
Na Tabia Mchakama
Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeshiriki na kudhamini tuzo katika Mkutano wa Wadau wa elimu ulioandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Sinyamule uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii jijini Dodoma.
Katika Mkutano huo, Kamishna wa Bima Dkt. Baghayo Saqware aliitaka jamii kukata bima kutokana na manufaa yake katika ulinzi wa afya zao, mali zao na za mali za serikali.
“Bima ni sehemu ya kujiongezea kipato kwa kuwa wakala wa bima”, alisema Kamishna Dkt. Saqware.
Mgeni Rasmi wa Mkutano huo alikuwa Dkt. Doto Biteko ambaye kutokana na majukumu mengine aliwakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi. Rosemary Sinyamule.
Mkutano huo uaneda sanjali na utekelezaji wa kauli mbiu isemayo ‘Uwajibikaji Wangu ni Msingi wa Kuinua Ubora wa Elimu na Ufaulu Dodoma’ na ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu zaidi ya 2,000.
Waliotunukiwa tuzo hizo ni walimu, wanafunzi, shule na Wilaya, zilizofanya vizuri katika mitihani ya darasa la nne, darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha Sita kwa mwaka 2024 katika Mkoa wa Dodoma.
Tuzo hizo zinatajwa kuwa chachu na hamasa kwa waliofanya vizuri na inatarajiwa kuwa chachu kwa wengine kuongeza bidii katika mitihani ijayo hivyo kuinua kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi kiwilaya, kimkoa na kitaifa.

Leave a comment