
Na Mack Francis-Arusha
Mkuu wa mkoa Arusha Kenani Kihongosi mapema wiki hii aliwaongoza wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Arusha kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Arusha, kumdhamini Mgombea Urais wa Chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wananchi walioambatana na Kihongosi ni kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo wajasiriamali, mama lishe na baba lishe, vijana wanaojishughulisha na usafiri wa bajaji na pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na wananchi wengine,
Sababu za kumuunga mkono zinatajwa kuwa ni kutokana na mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa Mkoani Arusha kwa kipindi cha Miaka minne ya uongozi wake.


Leave a comment