• Na Vincent Mpepo

    Wakristo wametakiwa kufanya kila kitu wakitanguliza upendo kwani upendo huondoa changamoto mbalimbali katika maisha ya kimwili na kiroho.

    Wito huo umetolewa na Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Obed Songoyo wakati akihubiri katika ibada Siku Jumapili, katika Mtaa wa Nambere, Usharika wa SokoniII Siku ya Bwana ya sita (06) baada ya Utatu ambapo alisisitiza kufanya kila kitu kwa upendo wa Yesu.

    Mchungaji Songoyo alisema ikiwa wakristo na jamii kwa ujumla itafanya kila kitu kwa upendo kuna namna ambapo kila mmoja ataishi kwa kutimiza wajibu wake bila kumkwaza mwingine na kila mmoja ataishi kwa ajili ya mwingine.

    “Neno la Mungu linasisitiza kuishi kwa kupendana kwa kuwa upendo ndio amri kuu”, alisema Mchungaji Songoyo

    Alisema amri ya upendo ina upya ndani yake na upya huo ni kwa sababu imeongeza suala la kupenda watu wote wawe ni maadui au wasio maadui.

    “Kipimo cha kupendana sisi kwa sisi ni Yesu mwenyewe”, alisema Mchungaji Songoyo

    Alisema upendo wa kweli haushindwi na dhambi na kwamba watu huishi kwa kuvumiliana na kuchukuliana akitolea mfano wa mume na mke kuwa wanahitaji upendo wa kweli kwa kuwa mwisho wa siku wanahitajiana.
    “Tukipendana sisi kwa sisi tunadhirisha kuwa sisi ni wakristo wa kweli”, alisema Mchungaji Songoyo.

    Alisema kwa kawaida ya mila za kimasai upendo unatakiwa kuanzia nyumbani na kuwatahadharisha baadhi ya watu ambao huwapenda watu wa nje ya nyumba yao badala ya watu wa ndani na kusisitiza huo siyo upendo wa kweli.

    Alisema wanandoa hawapaswi kuishi kihasara hasara bali wanapaswa kuishi kwa kuoneshana upendo ambao utawafanya kudumu katika ndoa kwa kuwa watavumiliana na kuchukuliana na kusisitiza kuwa kuishi bila upendo ni kinyume na maagizo ya Kristo.

    Aidha aliwajulisha washarika mtaani hapo kuwa Mwinjilisti wa Mtaa huo ameteuliwa kwenda kuinjilsha Zanzibar na kuwataka wamuombee na kumuwezesha ili asiende kuwa mnyonge akiwa katika kazi ya Mungu.

    Ibada hiyo iliongozwa kwa lugha ya kimasai na tafsiri ilitolewa kwa wageni ili waweze kufuatilia ujumbe wa neno la Mungu ambapo huduma kadhaa za kichungaji zilifanyika ikiwemo ubatizo wa wototo, kurudi kundin na chakula cha Bwana.

  • By Tabia Mchakama

    Dar es salaam – In a significant stride toward safeguarding Tanzania’s agricultural sector from the adverse effects of climate change, the Tanzania Insurance Regulatory Authority (TIRA) has joined hands with CRDB Bank PLC and the National Insurance Corporation (NIC) of Tanzania to spearhead the implementation of the Tanzania Agriculture Climate Adaptation Technology Deployment Programme (TACATDP).

    The initiative, supported by the Green Climate Fund (GCF) under project FP179, seeks to strengthen the resilience of smallholder farmers through access to climate adaptation technologies and innovative financial instruments, most notably parametric (weather index) insurance.

    The high-level meeting, hosted recently at TIRA’s Mtendeni offices by the Commissioner of Insurance General, Dr. Baghayo A. Saqware, brought together top representatives from the three institutions. Among the attendees was NIC Director General, Mr. Karim Mkeyenge, and key officials from CRDB Bank including Mr. Kenneth Davis Kasigila, Head of Policy Advisory and Climate Finance, and Ms. Linda Kamuzora, Head of Bank Assurance.

    Discussions at the meeting centered on reviewing the progress of the tripartite Memorandum of Understanding (MoU) signed in May 2024. The parties acknowledged several milestones already achieved, while also addressing current challenges and laying out a roadmap for the program’s continued execution.

    A pivotal component of the TACATDP is the development and rollout of a tailor-made parametric insurance product aimed at protecting smallholder farmers from climate-related risks such as droughts and floods. This innovative product uses weather data as a trigger for payouts, ensuring timely support for farmers affected by extreme weather events.

    The collaboration emphasizes three main areas:

    1. Policy Reform and Regulatory Coordination – to foster an enabling environment for climate-responsive insurance products;
    2. Product Design and Customization – to ensure the insurance model aligns with the practical needs of Tanzania’s small-scale farmers;
    3. Capacity Building – to enhance the skills of stakeholders in promoting, overseeing, and implementing the initiative.

    CRDB Bank, as an accredited GCF entity, plays a crucial implementation role. The bank has not only facilitated funding but also technical assistance and training to build capacity for the delivery of the weather index insurance solution.

    This partnership signals a transformative approach to agricultural financing and risk management in Tanzania. The meeting’s outcomes mark a critical step toward the official launch of the parametric insurance product—a landmark move expected to revolutionize agricultural insurance and bolster climate resilience for Tanzanian farmers.

    With climate change increasingly threatening food security, the TACATDP initiative offers a timely and strategic intervention that aims to secure livelihoods and promote sustainable agriculture for generations to come.

  • Na Vincent Mpepo

    Wadahiliwa wapya wa shahada za uzamili na uzamivu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kituo cha Mkoa wa Dodoma wametakiwa kutumia muda vizuri ili kuhakikisha wanamaliza programu walizodahiliwa ndani muda uliopangwa.

    Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha Mkoa cha Dodoma, Dkt. Mohamed Msoroka wakati wa ufunguzi na uwasilishaji wa mafunzo elekezi yaliyofanyika Jumamosi katika ukumbi wa mitihani wa kituo hicho na kuhudhuriwa na wanafunzi wa shahada za juu waliodahiliwa katika fani mbalimbali.

     Alisema baada kudahiliwa na kukubali kusoma ni lazima wakubali kupunguza baadhi ya vitu au majukumu mengine ya kijamii ili watumie vizuri muda katika masomo.

    “Wakati mwingine utalazimika kuacha posho za vikao, safari au shughuli za kijamii kama ndoa na nyinginezo ili utumie muda wako katika elimu”, alisema Dkt. Msoroka.

    Aliwataka kufuata taratibu na maelekezo mengine kwa mujibu wa miongozo ya chuo ikiwemo kuwasiliana na wasimamizi wao wa utafiti katika safari yao ya elimu.

    “Usikae na changamoto badala yake wasiliana na msimamizi wako upate ufumbuzi na ushauri wa namna ya kuendelea na masomo yako”, alisema Dkt. Msoroka.

    Alisema furaha ya walimu, wakufunzi na wahadhiri ni kuona wanafunzi wao wanamaliza masomo yao kwani ni jambo la faraja badala ya kuona hawamalizi kwa wakati.

    Akitoa mafunzo ya mifumo ya Tehama inayoyumika chuoni hapo kusomea na kujifunzia ya chuo hicho, Hassan Mwazema alisema mifumo hiyo inatoa nafasi nzuri ya mwanafunzi kupata huduma mbalimbali hata bila kufika ofisini kwa kuwa inasomana na mifumo mingine ya kitaifa ili kumhakikishia urahisi wa huduma.

    “Uzuri ni kuwa mifumo yetu inasomana hivyo si lazima sana kuja ofisini kwetu kwa kuwa unaweza kufanya kila kitu mahali ulipo”, alisema Hassan.

    Mdahiliwa wa Shahada ya Umahiri ya Sanaa katika Ushirikiano na Maendeleo ya Kimataifa (MAICD) choni hapo, Hafsa Lyimo alisema kama mama, mke na mzazi amependa kusoma Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kutokana na fursa ya kupangilia masuala mbalimbali ya kifamilia, kiofisi na kitaaluma na hivyo kuhakikisha kila kimoja kinapata muda wake.

    “Kama mwanamke kitu kilichonileta kusoma Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni kuhakikisha kuwa na ndoto yangu inatimia”, alisema Hafsa.

    Aliwataka wanawake kutumia fursa zilizopo katika eilimu badala ya ya kuwa na visingizio vingi ambavyo kimsingi havina uhalisia ili kutimiza ndoto zao ili kuongeza thamani ya maisha yao katika jamii.

    Katika mafunzo hayo. wadahiliwa hao wa shahada za umahiri na uzamivu walifundishwa masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kusoma katika mfumo wa elimu huria na masafa, namna ya kutumia mifumo ya Tehama ya chuo hicho na taratibu mbalimbali kuhusu wajibu wa wanafunzi na wasimamizi wa tafiti.

  • Na Issa Mwadangala

    Wazazi na walezi wa Kijiji cha Ikonya kilichopo Kata ya Bara Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe wametakiwa kuhakikisha malezi ya watoto yanazingatia maadili ya dini.

    Hayo yamesemwa na Naibu Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Songwe Mrakibu wa Polisi (SP) Ester Ngaja juzi wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa paa la Kanisa Katoliki Kigango cha Ikonya ambapo aliwataka waumini wa Kanisa hilo kuwalea watoto kwa kuzingatia mafundisho ya dini ili kuwaepusha kujiingiza katika tabia za kihalifu.

    “Kanisa linapaswa kuwa mahali sahihi kwa malezi kwa kushirikiana na familia na jamii kwa ujumla,” alisema SP Ngaja.

    Katika hafla hiyo ya harambee, ikiongozwa na mmoja wa wazaliwa katika kata hiyo Bi Mariam Nzowa alisema kuwa baada ya kutembelea kanisa hilo alikuta changamoto ya waumini kukosa sehemu ya kusalia kutokana na kanisa kutokuezekwa ndipo alipochukua hatua ya kufanya harambee ili kukusanya kiasi cha shilingi milioni saba (7) kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo.


    Tukio hilo lilihudhuriwa na viongozi wa dini, wanajamii na wageni mbalimbali walioungana kwa moyo mmoja katika kuchangia maendeleo ya kanisa.

    kwa upande wake Padre wa Parokia ya Bara Attilio Mbogela aliwapongeza waumini wa Kijiji cha Ikonya kwa mshikamano wao na moyo wa kujitolea katika kazi za maendeleo na kuhimiza waendelee kudumisha upendo, mshikamano na heshima kwa taasisi za kidini.

    Aidha, alilishukuru  Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe na mgeni rasmi Bi. Mariam Nzowa kwa ushirikino na mchango mkubwa katika mafanikio ya harambee hiyo huku akiahidi kuendelea kushirikiana na jamii na viongozi wa serikali katika kuimarisha maadili mema miongoni mwa waumini na jamii kwa ujumla.

  • By Vincent Mpepo

    Newly admitted master’s and doctoral students at the Open University of Tanzania have been urged to manage their time wisely to ensure they complete their respective programs within the scheduled time frame.

    The advice was given by the Director of the Dodoma Regional Centre, Dr. Mohamed Msoroka, during the orientation and introductory training held on Saturday at the Centre’s examination hall, which was attended by newly enrolled postgraduate students from various disciplines.

    He emphasized that once a student has enrolled and committed to study, they must be willing to sacrifice certain things or reduce some social responsibilities to dedicate enough time to their studies.

    “At times, you may have to forgo sitting allowances from meetings, trips, or social activities like weddings and others in order to focus on your education,” said Dr. Msoroka.

    He advised the students to adhere to the university’s guidelines and instructions, including maintaining communication with their research supervisors throughout their academic journey.

    “Don’t sit with your challenges in silence. Instead, communicate with your supervisor to get guidance and solutions to help you continue smoothly with your studies,” he said.

    He noted that the joy of teachers, lecturers, and academic staff is to see their students complete their studies successfully, which is far more satisfying than seeing them drop out or delay completion.

    During the session on the university’s ICT systems used for learning and academic services, Mr. Hassan Mwazema explained that the university systems provide students with access to various services even without physically visiting the university offices, as they are integrated with national systems to enhance service delivery.

    “The good thing is that our systems are interconnected, so you can handle everything from wherever you are without necessarily coming to our offices,” said Hassan.

    Hafsa Lyimo, a student pursuing the Master of Arts in International Cooperation and Development (MAICD) at the university, shared that as a mother, wife, and parent, she chose to study at the Open University of Tanzania because of the flexibility it offers in balancing family, work, and academic responsibilities, allowing her to allocate time to each area effectively.

    “As a woman, what inspired me to study at the Open University of Tanzania is the desire to fulfill my dream,” said Hafsa.

    She encouraged women and the general public to take advantage of available educational opportunities rather than making excuses that, in reality, have no strong basis to fulfill their dreams and enhance the quality of their lives in society.

    During the orientation, the postgraduate students were trained on various topics, including how to study under the open and distance learning system, how to use the university’s ICT platforms, and the roles and responsibilities of both students and research supervisors.

  • Na Issa Mwadangala, Songwe

    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Augustino Senga, ameongoza matembezi kwa vyombo vya usalama mkoani humo Julai 25, 2025.

    Akizungumza mara baada ya mazoezi hayo ya utimamu wa mwili, Kamanda Senga alisema kuwa lengo la mazoezi hayo ni kujenga umoja, ushirikiano na kuimarisha afya ya mwili na akili kwa vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani humo.

    Aidha, Kamanda Senga alizungumzia umuhimu wa afya njema kama nguzo muhimu katika utendaji wa kazi na maisha kwa ujumla na kuwahimiza Askari na Watumishi wengine kupenda kufanya mazoezi kwa faida ya afya zao.

    “Afya bora ni msingi wa ufanisi kazini na maisha ya baadaye”, alisema Kamanda Senga

    Alisema ni mihimu kuhakikisha kuwa mwili na akili imara si tu kwa ajili ya sasa bali pia kwa maisha baada ya kustaafu.

    Katika matembezi hayo wadau mbalimbali kutoka vyombo vya ulinzi na usalama walishiriki ikiwemo Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Jeshi la Kujenga Taifa, Jeshi la Magereza, Jeshi la Zimamoto na Uokozi pamoja na Ofisi ya Rais.

    Matembezi hayo yanatajwa kama sehemu ya msingi katika kuendeleza umoja na mshikamano siyo tu miongoni mwa vyombo vya ulizni na usalama  bali pia mahusiano mema na jamii kwa maendeleo ya Mkoa wa Songwe.

  • Na Rehema Kavishe

    Waandishi wa habari chipukizi wametakiwa kusoma kwa bidi ili kuwa na maarifa stahiki katika fani hiyo yatakayowawezesha kuendana na ushindani wa soko la ajira na ikibidi kuwa wajasiriamali katika maeneo mbalimbali ya tasnia hiyo.

    Hayo yamejiri wakati wa ziara ya Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Vincent Mpepo katika Chuo cha ‘Spring Institute of Business and Science’ hivi karibuni Mkoani Kilimanjaro ambapo aliwaasa mambo kadhaa ikiwemo faida za kujiendeleza kitaaluma.

    Akizungumza na wanafunzi wanaosomea fani ya uandishi wa habari na utangazaji chuoni hapo aliwataka kusoma kwa bidi ili kuhumili ushindani na kujiongezea wigo wa upatikanaji wa ajira na kujitengenezea fursa kwa ajili ya masomo ya juu.

    “Jitahidi uwe na ufaulu mzuri kuanzia GPA ya 3 ambayo ndiyo sifa ya kudahiliwa kusoma shahada awali”, alisema Mpepo.

    Pamoja na ushauri huo, Mpepo aliwasilisha vitabu vya masomo ya habari na utangazaji vitakavyowasaidia kujiongezea maarifa na maandalizi ya mitihani yao.

    Mwanafunzi wa stashahada ya uandishi wa habari na utangazaji chuoni hapo, Careen Kisanga alisema wamepokea vitabu hivyo na wanatoa shukrani kwa mhadhiri huyo.

    Mkuu wa Idara ya Uandishi wa Habari na Utangazaji chuoni hapo, Amos Majaliwa aliwakumbusha wanahabari wanafunzi hao kuwa na nidhamu katika masuala ya kitaaluma ili kuwa na matokeo mazuri kinadharia na vitendo ambayo ndiyo mtaji mzuri katika soko la ajira.

    “Ni muhimu mfanye vizuri ili kuwa na viwango vizuri vya ufaulu kwa asilimia 80 au 90”, alisema Majaliwa.

    Alisema uvivu na kutokujifunza kwa bidii ni vikwazo dhidi ya malengo mazuri wanayojiwekea na kusisitiza kuwa mafanikio katika taaluma hutegemea juhudi binafsi na kujituma.

    Kwa upande wake mwanafunzi wa mwaka wa pili katika fani ya uandishi wa habari na utangazaji chuoni hapo, Juliani Kimaro alielezea umuhimu wa kujiendeleza kitaaluma katika tasnia hiyo na kuwa ataongeza bidii ili kufikia maleongo yake.

    Aidha alielezea kufurahishwa na ziara ya mhadhiri huyo kwani wamepata uzoefu wa fursa mbalimbali zilizopo katika tasnia ya habari, sifa na vigezo vya kujiunga na masomo ya shahada katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

    “Leo tumepata uelewa kwa kuwa tumejifunza kuwa uandishi wa habari si kazi tu bali, ni taaluma yenye uzito na majukumu makubwa kwa umma,”, alisema Juliani.

  • Na Mwandishi Wetu

    Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ally Ussi amempongeza Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba kwa usimamizi madhubuti na utoaji wa fedha katika miradi mbalimbali ya maendeleo nchini. 

    Ussi alitoa pongezi hizo wakati wa ukaguzi na uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa daraja la Konkilangi na barabara ya maingilio kiwango cha changarawe yenye urefu wa Km 1.5 katika Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

    Alisema pongezi hizo ni matokeo ya ustawi wa jamii kiuchumi kutokana na usimamizi mzuri wa fedha za maendeleo zinazotolewa na serikali katika utekelezaji miradi ya maendeleo nchini ambayo imekuwa na matokeo chanya.

    “Tumeona hayo katika miradi ya ujenzi wa miundombinu ya katika sekta za maji, afya, elimu, umeme na kadhalika”, alisema Ussi.

    Alisema kazi hiyo nzuri inatokana na wajibu anaobeba kumsaidia Rais katikakuhakikisha wanafikiwa na huduma muhimu.

    Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba alisema serikali imedhamiria kusogeza huduma zote muhimu wa wananchi kwa kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) 2020-2025 na imefanya kwa kiwango kinachostahili.

    Alisema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa kiongozi imara katika kushughulikia changamoto zinazowakabili Wananchi wote Nchin kwa kuboresha mazingira ya huduma hizo muhimu kwa maendeleo ya Taifa

    Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zimeongozwa na Kauli mbiu isemayo ‘Jitokeze Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa amani na Utulivu’.

  • Na Issa Mwadangala.

    Madereva wa vyombo vya moto wanaofanya safari zao Barabara ya Mbeya-Tunduma wametakiwa kuacha tabia ya kuendesha vyombo hivyo kwa mazoea ili kupunguza ajali za barabarani.


    Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Raphael Magoma aliyasema hayo jana wakati akitoa elimu kwa madereva na abiria katika eneo la ukaguzi wa magari lililopo Chimbuya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe huku akiwataka kufuata sheria na miongozo ya usalama barabarani.


    “Mnapaswa kujitathmini na kuacha tabia ya kufanya kazi kwa mazoea”,alisema Magoma.

    Alisema kila safari ni ya kipekee na inahitaji umakini wa hali ya juu kulinda maisha maisha ya watu wasio na hatia.

    Aidha, aliwataka madereva hao kuzingatia sheria za usalama barabarani ikiwemo kutozidisha mwendo, kutoendesha wakiwa wamelewa na kuhakikisha vyombo vyao vya usafiri vipo katika hali nzuri kabla ya safari.

    “Ninawataka abria mtoe taarifa kuhusu madereva wazembe ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi yao”, alisema Magoma.

  • Na Vincent Mpepo

    Vijana wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mtaa wa Kwembe wameelezea mafanikio, fursa na changamoto zinazowakabili katika safari ya kujikwamua kichumi kama sehemu ya jamii huku wakitoa rai kwa washarika na jamii kuwaunga mkono katika harakati zao.

    Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Vijana Mtaani hapo, Abel Mvungi Siku ya Jumapili ambayo kwa kalenda ya KKKT ilikuwa ni Siku ya vijana ambapo vijana hao walitumia siku hiyo kuonesha talanta zao katika maonesho ya kazi za mikono, bidhaa na huduma wazitoazo kama sehemu ya shuhguli wazifanyazo ili kukuza mfuko wao na kujikwamua kichumi.

    Alisema pamoja na kumtumikia Mungu katika utume na shughuli mbalimbali za kikanisa wanahitaji kuungwa mkono na washarika na jamii ya wanakwembe ili waendelee kuwa imara kiuchumi na hivyo kupunguza utegemezi kwa wazazi na walezi.

    “Tunaomba muendelee kutushika mkono katika miradi mbalimbali ikiwemo huu wa matunda na mbogamboga ili kuisukuma mbele idara ya vijana katika kutekeleza malengo yake ya kuwainua vijana”, alisema Abel.

    Akizungumzia mafanikio ya umoja huo mtaani hapo, alisema wa Mwaka jana 2024 umoja huo ulifanikiwa kuhudhuria Kongamano la vijana jijini Arusha amabalo lililenga kuwafundisha vijana kumjua Mungu na namna bora ya kuishi katika jamii inayowazunguka.

    “Viongozi walipata safari ya kwenda Dodoma kwa ajili ya kongomano la kiuongozi”, alisema Abel.

    Alibainisha mafanikio mengine kuwa ni kuwawezesha vijana 103 kushiriki Tamasha la Twen’zetu kwa Yesu lililofanyika Kawe jijini Dar es salaam na kuwashukuru washarika wa Mtaa huo kwa kuwaunga mkono katika ununuzi wa tiketi kwa baadhi ya vijana ili washiriki katika kongamano hilo.

    Alisema Mwaka 2024 umoja huo uliazimia kuanzisha mradi wa pikipiki tatu yaani bodaboda kwa kufanya harambee ndogo Tarehe 7/7/2024 ambazo zingetumiwa na vijana kanisani kama sehemu ya ajira na kuuzalishia mfuko wa vijana fedha. 

    “Katika harambee hiyo tulifanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 1,300,000/ taslimu na ahadi za shilingi 2,600,000/ ambazo hazijalipwa mpaka leo hivyo kufanya mradi huo kutokufanikiwa kwa wakati”, alisema Abel.

    Mhubiri wa siku hiyo, Kresensia Kabala alizungumzia umuhimu wa vijana kuwa na nidhamu katika kila walifanyalo kwani kupitia nidhamu ndio inaonesha thamani ya ujana katika jamii  kinyume na hilo ni kuonekana hawafai.

    “Jitengenezee mazingira yatakayowakosesha watu na jamii sababu za kukukudharau”, alisema Kresensia.

    Aliwataka vijana kufanya kazi na wakati mwingine kutochagua kazi hata kama wamesoma hususani wakati huu ambapo kuna changamoto ya upatikanaji wa ajira.

    Aidha aliwaasa wazazi kuwafundisha kazi watoto wao ili waweze kujitegemea badala ya kuwalea kama mayai kitu ambacho ni janga katika masiha yao ya baadaye kama akina baba na akina mama watarajiwa.

    “Matatizo mengi katika ndoa yanatokana  na msingi mbovu wa malezi katika familia”, alisema Kresensia.

    Aliwaasa vijana wa kike na wa kiume wanaosoma kutumia vizuri muda wao shuleni na vyuoni katika kuandaa kesho yao na kuacha tamaa kwani itasababisha upotevu wao na kuwapa majonzi wazazi na walezi amabao hutumia rasilimali zao kuhakikisha wanapata elimu.

    Mchunganji Dkt. Mwatumai Mwanjota alihudumu katika ibada hiyo na huduma za kichungaji kadhaa zilifanyika ikiwemo ubatizo na huduma ya chakula cha Bwana.

    Siku hiyo ilipambwa na uimbaji kutoka kwa vijana huku huduma zote kanisani hapo zikiendeshwa nao jambo  lililoonesha hazina kubwa ya talanta na vipawa mbalimbali kwa vijana hao ambao wakipewa nafasi wanaweza kuidhihirishia jamii thamani yao.