
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi akipanda mti kama ishara ya kutunza mazingira na uboreshaji wa nishati ya jua katika Hospital ya Mchukwi.
Na Gabriel Msumeno, Pwani
Mwenge wa uhuru umezindua miradi sita ya maendeleo katika sekta za elimu na afya Wilayani Kibiti Mkoani Pwani yenye thamani ya shilingi milioni 600.
Akizindua miradi hiyo, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Ismail Ali Ussi aliwataka wananchi kuitunza ili iwe na manufaa kwa kizazi cha sasa na cha vizazi vijavyo ili kuboresha maisha.
Miradi iliyozinduliwa ni ya ujenzi wa matundu sita ya vyoo na vyumba vinne vya madarasa katika Shule ya Msingi Kibiti.
Miradi mingine ni pamoja na uzinduzi wa mashine mbili za kisasa za kubangulia korosho katika chama cha vijana cha Kibiti Cashernuts, uzinduzi wa nishati safi ya kupikia katika Shule ya Sekondari Kibiti na mradi wa maji katika kata ya Bungu.
Aidha, Kionbgozi wa Mbio za Mwenge Kitafia alishiriki upandaji mti ikiwa ni ishara ya kutunza mazingira na uboreshaji wa nishati ya jua katika Hospital ya Mchukwi.

Leave a comment