Na Vincent Mpepo

Walimu wanaosoma somo la Kifaransa kama mmoja ya somo la kufundishia wametakiwa kuwekeza nguvu nyingi na kujibidiisha kwani kuna fursa nyingi za ajira za ndani na nje ya nchi kupitia lugha hiyo.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki katika mijadala mbalimbali ya Siku ya Walimu wa Kifansa Duniani iliyofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Azania ambapo fursa za Lugha hiyo zilibabinishwa.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu wa Kifaransa Tanzania (TAFT), Dkt. Costantine Njalambaya alisema Kifaransa si tu lugha ya kujifunza, bali ni fursa ya ubunifu na chombo cha mshikamano kinachotumika kujieleza kupitia utamaduni na daraja linalounganisha watu.

Dkt. Njalambaya aliushukuru Ubalozi wa Ufaransa kwa msaada wa kifedha, ambao umewezesha sherehe hizo kufanyika na kwamba unasaidia kimarisha dhamira chama hicho kukuza ufundishaji wa lugha ya Kifaransa nchini Tanzania na kuendeleza jamii kielimu.

Aidha alizungumzia mipango na mikakati ambayo chama chake kimeiweka ili kuwafikia walimu wengi wa Kifaransa nchini mijini na vijijini ili kuongeza wigo wa walimu wa Kifansa nchini.

Mwalimu wa Kifaransa, Frola Musikula ambaye kwa sasa amestaafu, alisema kuna fursa nyingi kwa vijana ambao wanasoma Kifaransa na kutanabaisha kuwa kwa uzoefu wake amegundua wanafunzi wanaomliza Shule ya Msingi wengi wao wanapenda sana Kifaransa.

“Watoto wangu wawili wanafundisha Kifaransa na pia Kifaransa kimeniwezesha kugfanya kazi kwenye maeneo mengi ikiwemo sekta ya utalii na ualimu huko Zanzibar”, alisema Mwalimu Flora.

Alisema pamoja na kwamba amestaafu bado anafundisha Kifaransa kwa wanafunzi waliomaliza darasa la saba ambao wanajiandaa kuingia kidato cha kwanza katika kituo cha ‘Pugu Intercity Academy’.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, Afisa Elimu Kata, Upanga Magharibi ambaye alimwakilisha Afisa Elimu Jiji la Dar es Salaam, Mwalimu Immaculata Ngure alisema wakati umefika kwa serikali kubadilika na kuongeza idadi ya walimu wa somo la kifaransa kutokana na umuhimu na faida za somo hilo katika nchi na kwa mtu mmojammoja.

“Uhamasishaji ufanyike ili kuhakikisha watoto wetu wanasoma lugha ya kifaransa”, alisema Mwalimu Immaculata.

Akizungumzia matumizi ya nyimbo katika ufundishaji alisema ni zana muhimu katika kusaidia kukuza uelewa na kuweka kumbukumbu hatahivyo alishauri uchaguzi wa nyimbo hizo ufanyike kwa makini ili kuwa na maudhui yanayofaa kwa kuwa siyo nyimbo zote zinaweza kutumika.

Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Azania, Mwalimu Magreth Lawrance alisema shule hiyo ina darasa maalumu la Kifaransa na ameshukuru kusikia kuwa uongozi wa chama hicho unakusudia kufanya maboresho katika darasa hilo jambo ambalo ni jema.

“Sisi kama watanzania tumewasikia wenzetu kutoka Zanziobar na kilichotuunganisha ni Lugha ya Kifaransa kama ambvyo Mwalimu Nyerere alivyofanikiwa kuwaunganisha watanzania kwa kutumia Lugha”, alisema Mwalimu Magreth.

Aidha alishauri walimu wa shule nyingine kuanzisha somo hilo la Kifaransa kwa kuwa watoto wanapenda n ani fursa nzuri kwao.

Maadhimisho ya mwaka huu yenye kaulimbiu “Kuimba, Kucheza, Kufundisha: Lugha ya Kifaransa katika Muziki,” yanaangazia sanaa na michezo inavyotumika kwenye kufundisha lugha ya Kifaransa yamewakutanisha walimu, wahadhiri, wanafunzi wa lugha ya Kifaransa nchini yakihusisha bara na visiwani huku ikibanika kuwa Lugha hiyo ina ladha ya kipekee kwenye muziki hivyo ni rahisi kufundishika.

Posted in

Leave a comment