
Na Gabriel Msumeno, Pwani
Watanzania wametakiwa kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 ili kutimiza haki yao ya kikatiba ya kuwachagua viongozi watakaowaongoza kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo.
Wito huo umetolewa na Mkimbiza Mwenge Kitaifa, Ismail Ali Ussi akiwa katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani ambako anaendelea kukimbiza Mwenge wa Uhuru.
“Kila mtanzania mwenye umri wa kuanzia miaka 18 anapaswa kushiriki uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”, alisema Ussi.
Mwenge wa Uhuru umezindua miradi 5 na kuweka jiwe la Msingi kwenye mradi mmoja na kufanya jumla ya miradi iliyotembelewa katika Wilaya ya Kibaha ikiwa na thamani ya zaidi yaTsh Milioni 748.
Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 inasema “Jitokeze kushiriki uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa amani na utulivu”.
Leave a comment