Sehemu ya wanakwaya wa USCF Mlimani CCT wakihudumu katika ibada ya kwanza katika anisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Mbezi Luis siku ya Jumapili, (Picha Vincent Mpepo).

Na Vincent Mpepo

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam wameushukuru uongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Mbezi Luis kwa kuwapokea na kuwahudumia vizuri walipokua usharikani hapo kwa kambi Maalumu ya siku tatu.

Shukrani hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kwaya ya USCF Mlimani CCT, Joshua Richard wakati wa ibada ya kwanza mbele ya washarika alipokuwa akitoa salamu za shukrani na kwamba wamefarijika kwa namna wa uongozi wa kanisa na vikundi mbalimbali walivyowakarimu.

Alisema wametembelea sehemu nyingi kwa kambi lakini Usharika wa Mbezi Luis ni moja ya Sharika zilizowapokea na kuwakarimu vizuri kwani wameonja upendo na kujaliwa muda wote walipokuwa usharikani hapo.

Alisema madhumuni ya kambi hiyo Maalumu ni kwa ajili ya maombi na masuala mbalimbli ya kiimani kwa vijana na kwamba ni utaratibu waliojiwekea kila mwaka wanafanya hivyo ikiwa ni sehemu ya kukulia kiimani kwani kanisani ndio mahali salama zaidi.

“Vijana kujihusisha na masuala ya Mungu tunanakuwa salama zaidi kwani itatuepusha na mambo mengi yasiyofaa ikiwemo madawa ya kulevya”, alisema Richard

Alisema vijana wakiandaliwa vyema kiroho familia, jamii na taifa kwa ujumla limepona kwa kuwa watajitambua na kuwa wanajamii wanatabua wajibu wao.

Kambi hii ya maombi ilikuwa na vijana wa kike na wa kiume 132 tangu Ijumaa mpaka Jumapili, alisema Richard

Mwalimu Gadielson Mfinanga katika mahubiri siku hiyo aliwakumbusha wakristo kutoruhusu changamoto wanozaopitia kubadili uhalisia wa Mungu katika maisha yao kwani kufanya hivyo kutawagharimu baada ya hali hiyo kuisha.

Alisema Mungu ana tabia ya kuwabakiza watu ambao hata baada ya changamoto mbalimbali zinazowakabili wataedelea kutembea nao katika nyakati za huzuni au furaha.

“Ni muhimu sana kuwathamini wengine bila kuwahukumu au kuwadharau kwani huwezi kujua ni wakati gani watakufaa”, alisema Mwalimu Mfinanga.

Alisema matokeo ya kila mmoja na alivyo ni mjumuisho wa namna wa watu aliokutana nao katika maisha yake.

Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Mbezi Luis, Godlsiten Nkya aliwashukuru vijana wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwamba wanafanya kazi njema machoni pa Mungu.

Aidha, aliwakumbusha wazazi wa Dar es salaam kujiuliza ikiwa vijana wao wanaosoma vyuoni hususani Chuo Kikuu cha Dar es salaam kama wanajishughulisha na masuala ya kiimani kwa kati ya vijana 132 walifika usharikani hapo hawakuzidi 10 kutoka Dar es salaam.

“Ni wajibu wa wazazi kuwakumbusha vijana wao wasiende na maisha bila Mungu”, alisema Mchungaji Nkya.

Alisema wakati vijana hao wakijishughulisha na kwaya na masuala ya kikanisa wapo wengine ambao wamejiingiza kwenye mambo yasiyofaa ikiwemo ulevi.

Posted in

2 responses to “UDSM Wawashukuru Mbezi Luis kwa Ukarimu”

  1. Lucas Lutemba avatar
    Lucas Lutemba

    Ameeen sana kazi ni njema sana Mungu wa Mbinguni akubariki sana
    LAKINI
    Hapoo kwenye mwenyekiti wa kwaya inatakiwa awe mwenyekiti wa USCF
    Maana mwenyekiti wa choir na USCF ni tofauti.
    Ameeen barikiwa sana na Yesu

    Like

    1. mpepovincent0 avatar
      mpepovincent0

      Asante kwa kunirekebisha, nitajitahidi wakati mwingine nisirudie kosa hilo. Barikiwa sana mtumishi.

      Like

Leave a comment