Hawa Mikidadi, Morogoro

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Morogoro, Nuru Ngereja amewaomba waandishi wa habari kuendeleza ushirikiano na chama chake ili kuwatumikia wananchi katika utekelezaji wa ilani ya chama.

Kauli hiyo aliitoa Tarehe 24.03.2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha na kuwatambua waandishi wa habari wa mkoa huo.

“Katika kipindi ambacho nitakuwepo hapa ninaamini tutafanya kazi pamoja”, alisema Ngereja.

Alisema kupitia kalamu zao wana kila sababu ya kushirikiana na chama ili kufanikisha utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii ya wana Morogoro.

Posted in

Leave a comment