Wakristo wakatoliki nchini wamekumbushwa kuienzi imani yao na kuepuka kufuata upepo wa mijuiza hivyo kudumu na kutohamahama.
Hayo yamebainishwa wakati mahubiri na tafakari katika ibada ya Jumuiya Ndogondogo ya Mtakatifu Alfonsi iliyofanyika kwa mwanajumuiya Dkt.Issaya Lupogo wa Kihonda na kuhudhuriwa na wanajumuiya hiyo kama ilivyo kawaida ya kanisa hilo.
Katibu wa Jumuiya hiyo, Elisha Emmanuel alisema wakati umefika kwa wakristo kutambua kuwa ukombozi ulioletwa na Yesu Kristo haukuja ili kuondoa shida, dhiki na mahangaiko duniani badala yake ni jukumu la wakristo kutambua uwepo wa changamoto hizo na ziwape ari ya kupambana nazo kwa imani.
“Shida na matatizo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu”, alisema Elisha.
Aidha aliwakumbusha wanajumuiya kuendelea kulitegemeza kanisa kwa zaka, sadaka na michango mingine.
Mwenyekiti Msaidizi wa Jumuiya hiyo, Dkt.Issaya Lupogo alisema wakristo wanatakiwa kuishi maisha yanayompendeza Mungu ili kuandaa maisha ya umilele na ili kufanikisha hilo hawana budi kusoma neno la Mungu na kulielewa ili kulinasibisha kimwili na kiroho.
Alisema hata katika maisha ya kawaida hakuna mafanikio yanayokuja kirahisi bila watu kufanya kazi kwa bidii, maarifa na juhudi.
“Mchakato wowote wa kimaendeleo unahusisha kutumia nguvu, akili na wakati mwingine kutoka jasho”, alisema Dkt.Lupogo.
Jumuiya ya Mtakatifu Alfonsi ni mojawapo ya zilizopo katika Parokia Teule ya Mtakatifu Benedicto Jimbo Katoliki la Morogoro.
Sehemu ya wanajumuiya ya Jumuiya ya Mtakatifu Alfonsi katika Parokia Teule ya Mtakatifu Benedicto Jimbo Katoliki la Morogoro (Picha na Vincent Mpepo).
Kaimu Mkuu wa Dawati la jinsia na watoto Wilaya ya Singida Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Exaud Waya akitoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia kwenye kongamano la watoto waishio katika mazingira magumu katika ukumbi wa Vatican maeneo ya Mwenge, Manispaa ya Singida.
Na Sylvester Richard -Singida
Kaimu Mkuu wa Dawati la jinsia na watoto Wilaya ya Singida Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Exaud Waya amesema kuwa ndoa na mimba za utotoni ni chanzo cha watoto waishio katika mazingira magumu.
Amesema hayo Aprili 17, alipokuwa anatoa elimu juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia kwa jamii kwenye kongamano la kimataifa siku ya watoto wa mitaani lilofanyika kwa ngazi ya Wilaya kwenye ukumbi wa Vatican, uliopo Mtaa wa Mwenge , Manispaa ya Singida.
Alimesema yapo mambo mengine yanayochangia ongezeko la watoto waishio katika mazingira magumu ikiwemo wazazi kushindwa kutoa huduma muhimu kwa watoto wao, watoto kufanyiwa ukatili majumbani kwao, wazazi kugombana, wazazi wa kiume kukataa mimba au watoto, utumiaji wa dawa za kulevya kiholela na magonjwa kama vile VVU/UKIMWI.
Aidha amewasihi wazazi kulea familia zao katika maadili na kuwasisitiza kumcha Mungu kila mmoja kulingana na imani yake jambo ambalo litasaidia kujenga taifa imara lisilokwa na watoto waishio katika mazingira magumu.
Naye Sajenti wa Polisi Abihudi Kasonde kutoka kikosi cha usalama barabarani Singida ambaye pia amehudhuria kongamano hilo, amewaelimisha washiriki juu ya usalama barabarani ikiwemo mbinu za kuepuka ajali wakati wa kutumia barabara .
Pichani ni watoto wakishiriki wa kongamano la watoto waishio katika mazingira magumu katika ukumbi wa Vatican uliopo Mtaa wa Mwenge Manispaa ya Singida.
It is creditable hearing something from the authority as the profession of journalism relies on as the best way to ensure authenticity of information and trust.
Academicians are also entrusted with this feature as they are known to be knowledgeable in certain areas of specialization based on what they majored in their course of study.
Who is an academic then? He or she is a member of an association or institution for the advancement of arts, sciences, or letters.
In other countries an academician is the generic term for anyone employed by a higher education institution to teach and/or research, while “Professor” is reserved for those whose official title is professor and sometimes for only very senior academics who are full Professors.
Due to the reputation and honour they earn from the society based on areas of specialty they can be trusted to say and give information to the society.
For instance, a medical doctor, an engineer or surgeon automatically becomes a reliable source of information to the public in his area of specialty.
Due to this trust that is vested on them they need to uphold best practices in order to ensure they remain a reliable source of information.
According to the Vice Chancellor of the Open University of Tanzania, Professor Elifas Bisanda, some academicians have negative perceptions towards many issues that make their existence even unimportant to the public.
“In some cases educated people are corrupt and have negative attitude towards implementation of many issues”, denotes Professor Bisanda.
In the recent years, the trust to academicians has lost its way due to many reasons one being apolitical.
Some of the respected academicians have been swayed by politics and lost their reputation due to political influence and affiliation.
May be let us, not blame them, because they have followed green pastures.
They are sometimes not trusted due to the fact that what they are saying is politically motivated hence lost its potentiality.
However, the issue of newly revised education and training policy of 2023 has divided academicians into number a cross road.
“We have those who are against and the ones who are for the implementation of the policy”, says Prof. Bisanda.
Professor Makenya Maboko from University of Dar es salaam says the newly revised education and training policy emphasize acquisition of knowledge, skills and attitudes that uphold employability and self-employment.
“Tanzania need to transform its curricula through policy and implement best practices of it through competent based education from lower levels in order to produce competent graduates”, says Professor Maboko
He adds saying that, establishment of competent based programmes cater for the needs of labour market and economical opportunities in the country.
A lecturer from Faculty of Business Management of the Open University of Tanzania, Dr.Chacha Matoka says the implementation of the new revised policy should be delayed as there is no proper preparation of the implementing of the same from infrastructures to human resources.
“For instance provision of tablets to teachers in the country is of no use as many of them are using for chatting and other non beneficial uses for themselves and public at large” says Dr.Chacha.
Others are of the opinion that the medium of instruction in Tanzania is a hindrance towards implementing the newly revised education and training policy of 2023.
This means the language of teaching has something to do with creation of a barrier towards the real implementation of the policy.
With the current policy or regulations, with are using both English and Kiswahili for teaching in different levels of education.
According to Professor Bisanda, language is not the only leading factor as many people could be saying instead the focus should be on others if they real exist as what is needed is compatibility of the skills that teachers impart to the learners.
“The language of teaching is not a problem to children and students instead to teachers and lecturers who teach by using Kiswahili could be a problematic”, says Professor Bisanda.
He however insists that the language of teaching should be compatible with the local environment that moulds a child from his/her childhood endeavor.
Professor Makenya Maboko from University of Dar es salaam says Tanzania need to transform its curricula through policy and implement best practices of it through competent based education from lower levels that will determine the future of learners after completing a certain education level.
He says through the newly revised education and training programmes will have to be redesigned to emphasize acquisition of knowledge, skills and attitudes that uphold employability and self-employment.
“Establishment of programmes shall be more closely aligned with the needs of labour market and economical opportunities in the country”, says Professor Maboko .
“For instance provision of tablets to teachers in the country is of no use as many of them are using for chatting and other non beneficial uses for themselves and public at large” said Dr.Chacha.
The article highlights the important role that academicians play in disseminating information and fostering trust within society. However, it also acknowledges the challenges and criticisms faced by academicians, particularly regarding issues such as corruption, political influence, and the loss of public trust.
Idadi ya watoto wenye ulemavu wanaosoma katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko
iliyopo jijini Dar es Salaam imeongezeka baada ya Chuo Kikuu Huria Tanzania kwa kushirikiana na vyuo vikuu kutoka Norway kuanzisha programu ya kuwawezesha wanawake wenye watoto shuleni hapo kujifunza shughuli za ujasirimali ili kujiingizia kipato.
Hayo yamebainika wakati kukabidhi misaada ya vifaa katika Shule hiyo hivi karibuni iliyohudhuriwa na wahadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambao ni wenyeji na wanafunzi kutoka vyuo vikuu vya Norway, walimu na wanafunzi wa shule hiyo.
Katibu wa kikundi cha Uhuru Mamas, Caroline Nyamala alisema ongezeko la watoto wenye mahitaji maalumu shuleni hapo limetokana na fursa ya akina mama kuwezeshwa kiuchumi kupitia kufanya kazi za mikono ambazo wanaziuza ili kujikwamua kiuchumi.
Alisema kabla ya fursa hiyo walikuwa wanakutana shuleni hapo wakielezana vikwazo na madhila wanayokumbana nayo kifedha na kisaikolojia baada ya kuachwa na wenza wao kwa sababu ya kupata watoto wenye mahitaji maalumu lakini kwa sasa wanamshukuru Mungu kwa kuwa mambo yamebadilika.
“Lakini baada ya kupata ufadhili wa kupata mafunzo ya kutengeneza bidhaa mbalimbali za mikono tumeungana na tunafanya shughuli zetu huku tukiendelea kuwasubiri watoto wamalize vipindi vya darasani,” alisema Caroline.
Alisema kikundi hicho kimekuwa hospitali ya akina mama wenye watoto wa mahitaji maalum na wanaita kitengo kwa sababu kimeponya majeraha yao na kuwaweka sawa kisaikolojia huku pia wakijikwamua kiuchumi.
Mwenyekiti wa Kikundi hicho, Herieth Kabende alisema kwa sasa wamefikia 35 na kwamba wameunganishwa na wadau mbalimbali kwa ajili kupitia bidhaa wanazozitengeneza na kuzuiza ikiwemo vikiwemo vikapu.
Aidha, aliiomba serikali kusaidia matibabu bure kwa watoto wenye ulemavu kwa kuwa kuwa gharama za kuwahudumia ni kubwa ukilinganisha na watoto wa kawaida.
Alisema asilimia kuwa ya wanaowahudumia watoto hao ni wanawake ambao wameachwa na waume zao bila kuwa na chanzo cha uhakika cha mapato hivyo wanapitia wakati mgumu pindi wanapougua.
“Mtoto mwenye ulemavu akiumwa gharama zake ni kubwa sana kwa sababu atahitaji kutibiwa ugonjwa unaomsibu , viungo vyake na mahitaji mengine”, alisema Herieth.
Alisema kwa taratibu za sasa ambazo zinawalazimu kujikusanya hadi kufikia 100 ndipo wakate bima zimekuwa ngumu na kuomba serikali iwasaidie.
Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Chuo Kikuu Huria chaTanzania ambao watekeleza program za kuwasaidia watu wenye ulemavu Dkt. MarianaMakuu alisema lengo lao ni kuhakikisha watoto wenye ulemavu nchini wanapataelimu katika mazingira mazuri sambamba na kuwawezesha akina mama kujikwamuakiuchumi ili kuwalea vyema watoto.
Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Vincent Mpepo akifanya mahojiano na Mwenyekiti wa Kikundi Uhuru Mamas Collection, Herieth Kabende hivi karibuni katika viwanja vya Shule ya Msingi Mchanganyiko iliyopo jijini Dar es salaam wakati wa kukabidhi misaada ya vifaa katika Shule hiyo iliyohudhuriwa na wahadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na wanafunzi kutoka vyuo vikuu vya Norway, walimu na wanafunzi wa shule hiyo.(Picha na Solfrid Raknes kutoka Norway).
Vyuo vikuu viwili kutoka nchini Norway vimetoa msaada wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa watoto wenye mahitaji maalum, Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko iliyopo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati kukabidhi vifaa hivyo, Profesa Bente Dale Malones, alisema vifaa hivyo vitapunguza tatizo la uhaba wa nyenzo za kufundishia, kujifunzia na vifaa vya michezo shuleni hapo na kwamba vinagharimu kiasi cha shilingi milioni 9.5.
Alisema shule hiyo ambayo ni ya mfano kutembelea imekuwa na mambo mengi mazuri ya kujifunza kama vile uwezo watoto hao darasani na ari ya walimu kufundisha kitu kinachopaswa kuigwa.
Alianisha vifaa walivyovitoa kuwa ni madaftari, kalamu za wino na risasi, viti mwendo, vifaa vya usafi, mipira, sabuni, maandishi ya nukta nundu, midoli, ndoo za kuhifadhia maji na vifaa vingine.
“Tumefurahia mazingira ya shule kwa kipindi hiki cha wiki mbili tulichokaa na kuwafundisha watoto na tunaahidi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuendeleza ushirikiano katika eneo hili la kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalumu,” alisema Bente Dale.
Akipokea msaada wa vifaa hivyo, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo, Hajrati Kashakara, alisema vitasaidia kupunguza tatizo la uhaba wa wa vifaa hivyo kwa watoto hao,aliomba ushirikiano huo uendelee ili wapate vitu vingi kwa ajili kuwasaidia kusoma katika mazingira mazuri.
Mwalimu asiyeona, Saada Kiponza ambaye anafundisha wanafunzi wasioona hatua ya kwanza hadi ya tatu, alisema anafurahia kazi yake kwa sababu anafundisha watu wenye changamoto kama yake na kwamba anapofundisha anahakikisha wanamuelewa kwa sababu anajua mbinu za kuwasiliana nao.
Aliongeza kuwa licha ya kufurahia kuwafundisha watu wenye tatizo kama lake lakini anakabiliwa na tatizo la vifaa vya kufundishia,kujifunzia na miundombinu ya shule kutokuwa rafiki kwao hali inayohatarisha afya na usalama wao.
“Nimekuwa mwalimu kwa miaka 22 sasa nikifundisha mikoa mbalimbali naipenda kazi yangu na ninamshukuru Mungu watoto wangu wananielewa na wanafanya vizuri kwenye mitihani yao”, alisema Saada.
Aidha alisema kuna changamoto katika ufundishaji kwa baadhi ya watoto wenye wenye ulemavu zaidi ya mmoja hali ambayo ni ngumu kumudu lakini kama walimu wanajitahidi kwa sababu wanafunzi hao ni marafiki zao wa ukweli.
Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dk. Mariana Makuu alisema mahitaji ya kutunza watoto wenye mahitaji maalum shuleni ni makubwa kwa wakati huu kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto katika jamii.
“Tunaiomba serikali kuajiri maofisa ustawi wa jamii kwenye shule zote jumuishi ili kuongeza nguvu ya kuwasaidia watoto hao,kielimu, kiakili na kiafya ili kuwa sawa kama watoto wengine”, alisema Dkt.Makuu.
Alisema idadi kubwa ya watoto wenye mahitaji maalumu shuleni wanashindwa kutimiza ndoto zao za elimu kwa sababu ya kukosa uangalizi maalumu ili kusoma vizuri kama watoto wengine hivyo uwepo wa wataalamu wa ustawi wa jamii utasaidia kuwahakikishia ustawi na maendeleo yao.
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambacho kinatekeleza programu za kuwasaidia watu wenye ulemavu nchini kina ushirikianio na taasisi za elimu ya juu ndani na nje ya nchi ikiwemo kutoka Norway ambapo kinahusisha kubadilishana uzoefu kwa wahadhiri na wanafunzi katika maeneo ya ufundishaji na mafunzo kwa vitendo.
Sehemu ya picha katika matukio ya hivi karibuni wakati wa kukabidhi misaada ya vifaa katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko jijini Dar es Salaam tukio lililohudhuriwa na wahadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambao ni wenyeji, wahadhiri na wanafunzi kutoka vyuo vikuu vya Norway, walimu na wanafunzi wa shule hiyo. Vifaa hivyo vitapunguza tatizo la uhaba wa nyenzo za kufundishia, kujifunzia na vinakadiriwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni tisa na nusu za kitanzania.
Picha2: Bidhaa za kazi za mikono zinazotenegezwa na Kikundi cha Uhuru Mamas ambacho kinajumuisha akina mama wenye watoto wa mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko iliyopo jijini Dar es salaam ambacho ni sehemu ya mradi unaotekelezwa kati ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na vyuo vikuu vya Molde na Chuo Kikuu Kishiriki cha Sayansi Shirikishi vya Norway(Picha na Vincent Mpepo, OUT.
Na Mwandishi wetu, OUT
Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Mariana Makuu, ameishauri Serikali kuajiri wataalamu wa ustawi wa jamii katika shule za msingi jumuishi ili kuwaweka sawa kiakili na kisaikolojia watoto hao wawapo shuleni.
Wito huo umetolewa wakati wa kukabidhi misaada ya vifaa katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko huko Dar es Salaam leo jijini Dar es salaam na kuhuduriwa na wahadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambao ni wenyeji, wahadhiri na wanafunzi kutoka vyuo vikuu vya Norway, walimu na wanafunzi wa shule hiyo.
Dkt. Makuu ameeleza kwamba kuwepo kwa wataalamu wa ustawi wa jamii katika shule hizo kutaweza kusaidia kikamilifu watoto wenye mahitaji maalum ambao mara nyingi wanakosa mtu wa karibu kuelewa mahitaji yao wanapokuwa shuleni. Anasisitiza kuwa matunzo, uangalizi, na malezi kwa watoto hawa yanakabiliwa na changamoto nyingi, na hivyo kuna haja ya kuwa na wataalamu wa kutosha katika eneo hilo.
“Kuajiri wataalamu wa ustawi wa jamii kutapunguza athari hasi katika malezi na makuzi ya watoto hao, na hivyo kuwasaidia kufikia ndoto zao kielimu”, alisema Dkt.Makuu.
Alisema, kwa kuzingatia majukumu mazito ya walimu katika kutekeleza mtaala upo umuhimu wa kuwa na wataalamu wa ustawi wa jamii ambao watasaidia katika mambo mengine yanayohusiana na malezi na makuzi ya watoto hususani wenye mahitaji maalumu.
Aidha, alisisisitiza kwamba idadi kubwa ya watoto wenye mahitaji maalum katika shule wanakabiliwa na changamoto za kielimu kutokana na kukosa uangalizi maalum hivyo kukwama au kutofika mbali katika elimu.
Kwa upande wake, mwanafuzni wa ustawi wa jamii kutoka kutoka Norway, Marianne Valsvik alisema wanajisikia vizuri kuwa sehemu ya kuwafariji watoto kwa vifaa mbalimbali vitakavyosaidia katika kusoma, usafi na mahitaji mengine.
“Nimejifunza mengi hapa Tanzania kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii na namna watoto wenye mahitaji maalumu wanavyoishi”, alisema Marianne.
Mwakilishi wa wanafunzi kutoka Norway, Karoline Lie alisema msaada huo unajumisha vifaa mbalimbali ikiwemo vya usafi, madaftari, kalamu za risasi na wino, maboksi ya vifaa vya msaada wa kwanza, viti vya na vinagharimu zaidi kiasi cha shilingi milioni tisa na nusu za kitanzania.
“Vifaa vingine ni pamoja na makabati ya kuhifadhia vifaa vya walimu, vifaa vya ichezo mbalimbalimbali, matanki, mabeseni na vifaa vingine vya jikoni”, alisema Karoline
Tanzania imesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa ya watu wenye ulemavu ikiwemo mkataba wa haki za mtoto, CRC mwaka 1989 ambapo mataifa yalikubaliana kuwa na sheria na kanuni za kulinda haki za watoto kwa mataifa
Head of the Department of Social Work and Sociology at the Open University of Tanzania, Dr. Mariana Makuu, has advised the government to employ social work experts in inclusive primary schools to ensure the mental and psychological well-being of children while at school.
The call was made during the donation handover at Uhuru Mchanganyiko Primary School in Dar es Salaam yesterday which was attended by lecturers from the Open University of Tanzania, Norwegian university lecturers and students, teachers, and pupils from the school.
Dr. Makuu explained that having social work experts experts in these schools would fully assist children with special needs who often lack someone close to understand their needs while at school. She emphasized that the care, supervision, and upbringing of these children face many challenges, hence the need for an adequate number of experts in this field.
“Hiring social work experts will reduce the negative impact on the upbringing and development of these children, thus helping them achieve their educational dreams as normal children,” said Dr. Makuu.
She further emphasized the importance of having social work experts to assist in other aspects related to the upbringing and development of children, especially those with special needs, considering the heavy responsibilities of teachers in implementing the curriculum.
She said a large number of children with special needs in schools face educational challenges due to lack of special attention, thus hindering or limiting their progress in education.
On her part, Marianne Valsvik, a social welfare student from Norway, expressed satisfaction in being part of comforting children with various materials that will aid in their studies, hygiene, and other needs.
“I have learned a lot here in Tanzania about various social issues and how children with special needs live,” said Marianne.
Representing the students from Norway, Karoline Lie said that the assistance includes various materials such as hygiene items, notebooks, pens, first aid kits, chairs, and costs more than nine and a half million Tanzanian shillings.
“Other items include teacher storage cabinets, various play equipment, tanks, basins, and kitchen utensils,” said Karoline.
Tanzania has signed various international agreements on people with disabilities, including the Convention on the Rights of the Child (CRC) in 1989, whereby member states agreed to have laws and regulations to protect the rights of children.
Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Mariana Makuu akisisitiza jambo wakati wa kikao cha tathmini ya kutekeleza program za kuwasaidia watu wenye ulemavu kikiwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo, wahadhiri, walimu, maofisa maendeleo ya jamii na wafadhili kutoka nchini Norway iliyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni katika ukumbi wa chuo hicho.
Na Grace Mwakalinga, Dar es salaam
Serikali imeshauriwa kuajiri wataalamu wa ustawi wa jamii kwenye shule za msingi jumuishi ili kuwahudumia kikamilifu watoto wenye mahitaji maalum ambao wakati mwingine hukosa mtu wa karibu kujua mahitaji yao wawapo shuleni.
Mapendekezo hayo yametolewa na Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Mariana Makuu wakati wa kikao cha tathmini ya kutekeleza program za kuwasaidia watu wenye ulemavu kikiwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo, wahadhiri, walimu, maofisa maendeleo ya jamii na wafadhili kutoka nchini Norway iliyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni katika ukumbi wa chuo hicho.
Alisema mahitaji ya matunzo kwa watoto wenye mahitaji maalumu kwenye jamii na waliopo shuleni ni makubwa kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hivyo kuna uhitaji wa walimu kuongezewa nguvu kutoka kwa wataalamu wa ustawi wa jamii ambao watafanya kazi pamoja na walimu hao ili kuhahikisha ustawi wa watoto katika mazingira ya shule na jamii kwa ujumla.
“Walimu peke yao hawawezi kwani wana majukumu ya kutekeleza mtaala lakini hili la kuwasaidia kwa mambo mengine linaweza kufanyiwa kazi vyema na wataalamu wa ustawi wa jamii”, alisema Dtk. Makuu.
Alisema kutokana na changamoto hiyo Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinaishauri serikali kuajiri wataalamu wa ustawi wa jamii kwenye shule zote jumuishi ili kuongeza nguvu ya kuwasaidia watoto hao kielimu, kiakili na kiafya ili wawe sawa kama watoto wengine.
“Idadi kubwa ya watoto wenye mahitaji maalum shuleni wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na kukosa uangalizi maalum ili kusoma vizuri kama watoto wengine, alisema Dkt.Makuu.
Mwalimu wa shule ya msingi jumuishi ya Uhuru Mchanganyiko, Catherine Chitanda, alisema utaratibu huo utakuwa mwarobaini wa kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum shuleni kwa kupata usaidizi wa karibu kutoka kwa wataalamu wa ustawi wa jamii ambao watakuwepo shuleni kuwahudumia.
Aidha Catherine alisema katika kufanikisha hilo, lazima serikali ikubali kushirikiana na jamii, walimu na wataalamu wa ustawi wa jamii ili kutimiza kikamilifu jukumu la kuwatunza na kuwalea watoto wenye mahitaji maalum shuleni.
Mtalaam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Stella Shayo, alisema katika kutekeleza programu hiyo chuo kimejipanga kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia kwa wazazi, walezi na jamii juu ya athari za vitendo hivyo ili kuwaweka sawa kisaikolojia watoto hao wawapo shuleni.
Kwa upande wake, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kinondoni, Silider Ussuma alisema anaunga mkono jambo hilo na kwamba litasaidia kuwaweka sawa kiakili watoto wenye mahitaji maalumu.
Alisema sababu mojawapo inayosababisha changamoto kwa watoto ni migogoro ya mara kwa mara kwa baadhi ya wanandoa ambayo ina athari hasi kwa watoto na wakati mwingine kutofanya vizuri kitaaluma na hivyo uwepo wa wataalamu wa ustawi wa jamii utasaidia kuwapa ushauri watoto ili wawe sawa kiakili.
Tanzania imesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa ya watu wenye ulemavu ikiwemo mkataba wa haki za mtoto, CRC mwaka 1989 ambapo mataifa yalikubaliana kuwa na sheria na kanuni za kulinda haki za watoto kwa mataifa wanachama.
Sehemu ya washiriki wa kikao cha tathmini ya kutekeleza program za kuwasaidia watu wenye ulemavu kikiwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo, wahadhiri, walimu, maofisa maendeleo ya jamii na wafadhili kutoka nchini Norway iliyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni katika ukumbi wa chuo hicho.
Serikali imetakiwa kuajiri maofisa ustawi wa jamii kwenye shule za msingi jumuishi ili kuwahudumia kikamilifu watoto wenye mahitaji maalum ambao wakati mwingine hukosa mtu wa karibu kujua mahitaji yao wawapo shuleni.
Mapendekezo hayo yametolewa na Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Dkt. Mariana Makuu wakati wa kikao cha tathmini ya kutekeleza program za kuwasaidia watu wenye ulemavu kikiwahusisha wadau mbalimbali wakiwemo, wahadhiri, walimu, maofisa maendeleo ya jamii na wafadhili kutoka nchini Norway iliyofanyika jijini Dar es salaam hivi karibuni katika ukumbi wa chuo hicho.
Alisema mahitaji ya matunzo kwa watoto wenye mahitaji maalumu kwenye jamii na waliopo shuleni ni makubwa kutokana na kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia hivyo kuna uhitaji wa walimu kuongezewa nguvu kutoka kwa maofisa ustawi wa jamii ambao watafanya kazi pamoja na walimu hao ili kuhahikisha ustawi wa watoto katika mazingira ya shule na jamii kwa ujumla.
“Walimu peke yao hawawezi kwani wana majukumu ya kutoa elimu lakini hili la kuwasaidia kwa mambo mengine linaweza kufanyiwa kazi na maafisa ustawi wa jamii”, alisema Dtk. Makuu.
Alisema kutokana na changamoto hiyo Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinaishauri serikali kuajiri maofisa ustawi wa jamii kwenye shule zote jumuishi ili kuongeza nguvu ya kuwasaidia watoto hao kielimu, kiakili na kiafya ili wawe sawa kama watoto wengine.
“Idadi kubwa ya watoto wenye mahitaji maalum shuleni wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na kukosa uangalizi maalum ili kusoma vizuri kama watoto wengine, alisema Dkt.Makuu.
Mwalimu wa shule ya msingi jumuishi ya Uhuru Mchanganyiko, Catherine Chitanda, alisema utaratibu huo utakuwa mwarobaini wa kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum shuleni kwa kupata usaidizi wa karibu kutoka kwa maofisa hao ambao watakuwepo shuleni kuwahudumia.
Aidha Catherine alisema katika kufanikisha hilo, lazima serikali ikubali kushirikiana na jamii, walimu na maafisa ustawi wa jamii ili kutimiza kikamilifu jukumu la kuwatunza watoto wenye mahitaji maalum shuleni.
Mtalaam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Stella Shayo, alisema katika kutekeleza programu hiyo chuo kimejipanga kutoa elimu juu ya ukatili wa kijinsia kwa wazazi, walezi na jamii juu ya athari za vitendo hivyo ili kuwaweka sawa kisaikolojia watoto hao wawapo shuleni.
Kwa upande wake, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kinondoni, Silider Ussuma alisema anaunga mkono jambo hilo na kwamba litasaidia kuwaweka sawa kiakili watoto wenye mahitaji maalumu.
Alisema sababu mojawapo inayosababisha changamoto kwa watoto ni migogoro ya mara kwa mara kwa baadhi ya wanandoa ambayo ina athari hasi kwa watoto na wakati mwingine kutofanya vizuri kitaaluma na hivyo uwepo wa maafisa ustawi utasaidia kuwapa ushauri watoto ili wawe sawa kiakili.
Tanzania imesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa ya watu wenye ulemavu ikiwemo mkataba wa haki za mtoto, CRC mwaka 1989 ambapo mataifa yalikubaliana kuwa na sheria na kanuni za kulinda haki za watoto kwa mataifa wanachama.
Mahakama ya Wilaya Singida imemuhukumu Baraka Joel ambaye pia anajulikana kwa jina la Yohana (23), mkulima na mkazi wa Mughamo Manispaa ya Singida kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka.
Mshitakiwa Baraka alitenda kosa hilo Februari 17, 2023 huko Mtaa na Kata ya Mughamo, Tarafa ya Ilongero, Wilaya na Mkoa wa Singida ambapo alimbaka mwanafunzi wa darasa la 7 mwenye umri wa miaka 14.
Baada ya kutenda kosa hilo, Mshitakiwa alikamatwa na Jeshi la Polisi na kufikishwa mahakamani Machi 8, 2023 na kesi kusikilizwa na pande zote mbili. Kutokana na ushahidi uliowasilishwa na upande wa mlalamikaji, ulithibitisha mshitakiwa alitenda kosa hilo hivyo Mahakama kutoa adhabu hiyo Machi 14, 2024 mbele ya Mh. Hakimu Robert Uguda.