Na Vincent Mpepo

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dkt. Mwatumai Mwanjota amewataka wanaume kutokwepa wajibu kwa familia zao katika masuala mbalimbali ya kiimani ikiwemo kuhudhuria na waume zao kwenye huduma na sakramenti muhimu.

Hayo ameyasema leo baada ya ubatizo wa watoto katika Mtaa wa Kwembe na kwamba anakerwa na baadhi ya wanaume kuwaacha wake zao kwenda ibadani kwa ajili ya ubatizo wa watoto wao huku akihoji umuhimu wa shughuli walizoenda kufanya ambazo ni zaidi ya tukio kama ubatizo.

“Ubatizo ni kitu chenye thamani sana na alihoji kwa nini wapange safari siku ya ubatizo?”, alihoji Mchungaji Dkt. Mwanjota.

Alisema ikiwa kuna matatizo ya kuumwa mpaka kulazwa walao hapo wataeleweka vinginevyo wanakwepa wajibu wao kama wazazi na viongozi wa familia.

Aidha aliwataka akina mama hao wakaombe msamaha na kutengeneza na waume zao ikiwa kuna hitilafu ili mambo yawe mazuri kwa wakati ujao.

Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava akihubiri kwa kutumia maandiko kutoka kitabu Zaburi alisema ni kitabu chenye hazina kubwa ndani yake kwa kuwa unaweza kutunga nyimbo ukaimba, ukasifu na kushangilia ukuu wa Mungu.

Alisema kila kiumbe hakina budi kumsifu Mungu kwa kuwa ndiye aliyekipa uhai na uwepo wake hapa duniani.

“Kila kiumbe kina namna ya kumshukuru Mungu kwa ajili ya uumbaji wake ndio maana vitu kama Jua na Mwezi vinamsifu Mungu”, alisema Mwinjilisti Mzava.

Alisema mwadamu anapaswa kuimba wimbo mpya kila siku kwa kuwa ndiye aliyempa uhai na kwamba kuimba ni sehemu ya kushukuru na moyo unaoweza kushukuru ni ule uliojaa shukrani.

“Kama unaweza kumsifu mwanadamu ikiwa amekufanyia jambo fulani jema, je Mungu si zaidi ya mwanadamu?”, alisema Mwinjilisti Mzava.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Ujenzi Mtaani hapo, Exaud Mchome akitoa mwendelezo wa kazi ya ujenzi wa kanisa alisema kazi ya uwekaji bati inaendelea licha ya kusimama kutokana na hali ya hewa.

Aliwakumbusha washarika kuendelea kumtolea Mungu ili kufikia malengo kwa awamu ya kwanza ya January hadi Juni kwa kiasi walichokubaliana.

“Roho ya kupenda ikusukume ufanye jambo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Bwana”, alisema Mchome.

Ibada ya leo siku ya nne baada ya Pasaka kiliturujua ni maalumu kwa ajili ya uimbaji ikitambulika kwa jina na la ‘Domino Kantate’ na mtaani Kwembe ilipamwa na kwaya mbalimbali za mtaani hapo lakini pia uwepo wa Kwaya Kuu ya Umoja kutoka Mtaa wa Malamba Mawili ulinogesha na kufanya iwe siku ya Baraka tele.

Kwaya Kuu ya Umoja kutoka Mtaa wa Malamba Mawili ikihudumu katika ibada ya Leo, Siku ya nne baada Pasaka katika Mtaa wa Kwembe.

Sanjali na hilo huduma mbalimbali za kichungaji ikiwemo ubatizo, meza ya bwana na kuweka wakfu kwa vifaa vilivyoletwa kanisani kwa ajili ya kazi ya Mungu zilifanyika.

Posted in

Leave a comment