

Na Mack Francis-Arusha
Wananchi wa Mkoa wa Arusha jana Jumamosi Agosti 23, 2025 wamejumuika pamoja kushiriki kwenye Mbio za pamoja na mazoezi ya viungo, ikiwa ni siku ya Kilele cha Tukio la Tanzania Samia Connect, linalofanyika Mkoani Arusha kuelezea mafanikio yaliyopatikana Mkoani Arusha katika Kipindi cha Miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mbio hizo ziliratibiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Kenani Kihongosi na ziliambatana na huduma mbalimbali kwa wananchi ikiwemo matibabu bure na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya Taifa.

Kwa mujibu wa taarifa ya aliyekuwa Katibu wa Itikadi, uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa CPA Amos Makalla Kihongosi ndiye atamrithi kwa nafasi hiyo.

Leave a comment