Na Vincent Mpepo, Kwembe

Jamii imetakiwa kuwakumbuka wahitaji na wenye mahitaji maalumu katika huduma mbalimbali ikiwemo mavazi, chakula na mahitaji mengine ya msingi ili waendelee kuishi vyema kimwili na kiroho kama sehemu ya wanajamii.

Wito huo umetolewa Jumapili na Mwalimu Israel Mmari katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Mtaa wa Kwembe wakati akihamasisha uchangiaji wa sadaka maalumu ya udiakonia kwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu kinachotarajiwa kuhamishiwa Kitopeni Bagamoyo kutoka Kijichi jijini Dar es salaam kutokana na mahali kilipo sasa kuwa siyo salama.

Alisema bado kuna namna ambapo kila mtu kwa nafasi yake au familia au mashirika iwe ya umma na binfasi yanatakiwa kuwakumbuka wahitaji kwa namna moja au nyingine ili kuwasadia katika kuhakikisha mahitaji yao ya msingi yanapatikana.

“Kuna mahali ambapo maombi peke yake hayasaidii ni lazima ufanye kitu cha ziada ikiwemo sadaka na matendo ya huruma”, alisema Mwalimu Mmari.

Alibainisha wahitaji wengine ambao wanahitaji misaada mbalimbali ya kibinadamu katika jamii kuwa ni pamoja na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, wajane, wafungwa na wagonjwa.

Aidha aliitahadharisha jamii dhidi ya matumizi mabaya ya mitanadao ya kijamii na kwamba wapo ambao huitumia vibaya kuharibu wasifu na sifa za wengine.

“Wapo watu ambao hugharimia mambo yanayowaumiza wengine kupitia mitandao ya kijamii”, alisema Mwalimu Mmari.

Aidha aliwakumbusha wazazi na walezi kujuenga mazingira mazuri na wezeshi kwa watoto wao ili wakue katika namna njema badala ya mazingira ambayo yatakuwa magumu kwao.

Mwalimu wa Shule ya Jumaipili, Thomas Lukindo akifundisha watoto kama alivyoonekana na mpiga picha wetu Siku ya Jumapili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Mtaa wa Kwembe, (Picha na Vincent Mpepo).

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi umebaini kuwa matendo ya huruma kwa wanajamii huwa yanafanyika nyakati za mifungo ya kiimani mfano Kwaresma kwa wakristo na Mwezi Mtukufu wa Ramadani kwa waislamu wakati kiuhalisia mahitaji kwa watu wa Makundi Maalumu yapo muda wote.

Mwandishi anadhani ifike  mahali jamii ione kuwa mahitaji kwa wahitaji ni sehemu ya maisha ya kila siku na siyo siku za mifungo au msimu tu hivyo jamii ibadilike na kuwathamini wahitaji nyakati zote na ikibidi wafanye kwa kudhamiria kutoka ndani siyo kwa maonesho na kujitangaza kama inavyofanyika sasa.

Mwalimu Joyce Kamugisha wa shule ya Jumapili akifundisha watoto katika ibada katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Mtaa wa Kwembe, (Picha na Vincent Mpepo).

Posted in

Leave a comment