Na Thomas Okello
Fuatilia habari picha za matukio mbalimbali ya Maonesho ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi yaliyofanyika Mkoani Singida Aprili 28, 2025.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi katika viwanja vya Mandewa Mkoani Singida _ Aprili 28, 2025.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Zuhura Yunus (kulia) akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga alipotembelea banda la Mamlaka katika Maonesho ya Kitaifa ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayoendelea katika vīwanja vya Mandewa Mkoani Singida kuanzia Aprili 24 hadi Aprili 30, 2025.

Baadhi ya wageni walioshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi katika hafla ya Maadhimisho hayo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mandewa Mkoani Singida Aprili 28, 2025.


Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga (kati kati picha ya juu) na Saile Kurata (picha ya chini kushoto) wakitoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya Vinasaba vya Binadamu.

Wachezaji wa timu уа Afya wakifanya mazoezi mepesi kabla уа kuanza mchezo na timu ya Wizara ya Mambo ya Nje katika hatua ya robo fainali katika viwanja vya Aintel mkoani Singida Aprili 26, 2025. Kulia ni mtumishi wa Mamlaka Jackson Mwijage. Mambo ya Nje ilishinda kwa mikwaju ya penati.
Leave a comment