Na Mack Francis – Arusha ‎ ‎

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amezitaka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kuweka mikakati ya pamoja ya kupambana na rushwa.

Majaliwa alitoa wito huo hivi karibuni 2025 Jijini Arusha wakati akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika ufunguzi wa warsha ya kikanda kwa viongozi wa taasisi za kupambana na rushwa kwa nchi za SADC iliyofanyika Jiji humo kwa siku Mbili. ‎

‎Katika hotuba yake, Waziri Mkuu alisema mapambano dhidi ya rushwa hayawezi kufanikiwa bila ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wakiwemo sekta binafsi, taasisi za dini na vyombo vya habari, akisisitiza kuwa ushirikiano huo ni muhimu kwa kudhibiti mizizi ya rushwa.

Posted in

Leave a comment