Na Vincent Mpepo

Wadahiliwa wa Shahada za Uzamili na Uzamivu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Mkoa wa Dar es salaam wameelezea mipango na mikakati yao binafsi ili kuhakikisha wanamaliza masomo yao kwa wakati na kwa mafanikio.

Wakizungumza na mwandishi wetu katika mahojiano, wadahiliwa hao  walionesha kufurahia mafunzo elekekezi yaliyotolewa na chuo hicho kwani yamewafungua kuona namna ya usomaji chuoni hapo.

Mwanaidi Salim, mdahiliwa wa Shahada ya Uzamili katika Eilimu, Sera na Mipango alisema mafunzo elekezi aliyoyapata yamemsaidia kutambua mifumo ya kujifuza na kujifunzia huku akidai kuwa vitu vingi vimerahishishwa.

“Kila kitu kipo mtandaoni kuanzia masomo na sehemu ya kuhifadhi taarifa za malipo”, alisema Mwanaidi.

Alisema wameelekezwa kuwatambua waratibu wa programu ambao ndio waongoza njia katika safari yao ya masomo kwa kuwa wana taarifa muhimu katika programu wasomazo.

Kwa upande wake, Beatus Kamugisha mdahiliwa wa Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Maktaba na Habari alisema amejipanga vyema kuanza masomo na kwamba mafunzo elekekezi yamemsaidia kujua namna ya kusoma hususani kwa mfumo wa elimu huria na masafa ambao nyezo yake kuu ni mtandao.

“Tumefundishwa mifumo ya kusomea, matumizi ya programu tumizi kama vile Zoom na namna ya kutoa mrejesho kwa walimu kwa kazi za darasani”, alisema Kamugisha.

Mdahiliwa wa Shahada ya Uzamivu katika masuala ya kibenki na mifumo ya malipo katika Kitivo cha Usiamizi wa Biashara, William Fidelis alisema mafunzo elekezi n muhimu lakini kuna sehemu ya wajibu kati ya mwanafunzi na msimamizi wa utafiti.

“Mafunzo elekezi yametoa matumaini na mwanga kwa wadahiliwa hususani sisi ambao ni watu wazima kwa kuwa tumepata miongozo itakayotusaidia kuenenda katika safari ya masomo”, alisema William.

Alisema elimu ya utu uzima ina changamoto hususani elimu  huria na masafa ambayo mwanafunzi anasoma kwa namna ya kutokakaa darasani ambapo atatakiwa kuwa makini zaidi ili aendane na matakwa ya asomeacho kwa miongozo iliyopo.

“Uthabiti na usaidizi wa msimamizi kwa mwanafunzi ndio kitu muhimu ili kuhakikisha kuwa hakuna anayemfelisha mwingine”, alisema William.

Mratibu wa Idara Usimamizi na Kumbukumbu wa Kurugenzi ya Masomo ya juu chuoni hapo, Mhadhiri Mary Ogondiek alielezea wajibu wa mwanafunzi na msimamizi katika mchakato wa utafiti huku akiwataka wanafunzi kujenga utaratibu wa mawasiliano ya mara kwa mara na wasimamizi wao.

Posted in

Leave a comment