Na Annamaria John

Imeelezwa kuwa mafunzo elekezi ni muhimu kwa wafanyakazi wapya ili kuwajengea uwezo kutambua misingi ya kazi, sheria, kanuni, taratibu na maadili ya utumishi wa umma.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu Bi. Christina Akyoo jijini Ddodoma wakati akiongea kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Maji na kusisitiza kuwa mafunzo hayo ya awali ni utekekezaji wa matakwa ya sheria kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu katika Utumishi wa Umma.

“Kanuni hizo zitawawezesha waajiriwa wapya kutambua misingi ya utoaji wa huduma bora kwa wateja elimu kuhusu rushwa na madhara yake mahala pakazi na utunzaji wa siri”, alisema Bi. Akyoo.

Alisema mafunzo yanasisitiza kufanya kazi kwa upendo, ushirikiano na umoja kipindi chote cha utumishi wa umma ikiwemo kufikia azma ya serikali ya kutoa huduma ya maji kwa wananchi kwa asilimia 95 mIjini na 85 vijijini.

Kada zilizoshiriki mafunzo hayo ya siku tatu ni pamoja na waendesha ofisi, wahandisi, madereva, na wataalamu wa ubora wa maji ikijumuisha watumishi 60 na yaliratibiwa na Wizara ya Maji kwa kushirikiana na Chuo cha Utumishi wa Umma.

Posted in

Leave a comment