Na Sylvester Richard

Afisa Polisi Jamii Mkoa wa Singida, ACP Richard Mwaisemba amewataka wananchi wa Kata ya Makanda, Wilaya ya Manyoni, kuitii sheria na kanuni za uchaguzi mkuu 2025 bila kushurutishwa ili kulinda amani na usalama katika maeneo yao.

Akihitimisha mafunzo ya Polisi Jamii kwa vijana 32 wa kijiji cha Magasai, ACP Mwaisemba amesisitiza umuhimu wa uadilifu, nidhamu na kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuzuia uhalifu.

Viongozi wa jamii wamepongeza mafunzo hayo na kuomba yaendelezwe kwa kuwahusisha vijana zaidi.

Posted in

Leave a comment