
Sababu za kumuunga mkono zinatajwa kuwa ni kutokana na mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa Mkoani Arusha kwa kipindi cha Miaka minne ya uongozi wake.


-


Na Damasi Kalembwe
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Acp Pili Misungwi amekabidhi pikipiki mbili kwa watendaji wa dawati la jinsia na watoto Wilaya ya Kimara na Kinondoni. Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika kituo cha Polisi Oystebay ambapo yamehudhuriwa na maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali Mkoa wa kinondoni.
Watendaji wa dawati la jinsia na watoto waliokabidhiwa pikipiki hizo wamepewa elimu na matumizi sahihi ya vyombo hivyo ambvyo ni kwa ajili ya kuhakikisha wanawafikia wananchi kila eneo kwa haraka na kuwapatia huduma za kutanzua ukatili wa kijinsia.
