Na Gabriel Alex Msumeno, Kibaha

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Phillip Mpango ameongoza wananchi na wakazi wa Mkoa wa Pwani katika sherehe za uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa zilizofanyika Leo katika viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha.

Akizungumza wakati wa sherehe hizo Dkt.Mpango amewataka watanzania kutumia vizuri haki yao ya kidemokrasia kwenye uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika baadaye Oktoba 2025.

“Kila mtanzania mwenye sifa atImize haki yake ya kikatiba KUmchangua kiongozi anayemtaka ili kuendelea kulinda amani na utulivu wa nchi yetu”, alisema Dkt Mpango.

Aidha alibainishwa kuwa licha ya Mwenge wa Uhuru 2025 kuwa na kauli mbiu inayosema “Jitokeze kushiriki uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu”, umebeba ujumbe kwa watanzania kuhusu masula mengine ikiwemo lishe bora kwa afya imara, mapambano dhidi ya rushwa, VVU/UKIMWI, dawa za kulevya na ugonjwa wa Malaria.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbal wa chama na serikali wakiwemo Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu, Rais Mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne Dkt.Jakaya Kikwete, Naibu Spika wa Bunge la Jumhuri ya Tanzania, wakuu wa taasisi za umma, vyombo vya ulinzi na usalama, watumishi wa serikali na taasisi binafsi, wasanii na wananchi kwa ujumla.

Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Mikoa 31 kwa muda wa siku 195 ukizindua miradi mbalimbali na katika Mkoa wa Pwani utazindua jumla ya miradi 64 yenye thamani ya shilingi Trilioni1.2.

Posted in

Leave a comment