Na Farida Mkumba, Dodoma  

Ofisi ya Rais – TAMISEMI imeomba Shilingi trilioni 11.78 kwa matumizi ya mwaka wa fedha 2025/2026.

Katika hutuba aliyoisoma Leo jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa alibainisha kuwa Trilioni 3.95 zitakwenda kwenye miradi ya maendeleo, na Trilioni 7.84 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Waziri Mchengerwa alisema bajeti hiyo inakusudia kuleta matumaini na maendeleo kwa wananchi wote na kusisitiza ushirikiano kati ya serikali, mikoa, na wananchi.

Aidha, amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mwelekeo mzuri wa maendeleo kwa watanzania.

Bajeti ya TAMISEMI kwa mwaka huu wa fedha imeongezeka ikilinganishwa na mwaka uliopita ambapo ilikuwa trilioni 10.13.

Posted in

Leave a comment