Na Mack Francis-Arusha ‎ ‎

Mwanamuziki maarufu wa Bongo Fleva na mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulazizi Abubakari Chende almaarufu Dogo Janja, ameibuka mshindi wa kura za maoni na kutangazwa rasmi kuwa mgombea udiwani wa CCM katika Kata ya Ngarenaro, jijini Arusha. ‎ ‎

Katika uchaguzi huo wa ndani wa chama uliofanyika hivi karibuni, Dogo Janja amepata ushindi wa kishindo kwa kura 76, akimshinda aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo, Isaya Doita, ambaye alipata kura 60, huku Benjamin Mboyo akipata kura 2 pekee. ‎ ‎

Kura hizo zilihesabiwa mbele ya wasimamizi wa uchaguzi wa CCM, Sophia Islam na Rajab Mwaliko, waliothibitisha kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki. ‎ ‎Ushindi huo unamuweka Dogo Janja kwenye nafasi ya kugombea rasmi nafasi ya Udiwani wa Kata ya Ngarenaro katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Posted in

Leave a comment