Na Gabriel Msumeno

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkuranga Omary Mwanga amewataka wakazi wa Wilaya hiyo kuongeza thamani ya mazao ya nyuki ili kuwa bidhaa bora ambazo zitakuwa na tija katika kukuza uchumi wao.

Wito huo aliutoa hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya siku ya nyuki yaliyofanyika Wilayani humo na kuhusisha vikundi mbalimbali vya wafugaji nyuki.

“hii siyo kwenye asli tu ni bali hata bidhaa nyingine zinazopatikana kwenye asali uwe na uwezo wa kuziongezea thamani ili bora kiushindani katika biashara”, alisema Mwanga.

Alisema ni muhimu kujitangaza kupata ili kuapata wateja huku serikali ikitafuta namna ya kuwasogezea fursa zinazopatikana kwenye ufugaji wa nyuki.

Kadhalika Katibu Tawala huyo alisema ni vema kubadilisha mfumo wa maadhimisho kama hayo Ili yaweze kuwa na tija kwa washiiriki kwa kuwa kikao kazi na kutengeneza maazimio ya namna ya kuinua ufugaji.

Aidha, alishauri wataalamu kuyatumia maadhimisho kama hayo kwa nyakazi zijazo kama fursa ya kutoa ujuzi kwa wafugaji nyuki ili waboreshe shughuli hizo kwa faida zaidi.

Mkuu wa Kitengo cha Uhifadhi na Utunzaji Misitu Wilaya ya Mkuranga, Asted William alisema kwa kipindi cha miaka mitano wamefanikiwa kuwa na mizinga ya kisasa 1,015 na mizinga ya kienyeji 72 yote ikizalisha ikizalisha zaidi ya tani 3000 ya asali.

“Tunaishukuru serikali kwa namna iliweka kipaumbele suala la ufugaji nyuki kwa kuhakikisha inatengenezwa mazingira wezeshi ya soko la asali kuuuzwa katika masoko ya nje ya nchi ikiwemo China na nchi nyingine duniani,” alisema William

Sanjali na hayo alisema Tanzania imepewa heshima ya kuandaa mkutano mkubwa unaowakutanisha wadau wa ufugaji nyuki duniani.

Kwa mujibu wa Asted kwa sasa wanakabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi, yanayotokana na uchomaji wa moto mazinga na mbinu za uvunaji zisizo za kitaalamu.

Posted in

Leave a comment