Na Vincent Mpepo, OUT
Serikali imetakiwa kuweka mazingira wezeshi kwa taasisi zake ili kuwa namna nzuri ya kutekeleza majukumu kwa taasisi, wakala na mashirika yake ili kuepusha changamoto za mafunzo ya zimatoto katika mambo yake na kufanya vitu vyenye tija kwa maslahi ya umma.
Wito huo umetolewa na wafanyakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kufutia mafunzo ya Mafunzo ya uingizaji wa malengo ndani ya mfumo wa PEPMIS jana ambayo makataa yake yakiwa ni leo 27/01/2024.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mafunzo hayo baadhi ya watumishi wamesema uanzishwaji wa mambo mapya au programu mpya lazima uangalie muda na ratiba za taasisi pamoja na mafunzo ili kufanya utekelezaji uwe mwepesi kwa watumishi.
Leave a comment