
Na Cartace Ngajiro, Tanga
Serikali imepongezwa kwa kuendelea kuboresha bandari nchini na kuziwezesha kukusanya baadhi ya mapato “Wharfage” jambo ambalo limeongeza ufanisi katika utendaji.
Pongezi hizo zilitolewa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uchukuzi Ludovick Nduhiye hivi karibuni wakati ziara yake katika bandari ya Tanga kujiuonea utendaji kazi wa bandari hiyo.
Akipokea taarifa ya mradi wa maboresho yaliyofanyika katika bandari hiyo Nduhiye alisifu mfumo mzima wa utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ambao umesaidia ongezeko la makusanyo ya mapato bandarini hapo.
“Kukua kwa mzigo toka shehena tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka inaonyesha kwa kiasi gani maboresho hayo yamezaa matunda matunda”. Alisema Nduhiye
Kwa upande wake, Meneja wa Bandari ya Tanga, Masoud Mrisha alisema kukamilika kwa mradi huo kumeleta ufanisi, tija na faida ikiwemo uharaka katika kuhudumia Meli ongenzeko la idadi ya meli, na kupungua kwa gharama za uendeshaji.

Leave a comment