• Mwalimu Bupe Mwabenga akifundisha  wakati ibada ya Jumapili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mtaa wa Kwembe jijijini Dar es salaam

    Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Wanandoa wamekumbushwa kuishi kwa kadiri ya mpango wa maagizo ya Mungu ili kuepuka migogoro inayotokana na mwingiliano wa majukumu kati yao.

    Wito huo umetolewa Jumapili  na Mwalimu Bupe Mwabenga wakati akifundisha katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe na kubainisha kuwa sababu mojawapo ya migogoro katika ndoa ni kwa baadhi ya wanandoa kutoishi kwa utaratibu uliowekwa na Mungu.

    Alisema si vibaya kwa wanandoa kuamua kusaidiana majukumu lakini kusaidiana huko kuwe katika utaratibu ambao unatambua haki na wajibu wa kila mwanandoa ili kupata tafsiri sahihi ya anayesaidia na anayesaidiwa.

    “Wanawake wamejengewa uwezo, wamewezeshwa na wanatambua haki zao hatahivyo bado haiwapi nafasi ya kuwa wanaume”, alisema Mwalimu Mwabenga.

    Aliikumbusha jamii kuwa makini na mafundisho ya mitandaoni kuhusu masuala ya ndoa kwani siyo kila maudhui yanalenga ustawi wa ndoa badala yake ni upotoshaji ambao matokeo yake ni kuwa na ndoa zenye migogoro ambayo inazorotesha ustawi wa taasisi muhimu ya ndoa.

    Akizungumzia malezi ya watoto ambao kila familia inajaaliwa alisema huwa wanakuja na changamoto hivyo aliwataka wazazi na walezi kutokawakatia tamaa watoto wao kwa kuwa watoto hao wamebeba kusudi la Mungu.

    “Malezi ya watoto huwa yanaambatana na changamoto mbalimbali katika hatua za malezi tangu utoto hadi utu uzima”, alisema Mwalimu Mwabenga.

    Mwinjilisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava aliwajulisha washarika kuhusu ujio wa vijana zaidi ya mia mbili (200) ambao walikuja siku hiyo kwa ajili ya mkutano kwa ajili ya mipango yao ya shughuli za vijana.

    “Niliipokea taarifa ya mkutano huo kwa kwa shukrani japo nlijiuliza ikiwa Kwembe imeonwa kuwa yaweza kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa kama huo”, alisema Mwinjilisti Mzava.

    Mwenyekiti wa Kwaya Kuu ya Mtaa huo, Jonas Mnkeni aliwajulisha washarika wa mtaa huo kuhusu uzinduzi wa albamu ya kwanza ya picha mjongeo (video) ambao unatarajiwa kufanyika Jumapili ya Tarehe 23 Februari 2024.

    “Ninaomba washarika mtuunge mkono ili kuendeleza kuitangaza injili kupitia albamu hii ya kwanza ya toleo la video”,alisema Mnkeni.  

    Sehemu ya jengo la Kanisa Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe ambalo linaendelea kujengwa, (Picha zote na Michael Mwambage).

  • Na Vincent Mpepo, Kwembe

    Vijana wa kike na kiume nchini wametakiwa kujishughulisha na kuzalisha kipato kitakachowasidia hata kama hawakupata ajira kwenye mifumo rasmi iwe serikalini au sekta binafsi.

    Wito huo umetolewa na Mwalimu Bupe Mwabenga wakati akihubiri katika ibada siku ya Jumapili katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mtaa wa Kwembe na kusisitiza kuwa bado wana wajibu kama wanajamii kujibiidisha ili kufikia maono ya ndoto zao.

    Alisema kufanya kazi na kuzalisha baada ya kuhitimu masomo kutawasaidia kuepuka utegemezi kwa wazazi na walezi ambao wamejitoa kuwafikisha hatua hiyo.

    Alisema vijana wanatakiwa kujisimamia katika maisha na kuwakumbusha kujenga mahusiano mema na Mungu na wanajamii wanaowazunguka.

    Aidha,aliwapongeza washarika wa Mtaa huo kwa ujenzi wa nyumba ya Mungu huku akitanabaisha kuwa ujenzi siyo rahisi na kuwatia moyo kwa kuwa wanafanya jambo jema machoni pa Mungu.

    “Kujenga siyo rahisi iwe kwenye ngazi ya familia au taasisi”, alisema Mwalimu Mwabenga.

    Mwinjiisti Kiongozi wa Mtaa huo, Emeline Mzava alimshukuru Mwalimu Mwabenga mafundisho mazuri kwa kuwa kilichofundishwa kimegusa maeneo mengi na kwa washarika wa rika zote kiasi kwamba kila aliyehudhuria amepata kwa sehemu yake.

    Aidha, aliwakumbusha washarika kuhusu harambee ya kuchangia kituo cha Udiakonia cha watoto wenye mahitaji maalumu ambacho kitahamishwa kutoka Kijichi Kwenda Kitopeni-Bagamoyo kutokana na changamoto za kimazingira mahali kiliposasa.

    “Tuhusike kwenye harambee hii kama sehemu ya kumshukuru Mungu kwa kutujalia Watoto”, alisema Mwinjisti Mzava.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Mtaa huo, Exaud Mchome aliwashukuru washarika kwa kuendelea kuchangia ujenzi wa kanisa huku akiwataka kutokata tamaa na kazi hiyo.

    Alisema kazi inayofuata ni kutengeza mifumo ya uwekaji paa ambapo kuna uhitaji wa matofali ya kawaida 5,000,  ya ruva 1500 na mifuko ya saruji ipatayo 1,500.

  • Na Tabia Ally, DSM

    Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) itashirikiana na Jeshi la Polisi Tanzania katika utekelezaji wa mikakati ya kuimarisha usalama barabarani ili kupunguza ajali.

    Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda SACP William Mkonda katika Ofisi za Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) zilizopo Mtendeni, Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki hii.

    Kamanda SACP William Mkonda alisema lengo la ziara hiyo kujadili na kuweka mikakati ya ushirikiano kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) na Jeshi la Polisi Tanzania ikiwa ni maandalizi ya Kikao Kazi cha Makamanda wa Polisi wa Usalama Barabarani wa Mikoa na Wilaya kinachotarajiwa kufanyika jijini Dodoma Februari 2025.

    “Kikao hicho kinalenga kuweka mikakati madhubuti ya kupunguza ajali za barabarani na madhara yake kwa watumiaji wa barabara”, alisema Kamanda SACP Mkonda.

    Alisema kuna umuhimu wa elimu ya bima kwa makamanda wa polisi wa usalama barabarani wa wilaya na mikoa hususani katika uhakiki wa bima kupitia mifumo rasmi.

    Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware alisema hatua ya kuunganisha mifumo ya TIRA na Polisi itasaidia upatikanaji wa taarifa za ajali mara zinapotokea.

    “Hatua hii inalenga kuhakikisha waathirika wa ajali wanapata fidia zao kwa haraka, kwani taarifa za ajali zitasomwa moja kwa moja na kampuni za bima kupitia mfumo wa TIRA”, alisema Kamishna Dkt.  Saqware.

    Mkutano makamanda wa Polisi wa Usalama Barabarani wa mikoa na wilaya utafanyika jijini Dodoma wiki ya tatu ya Mwezi Februari 2025 huku Mkuu wa Mkoa huo, Bi. Rose Senyamule anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi.

  • Na Martha Joachim,Tanga

    Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi, Mawasiliano, Ardhi na Nishati Zanzibar, imelipongeza Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kwa utendaji kazi madhubuti katika usimamizi wa sheria na kanuni za usalama, ulinzi na utunzaji mazingira  wa usafiri majini.

    Pongezi hizo zimetolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Yahya Rashid Abdulla, walipotembelea Ofisi za TASAC mkoani Tanga na kufanya kikao na watumishi wa TASAC pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA).

    “Tumefurahishwa na utendaji kazi mzuri wa TASAC katika udhibiti na usimamizi wa safari kwa njia ya maji hasa katika Bandari ya Tanga”, alisema Mhe. Abdulla

    Alisema usimamizi mzuri umesaidia kurahisisha usafiri kati ya Tanzania Bara na Visiwani kwa eneo la mwambao ambalo lilikua na changamoto kubwa ya usafiri kwa njia ya maji.

    Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu TASAC, Meneja Mafunzo na Utoaji vyeti Mhandisi Lameck Sondo ameishukuru Kamati hiyo na kuahidi kuendeleza weledi, ufanisi na ushirikiano na taasisi nyingine katika kudhibiti na kusimamia shughuli za usafiri majini kwa maslahi mapana ya Taifa.

    Mhandisi Sondo alisema Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeendelea na utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa usalama wa usafiri katika Ziwa Victoria  ambao ni mradi unaoshirikisha nchi za Uganda na Tanzania katika kanda ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

    Aidha, ameeleza kuwa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) imefanikiwa katika ukaguzi wa meli za kigeni pamoja na kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi ili kuwajengea uwezo katika kutekeleza majukumu hayo kwa weledi.

    Kamati ya Kudumu ya Baraza la Wawakilishi, Mawasiliano, Ardhi na Nishati Zanzibar ilifanya ziara hiyo mwanzoni mwa wiki hii ili kujifunza utendaji kazi na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) na TPA mkoani Tanga ikiwemo Bandari za Tanga, Pangani na Kipumbwi.

  • Na Ruth Kyelula, Mbulu

    Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Joseph Mandoo amewataka madiwani na  wakuu wa idara kushirikiana ili kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shule kabla ya muda uliopangwa kuisha.

    Mandoo aliyasema hayo wakati akifungua baraza la madiwani katika robo ya pili ya Octoba-Desemba 2024/2025 iliyofanyika hivi karibuni kwenye ukumbi wa halmashauri ya Wilaya hiyo huku akitanabaisha kuwa serikali hutumia fedha nyingi katika kuboresha miundombunu ya shule huku idadi ya wanaosoma ni chache.

    “Wanafunzi wote waliofaulu Kwenda kidato cha kwanza wahimizwe Kwenda shule”, alisema Mandoo

     Aliwataka maafisa elimu na watendaji wa kata na vijiji kushirikiana ili kufanikisha jambo hilo.

    Aidha, aliwakumbusha watumishi hao kujitathimini na kujua sababu zinazochangia shule za msingi za umma kutofanya vizuri katika mitihani ya taifa hivyo kuja na mikakati madhubuti ili kunusuru hali hiyo.

    Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Abubakar Kuuli alisema uandikishaji wa wanafunzi wa elimu msingi na wanafunzi wa sekondari wanaoripoti bado hauridhishi licha ya kuwashirikisha watendaji wa kata kwenye zoezi hilo.

    “Hadi sasa ni asilimia 51 ya wanafunzi wa elimu msingi ndio wameandikishwa huku asimilia 52 ndio wameripoti shule kwa upande wa sekondari.

    Akitoa ripoti ya ufaulu kwa matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2024 alisema ufaulu umefika asilimia 98.7 ambapo umeongezeka kwa asilimia 3.7 kutoka matokeo ya mwaka 2023.

    Kwa upande wake, Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Massay aliwapongeza madiwani na wakuu wa idara wote kwa kazi kubwa kufuatia ufaulu huo.

    Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbulu, Paulo Bura aliutaka uongozi wa  Halmashauri kuhakikisha wanafunzi wanaripoti mapema katika Shule ya Sekondari ya Eshkesh huku pia akitoa makataa ya kuripoti kuwa March 31, 2025.

    Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mbulu, Melkiadi Nar aliwashukuru viongozi kwa kazi kubwa  wanayofanya huku pia akitoa rai ya kuongezwa kwa shule za sekondari za kidato cha tano (5) na cha sita(6).

  • Na Cartace Ngajiro, Tanga

    Serikali imepongezwa kwa kuendelea kuboresha bandari nchini na kuziwezesha kukusanya baadhi ya mapato “Wharfage” jambo ambalo limeongeza ufanisi  katika utendaji.

    Pongezi hizo zilitolewa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uchukuzi Ludovick Nduhiye hivi karibuni wakati ziara yake katika bandari ya Tanga kujiuonea utendaji kazi wa bandari hiyo.

    Akipokea taarifa ya mradi wa maboresho yaliyofanyika katika bandari hiyo Nduhiye alisifu  mfumo mzima wa utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ambao umesaidia ongezeko la makusanyo ya mapato bandarini hapo.

    “Kukua kwa mzigo toka shehena tani 750,000 hadi tani 3,000,000 kwa mwaka inaonyesha kwa kiasi gani maboresho hayo yamezaa matunda matunda”. Alisema Nduhiye

    Kwa upande wake, Meneja wa Bandari ya Tanga, Masoud Mrisha alisema kukamilika kwa mradi huo kumeleta ufanisi, tija na faida  ikiwemo uharaka katika kuhudumia Meli ongenzeko la idadi ya meli, na kupungua kwa gharama za uendeshaji.

  • Na Vincent Mpepo, OUT

    Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kimeeleezea nia yake ya kuendelea kuenzi uhusiano mwema na vyuo vikuu inavyoshirikiana navyo kutoka Norway kutokana faida ya mahusiano hayo katika ustawi wa watoto wenye mahitaji maalumu kitu kinachoongeza thamani na faraja katika maisha yao.

    Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii ya chuo hicho, Dkt. Dunlop Ochieng wakati wa kuwakaribisha wahadhiri na wanafunzi kutoka Norway iliyofanyika Kinondoni, jijini Dar es salaam leo ambao watakuwa nchini kwa mafunzo ya vitendo kwa muda wa miezi mitatu.

    Alisema chuo chake kinathamini uhusiano huo na kwamba kitaendelea kutoa ushirikiano kwa wahadhiri na wanafunzi hao ili kuhakikisha uwepo wao hapa nchini unaendelea kuwa na tija lakini zaidi kutimiza malengo ya uanzishwaji wa ushirikiano huo ambao una maslahi kwa watoto wenye mahitaji maalumu.

    “Nitumie fursa hii kueleza kuwa kama wadau wa mradi huu, tupo makini na tutafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kuwa malengo ya mradi huu yanatimia”, alisema Dkt.Ochieng.

    Aidha alieleza kuwa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni taasisi ya umma ambayo inatoa huduma ya elimu kwa njia ya huria na masafa na kwamba inawafikia watu walipo kutokana na uwepo wa vituo vya mikoa nchi nzima.

    Mkuu wa Idara ya Sosholojia na Ustawi wa Jamii ya chuo hicho, Dkt.Mariana Makuu alisema mradi huo umeanza kutekelezwa kwa awamu ya pili ambapo awamu ya kwanza ilianza mwaka 2022 hadi mwaka 2024 na kwamba baada ya utekelezaji wenye mafanikio wadau wa pande zote wamekubaliana kuongeza muda wa utekelezaji wake kwa wamu ya pili ambao ni kuanzia mwaka 2025 hadi 2027.

    “Awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huo uliihusisha Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko pekee lakini kwa awamu hii mradi huo huo utaihusiha Shule ya Sinza Maalumu na kufanya idadi ya shule nufaika kuwa mbili”, alisema Dkt.Makuu

    Alisema kundi la kwanza la watekelezaji wa mradi awamu ya pili linahusisha wahadhiri na wanafunzi 10 kutoka Norway ambao watafanya kazi na walimu wa shule tajwa kusaidia watoto wenye ulemavu kwa muda wa miezi mitatu.   

    Mhadhiri Msaidizi kutoka Idara ya Sosolojia na Ustawi wa Jamii, Alexander Ndibalema alielezea masuala ya haki, sheria na sera kuhusu watu wenye ulemavu nchini na kwamba kumekuwa na mitizamo tofauti kuhusu hali ya ulemavu ambayo inatafsiriwa kwa milengo ya hasi na chanya.

    “Mtizamo hasi ni ule unaomuona mtu mwenye ulemavu kama tegemezi, asiye na msaada na ikihusishwa na laana au mikosi”, alisema Ndibalema.

    Kwa upande wake Profesa Mshiriki Karen Reimers ambaye ni msimamizi wa wanafunzi kutoka Norway alisema katika nchi yake kuna sera na sheria madhubuti zinazotekelezwa ili kuhakikisha ustawi wa mtoto hususani mwenye mahitaji maalumu anapata usaidizi wa karibu katika ngazi mbalimbali kutoka kwenye familia hadi shuleni. “Masuala ya watoto yamewekwa kisheria ili kumhakikishia mtoto apate huduma zote muhimu ikiwemo elimu bora na kwenye mazingira rafiki”, alisema Profesa Reimers

  • By Vincent Mpepo, OUT

    The Open University of Tanzania (OUT) has expressed its commitment to maintaining strong relationships with partner universities in Norway due to the positive impact of such collaborations on the welfare of children with special needs something which is significantly improving their lives.

    The statement was made today in Kinondoni, Dar es Salaam by the Dean of the Faculty of Arts and Social Sciences of the Open University of Tanzania, Dr. Dunlop Ochieng, during a welcoming ceremony to lecturers and students from Norway who will be in Tanzania for three months of internship.

    Dr. Ochieng said due to the value of the partnership, his university will continue supporting the Norwegian team to achieve the goals of the collaboration which primarily benefit children with special needs.

    “I take this opportunity to affirm that, as stakeholders in this project, we are committed to doing everything possible to realize its objectives,” he said.

    The Head of Department of Sociology and Social Work, Dr. Mariana Makuu said the project has entered its second phase, with the first phase running from 2022 to 2024 due to its success, stakeholders agreed to extend it for the second phase, from 2025 to 2027.

    Dr. Makuu added that the first phase focused solely on Uhuru Mchanganyiko Primary School, but the second phase will include Sinza Maalumu Primary School thus increasing the number of beneficiary schools to two.

    The first team for the second phase includes 10 people who are lecturers and students from Norway who will work alongside teachers at the mentioned schools to support children with disabilities over the next three months.

    Assistant Lecturer from the Sociology and Social work Department, Alexander Ndibalema discussed the rights, laws, and policies concerning people with disabilities in Tanzania noting varying perceptions of disability, often viewed negatively as dependence or associated with curses or misfortune.

    Professor Karen Reimers, a supervisor of the Norwegian students, explained that Norway has strong laws and policies ensuring the welfare of children, especially those with special needs, guaranteeing access to quality education and supportive environments.

    “Children’s rights are legally protected to ensure they receive essential services, including quality education, in a conducive environment,” stated Professor Reimers.

  • Na Grace Mwakalinga, RUKWA

    MKUU wa Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa, Lazaro Komba, ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama  wilayani humo kuhakikisha vinadhibiti mienendo inayolenga kuhatarisha ustawi wa watoto  wakiwemo wenye ualbino katika jamii.

    Komba alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa kujadili masuala ya  kuimarisha ulinzi na usalama wa watoto ili kulinda haki ya msingi ya kuishi.

    “Imani potofu zimesababisha watoto  wenye ulemavu hususani wenye ualbino kufanyiwa ukatili kama vile kuuawa na kunyofolewa baadhi ya viongo  kwenye miili yao”, alisema Komba.

    Kutokana na suala hilo kuripotiwa katika baadhi ya maeneo nchini, Komba alisema tayari wilaya ya Kalambo imeanza kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa  kwa kuweka mikakati kuanzia ngazi ya kitongoji kwa kutumia vyombo vya ulinzi na usalama kuthibiti vitendo hivyo.

    “Ulinzi na usalama kwa watoto wenye mahitaji maalum ni jukumu la kila mmoja wetu, tushiriki kuhakikisha wanalindwa dhidhi ya ubaguzi, unyanyasaji na ukatili wa aina zote ikiwemo mauaji ya watoto wenye ualbino,” alisema Komba.

    Aliongeza kuwa tayari baadhi ya wadau wanaendelea kutekeleza jukumu la ulinzi na usalama wa watoto wenye mahitaji maalum wakiwemo wenye ualbino ambao ni Child Support Tanzania (CST), kukemea na kupinga ukatili na mauaji dhidi ya watu wenye Ualbino yaliyoripotiwa hivi karibuni likidai vitendo hivyo vinajenga hofu na kutishia usalama kwa makundi hayo.

    Mratibu wa shirika la Child Support Tanzania (CST), Nemes Temba alisema wananchi wanapaswa kuachana na imani potofu dhidi ya watu wenye ualbino kwa kuwa kuendeleza imani hizo ni kwenda kinyume na maagizo ya vitabu vitakatifu, katiba ya nchi na mikataba mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ambayo inasisizita haki ya kuishi kwa kila mtu bila kujali hali aliyonayo.

    Alisema jukumu la jamii ni kufungua fursa za kielimu  na kuweka mazingira rafiki kwa watoto wenye mahitaji maalum ili kuwasaidia kutimiza ndoto zao.

    “Tulikuwa na maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika hapa mkoani Rukwa ambayo ilikuwa mahsusi kujadili na kuangalia masuala ya kuyatekeleza ili kuhakikisha ulinzi na usalama kwa watoto wenye mahitaji maalum.

    Alisema miongoni mwa miradi wanayotekeleza ni kuhakikisha watoto wenye ulemavu wanapelekwa shule kuanza masomo, uboreshwaji wa miundombinu ya shule  jumuishi zilizopo mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi pamoja na utoaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kulingana na ulemavu wa kila mmoja.

    “Kauli mbiu ya mtoto wa Afrika  mwaka huu inazungumzia Elimu Jumuishi kwa watoto izingatie  maadili na maarifa na stadi za maisha inahimiza jamii kutoa elimu yenye usawa kwa watoto wote, wenye ulemavu na wasio na ulemavu,” alisema Temba.

  • Na Grace Mwakalinga, Dodoma

    Wadau wa sekta ya Sanaa wamekutana jijini Dodoma kujadili vikwazo wanavyokabiliana navyo wakati wa kutekeleza majukumu yao.

    Kikao hicho kimefanyika leo jijini humo kimewahusisha wadau ikiwemo Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) na Taasisi ya Hakimiliki (COSOTA) ili kupata suluhu ya masuala yanayohusu haki na maslahi  ya wasanii Tanzania.

    Agness Kahamba, msanii wa maigizo nchini amesema wanapitia changamoto nyingi wakati wa kutekeleza majukumu yao na kwamba vinapoandaliwa vikao kama hivyo vinatoa fursa kueleza wanayoyapitia ili kupata suluhu kwa wadau wao.

    “Tunatamani kufanya Sanaa yetu kibishara kwa kuuza bidhaa tunazozizalisha ndani na nje ya nchi  lakini  changamoto ni maslahi duni na kukosa mitaji ya kuandaa kazi bora zenye ushindani. Tunaimani Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kupitia ziara alizozifanya mataifa mbalimbali zinaendelea kutangaza sanaa zetu,” amesema Agness.

    Mkuu wa Idara ya Sheria wa Kituo cha Kutetea Haki za Wasanii Tanzania (TARO), Ally Ramadhan, amesema wameendesha vikao mbalimbali kuhusu wasanii na kupokea mapendekezo yao.

    Amesema baada ya mapendekezo hayo watayachakata na hapo baadae watayapeleka bungeni kwa ajili kufanyiwa maboresho na kutungwa kwa sheria zitakazoendelea kuwalinda wasanii nchini.

    Kwa upande wake wakili wa Baraza la Sanaa la Taifa,    Joseph Ndosi, amesema wao kama    walezi wa sekta ya Sanaa wataendelea kuwashauri wasanii namna bora ya kuzalisha kazi zenye ushindani ili kufikia malengo waliyokusudia.