• Na Damas Kalembwe

    Mkuu wa Ushirikishwaji Jamii wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Ally S. Wendo, akimwakilisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, SACP Mtatiro Kitinkwi, ameongoza kikao kazi na Kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Wilaya ya Kinondoni (USHITA), kilichofanyika katika ukumbi wa Club 361, Mwenge jijini Dar es Salaam.

    Akizungumza katika kikao hicho, ACP Wendo alitoa wito kwa wanachama wa umoja huo kuendeleza uwajibikaji, nidhamu na mshikamano katika kutekeleza majukumu yao, akibainisha kuwa ulinzi shirikishi ni nyenzo muhimu katika kudumisha utulivu wa mijini.

    “Amani ni injini ya maendeleo bila kuwa na utulivu hakuna shughuli za kiuchumi zinazoweza kufanyIka”, alisema ACP Wendo.

    Aidha, aliwataka wanachama kuendeleza utamaduni wa kuchangia ada walizojiwekea ili kuimarisha uwezo wa kifedha wa umoja huo na kuweka msingi imara wa utoaji wa huduma kwa wanachama.

    “Ninawaomba muendelee kuwa mabalozi wa amani katika mitaa yenu na kuendelea kushirikiana na Polisi kwa maslahi mapana ya usalama wa wananchi”, alisema ACP Wendo.

    Kwa upande wake, Mwenyekiti wa USHITA, Ndugu George, aliishukuru Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa kujitoa mara kwa mara kutoa elimu ya ulinzi shirikishi, akieleza kuwa mwamko huo umeongeza uelewa na kuimarisha mahusiano kati ya jamii na Jeshi la Polisi.”Tunaona matokeo chanya ya elimu hii. Tunaiomba iendelee kufikishwa kwa wananchi wengi zaidi ili kujenga jamii inayowajibika, yenye uelewa wa usalama na umoja,” alisema.

    Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa kikundi hicho, Lilygray Mwikosi, aliahidi kuwa USHITA itaendelea kuwa mshirika thabiti wa Jeshi la Polisi katika kulinda amani ya Dar es Salaam na taifa kwa ujumla.

    “Amani ndiyo msingi wa ustawi wa maisha na uchumi. Tukiiweka hatarini, tunahatarisha kila hatua ya maendeleo tunayoyapa nchi yetu, alisema Lilygray.

    Kikao hicho kimehitimishwa kwa makubaliano ya kuimarisha mifumo ya mawasiliano, mafunzo na uratibu kati ya Jeshi la Polisi na kikundi cha USHITA ili kukuza ufanisi wa shughuli za ulinzi shirikishi katika Mkoa wa Kinondoni.

    Kikao hicho ni mwendelezo wa kuimarisha ushirikiano kati ya Jeshi la Polisi na vikundi vya ulinzi shirikishi, sambamba na kukuza uelewa kuhusu nafasi ya wananchi katika kulinda amani na usalama wa maeneo yao.

    Kikundi cha Umoja wa Ulinzi Shirikishi Tanzania (USHITA), ni umoja wa wanachama wanaojitolea kuimarisha ulinzi wa jamii, pia hujishughulisha na mfuko wa kuchangiana kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za kifamilia na za kijamii zinazoikumba jumuiya yao.

  • Na Vincent Mpepo

    Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wametakiwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuboresha utoaji wa huduma na kukuza mapato ya chuo hicho.

    Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Alex Makulilo, alitoa wito huo jana katika hafla ya uzinduzi wa gari jipya la ofisi yake iliyofanyika Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

    Alisema menejimenti ya chuo inaendelea kuboresha mazingira ya kazi kadiri uwezo wa kifedha unavyoruhusu.

    “Natambua kuna mahitaji mengi ikiwemo samani na vitendea kazi vingine, lakini tutajitahidi kuboresha mazingira ya kazi kulingana na uwezo wetu,” alisema Profesa Makulilo.

    Aidha, alilipongeza kila kitengo kilichohusika katika mchakato wa ununuzi wa gari hilo na kubainisha kuwa fedha zilizotumika zimetokana na mapato ya ndani ya chuo.

    Kwa upande wake, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Huduma za Mikoa na Teknolojia za Kujifunzia, Profesa Leonard Fweja, alisema kuwa gari hilo limekuja kwa wakati muafaka, na litasaidia kuboresha usafiri wa kiongozi huyo katika kutekeleza majukumu mbalimbali, ikiwemo kuvifikia vituo vya mikoa vya chuo hicho mikoani.

    Naye Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Masuala ya Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu, ambaye pia ni Mkuu wa Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii, Dkt. Dunlop Ochieng, alisema kuwa upatikanaji wa gari hilo ni matokeo ya kufanya kazi kwa bidii.

    “Haya ni matunda ya juhudi za pamoja na ninawaomba wafanyakazi wenzangu tuendelee kujituma kwa sababu kufanya kazi kwa bidii kunalipa,” alisema Dkt. Ochieng.

    Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo wa Chuo, Benjamin Bussu, alisema mchakato wa ununuzi wa gari hilo ulianza Februari 2025 na umefuata taratibu zote, ikiwemo kuomba kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi, kwa kuwa chuo kilihitaji gari linaloendana na hadhi ya taasisi na kiongozi wake.

    “Ninatoa rai kwa madereva kulitunza gari hili na kulitumia kwa uangalifu ili kuhakikisha usalama wa viongozi,” alisema Bussu.

    Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, gari lililonunuliwa ni Toyota Land Cruiser, ambalo limegharimu kiasi cha shilingi milioni 386.

    Uzinduzi wa gari hilo ulitanguliwa na dua, sala na maombi kutoka kwa watumishi mbalimbalimbali chuoni hapo ikiwemo mhadhiri Msaidizi na Mchungaji Hanington Kabuta, Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa chuo hicho Francis Badundwa na Dtk. Omari Mohamed suala linalodhihirisha imani na heshima kwa Mungu wakitambua kuwa kila kitu kiafanyika kwa uwezo wa Mungu.

  • Na Vincent Mpepo, Songea

    Wataalamu wa afya wa Zahanati ya Kijiji cha Mlete iliyopo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamepongezwa kwa moyo wao wa kujitoa na kujituma katika kuhudumia wagonjwa.

    Hayo yamebainishwa na ndugu wakiwemo watoto wa marehemu Amalia Chilongo wakati wa ibada ya mazishi yake jana huku ikibainika wazi kuwa watumishi wa Zahanati hiyo walikuwa tayari kufanya kazi muda wote walipohitajika kmhudumia marehemu Amalia.

    Akizungumza kwa niaba ya familia, mtoto wa marehemu Manswetus Mwimba aliwashukuru wauguzi hao ikiwa ni miongoni wanajamii aliowashukuru wakati akitoa shukrani za familia wakati wa ibada hiyo.

    “Kipekee ninapenda kuwashukuru sana wataalamu wa afya wa Zahanati ya Mlete kwa namna ambavyo walijitahidi kuokoa maisha ya mama yetu hata walipohitajika muda nje ya kazi”, alisema Mwimba.

    Aliwaomba waendelee na moyo huohuo kwani kufanya hivyo siyo tu kutimiza majukumu lakini pia ni baraka na matendo mema.

    Aidha aliwashukuru ndugu, jamaa, marafiki na wageni wote waliofika na kuhudhuria katika safari ya mwisho ya mama yake na kuwatakia kila la kheri katika safari za kurejea makwao.

    Akihubiri katika ibada hiyo, Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu, Shule ya Tanga Jimbo Kuu la Songea, Padre Soo Sai Raj aliwataka wakristo kujiandaa na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu kwa kuwa hakuna ajuaye siku wala saa ya kuitwa kwake.

    Alisema kifo siyo mwisho wa maisha na muhimu zaidi ni kumuomba Mungu awajalie imani na waishi katika kulielewa fumbo hilo huku kila mmoja akifanya maandalizi.

    Marehemu Bi. Amalia Chilongo alizaliwa mwaka 1935 na alifunga ndoa takatifu 1953 Mzee Daniel Mwimba (sasa marehemu) na katika uhai wao walijaaliwa kupata watoto sita na marehemu ameacha watoto 5, wajukuu 28, vitukuu 61, na vilembwe 4.

    Ibada hiyo ya mazishi ilihudumiwa na Katekista Aron Mhagama na Kwaya ya Umoja ya Kigango cha Mlete ikijumisha kwaya ya Mtakatifu Joseph na Mtakatifu Bernadeta zote za kigango hicho huku ibada hiyo ikuhudhuriwa na wageni kutoka sehemu mbaalimbali mkoani Ruvuma na nje ya mkoa.

  • Na Vincent Mpepo, Mtwara

    Wanandoa katika jamii wametakiwa kuishi kwa upendo, kusameheana na kuvumilana kwa kuwa kila mwanadamu ana udhaifu wake na hakuna mkamilifu.

    Wito huo ulitolewa jana na Paroko wa Parokia ya Yesu Kristo Mkombozi – Magomeni, Jimbo Katoliki la Mtwara, Padre Silvanus Chikuyu wakati wa mahubiri katika ibada ya ndoa kati ya Edgar Joseph na Maria Danford na kusisitiza kuwa wanandoa wanapaswa kuishi kwa kuchukuliana ambako kuna msamaha, upendo na zaidi malengo mema ya kujenga familia.

    Alisema kama wanandoa wana wajibu na ni mpango wa Mungu kuzaa watoto kuwalea na kuwatunza vizuri kiroho na kimwili ili kuendela kuwa na jamii inayomjua Mungu na yenye maadili mema.

    “Mpango wa Mungu ni kuwa mkazae na kuijaza dunia, lakini msiishie tu kuzaa bali mkawalee watoto mtakaojaaliwa katika maadili mema”, alisema Padre Chikuyu

    Aidha aliwataka ndugu na jamaa kutokuwa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa badala yake wawe kimbilio na wasuluhishi wema ili kuifanya ndoa hiyo kudumu.

    “Wakati mwingine wazazi, walezi, wifi na shemeji wamekuwa ni chanzo cha kuvunjika kwa ndoa, ninaomba ndugu na wasimamizi muwasaidie wanandoa hawa”, alisema Padre Chikuyu

    Wakati wa hafla ya ndoa hiyo iliyofanyika katika Bwalo la Maafisa wa Polisi Mtwara, Mwakilishi wa familia ya Edgar Joseph, Francis Mpepo aliwataka wandoa kuishi kwa kujaliana iwe kwa shida na raha kwa kuangalia pande zote za upande wa mume na mke.

    “Likitokea kwa mume, mke uwe wa kwanza kusaidia na kushauri na kwa likitokea kwa mke mume pia uhusike”, alisema Francis.

    Mama wa bibi harusi, Zenapokea Makota, katika nasaa zake kwa wanandoa hao hao alimkumbusha Maria umuhimu wa kumpikia mumewe.

    “Natamani usiende kununua vitumbua wala njugu kwa mama ntilie, badala yake uwe unapika mwenyewe nyumbani kwako”, alisema Bi Makota.

    Kwa upande wake mwakilishi wa madereva Benedicto Tesha aliwaasa wanandoa hao kuwakimbilia wafanayakazi wenzao wakati wa shida na raha.

    “Ninakuomba Edgar na mkeo Maria muwe na utayari kuwakimbilia wenzenu iwe katika shida au raha”, alisema Tesha.

    Hafla ya ndoa hiyo imeshuhudiwa na kuhudhuriwa na wafanyakazi wa Idara mbalimbali za serikali kutoka Manispaa ya Mtwara ikiwemo Idara ya elimu sekondari, Idara ya fedha, Idara ya utawala na madereva kitu kinachoonesha uhusiano mzuri wa wafanyakazi katika manispaa hiyo.

  • Na Damasi Kalembwe-Dar es Salaam

    Shule ya Sekondari Saranga iliyopo Mtaa wa Matangini, Kata ya Saranga, imefanya mahafali ya kuhitimu Kidato cha Nne ambapo pamoja na sherehe hizo, wanafunzi na wazazi walipata elimu ya ushirikishwaji jamii kutoka Jeshi la Polisi.

    Katika mahafali hayo, Polisi wa Kata ya Saranga Insp. Elias na Polisi wa Kata ya Kimara Insp. Mussa walihudhuria na kutoa mada kuhusu umuhimu wa kushirikiana na jamii katika kulinda usalama, kupinga vitendo vya uhalifu na kuimarisha maadili kwa vijana.

    Sherehe hizo zilihudhuriwa na walimu wakuu wa shule za binafsi na za serikali za Kata ya Saranga, walimu na wafanyakazi wa shule, wazazi pamoja na wageni waalikwa huku mgeni rasmi alikuwa mwakilishi wa uongozi wa elimu kata hiyo.

    Viongozi hao wa polisi walisisitiza kuwa elimu na nidhamu ni nguzo muhimu za maendeleo ya taifa na kuwataka wahitimu kutumia vyema maarifa waliyoyapata kwa faida yao na jamii inayowazunguka.

  • Na Vincent Mpepo, Karatu

    Wakristo wamekumbushwa faida na umuhimu wa kumtolea Mungu kwa uaminifu sadaka mbalimbali hususani fungu la kumi.

    Ukumbusho huo umetolewa na Mwalimu wa neno la Mungu, Tumsifu Lema katika mahubiri wakati wa ibada ya kwanza katika ibada Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) leo, katika Usharika wa Karatu Mjini, Dayosisi ya Kaskazini, Jimbo la Karatu Mjini.

    Alisema kuna faida nyingi za kumtolea Mungu kwa uaminifu na kuwa hakuna ambaye anamtolea Mungu kwa kumaanisha ataachwa hivyo alivyo akibanisha mojawapo ya faida ni kufunguliwa milango ya baraka.

    “Mtu yeyote anayekwenda mbele za Mungu kwa uaminifu, imeahidiwa atafunguliwa milango ya baraka”, alisema Mwalimu Tumsifu.

    Alianisha milango katika aina mbili ikiwemo inayoonekana naisiyoonekana na kwamba wakristo wengi wana ufahamu na milango inayoonekana zaidi ya ile isiyoonekana ambayo hutumiwa na watu wema na wabaya kutimiza malengo yao.

    “Kuna milango ya kiroho ikifungwa utapata tabu sana”, alisema Mwalimu Tumsifu.

    Aliongeza kuwa faida nyingine ya kuwa mwaminifu katika kumtolea Mungu sadaka ya fungui la kumi kuwa ni ulinzi dhidi ya maadui na kuinua uchumi wa mtoaji na kusisitiza kuwa kila mtu ana maadui kutokana na kitu afanyacho na wanaweza kuwa ni maadui wa mbali au wa karibu.

    “Kuna watu wakikutazama wana wivu mbaya”, alisema Mwalimu Tumsifu.

    Alianisha mambo muhimu ya kuzingatia katika utoaji akisisitiza kwa mtoaji kusamehe waliomkosea hata kama hawakuomba msamaha na kwamba utoaji wenye manung’uniko na lawama.

    Aliwataka wakristo kuwa waangalifu na maneno au nia wawekazo wanapoenda kumtolea Mungu kwa kuwa Mungu hadhihakiwi na hujibu akitolea mfano wakristo ambao huahidi nyakati za harambee bila kutekeleza na kuwa wasikivu kwa sauti ya Mungu ndani yao.

    Kwa upande wake, Mchungaji Kiongozi Usharika wa Karatu Mjini, Fanuel Sippu aliwakumbusha washarika kukamilisha michango ya sadaka kwa ajili ya Sikukuu ya Mikael na Watoto ambayo imekaribia ili kufanya siku hiyo muhimu kwao kuwa ya kuvutia.

    Aidha aliwaomba kuchangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa kanisa jipya la moja ya mtaa unaohudumiwa na Usharika huo.

  • By Vincent Mpepo

    It has been emphasized that men in society should seek happiness and strengthen their bonds with their families in order to live longer, healthier lives in order to reduce mental health challenges, stress and the risks of early death when compared to women.

    These insights were shared by participants in an online seminar for men, held on September 16, 2025. The seminar was organized by the Gender Unit of the Open University of Tanzania in collaboration with various stakeholders.

    During the seminar, the former Vice Chancellor of the Open University of Tanzania, Professor Elifas Bisanda, shared his views on the biblical and historical relationship between men and women. He highlighted that historically, men were seen as the primary decision-makers in family matters, a dynamic that has since changed.

    Professor Bisanda explained that in traditional African customs, the practice of a man paying dowry when marrying gave him power and authority over women, with the community expecting the man to be the source of success in the family.

    He remarked, “The expectation was that the man would bring success to the household; if he failed, the whole family failed.”

    However, as the world has moved towards modernization, many aspects have changed, and it is important to address how young boys are raised.

    He pointed out that while there has been significant investment in empowering girls, much less focus has been placed on preparing boys to be men and husbands.

    Professor Bisanda also discussed the unequal access to educational opportunities, noting that there are far more schools and educational programs for girls than for boys, which is a worrying trend for the future of boys.

    He expressed concern that such disparities could lead to feelings of abandonment and hopelessness among boys, which might result in destructive behaviors such as drug abuse and gambling.

    Dr. Ally Abdallah, a law lecturer at the Open University of Tanzania, discussed several theories that have historically shaped the role of men in society.

    He explained that men were traditionally given greater authority due to their role as primary providers, though there is no scientific evidence supporting the idea that men inherently possess more power than women.

    He emphasized that in today’s world, men need to shift their mindset to embrace the idea of equality, where both men and women have the capacity to contribute to family success.

    “The idea that women were merely assistants or dependents is no longer valid,” Dr. Abdallah said.

    He noted that the rise of women’s education, employment, and economic empowerment has led to increased conflicts, and sometimes the breakdown of marriages, due to shifting power dynamics and differing expectations between men and women.

    He added that while biological gender roles, such as the ability of women to bear children, will remain, other social responsibilities like cooking and cleaning, which were once considered women’s duties, should now be shared between men and women.

    Dr. Katanta Simwanza, a Senior Technical Advisor for Gender, Sexuality, Child Protection, and Family Health, discussed the importance of addressing gender issues, which he believes have contributed to many challenges faced by men today. “The painful truth is that many men are passing away prematurely due to gender-related issues,” Dr. Simwanza stated.

    He further pointed out that there are significant benefits to couples working together in family settings. These benefits include shared vision and responsibilities, with women sometimes taking the lead in managing family resources. “In families where there is mutual respect and shared responsibility, the results are often more positive,” he said.

    Dr. Simwanza stressed the importance of every family having clear guidelines and roles for each member to ensure that all family members are empowered and contribute effectively.

    The seminar was organized by the Gender Department of the Open University of Tanzania, in partnership with the non-governmental organization MBS Trinity Care. The event aimed to raise awareness about the role of men in empowering women, breaking down harmful stereotypes, fostering gender cooperation, and encouraging men to become ambassadors for positive change in society.

    The seminar, which was hosted by a journalist from the Tanzania Broadcasting Corporation (TBC), Njwaba Mwaijibe captured the attention of many participants and sparked diverse reactions.

    This indicates the presence of challenges that require concerted efforts, particularly when it comes to raising and nurturing boys in society.

  • Na Vincent Mpepo, Karatu

    Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mstaafu, Profesa Elifas Bisanda ametoa wito kwa mamlaka za elimu kuingiza masomo ya Astronomia (anga za mbali) katika mtaala wa elimu kuanzia ngazi ya shule za msingi ili kuandaa wataalamu wa baadaye katika sekta hii mpya na inayochipukia kwa kasi.

    Akizungumza katika siku ya kwanza ya mafunzo ya utalii wa anga za mbali (Astrotourism) yaliyofanyika Karatu, Arusha, Prof. Bisanda alisema utalii wa anga ni eneo jipya lenye fursa kubwa za kiuchumi kwa Tanzania na kuwaandaa wataalamu mapema kutaiwezesha nchi kunufaika ipasavyo.

    “Kuanzisha masomo ya Astronomia na utalii unaohusiana nayo shuleni kutasaidia kuandaa wataalamu mahiri watakaoweza kutumia fursa hii ipasavyo,” alisema Prof. Bisanda.

    Aliwahimiza washiriki wa mafunzo hayo kujiunga na Asasi ya Uhamasishaji Uhifadhi wa  Anga-giza la Tanzania unaolenga kulinda anga za usiku wenye giza totoro na kuendeleza utalii wa anga ili waanze kutekeleza kwa vitendo mafunzo waliyopata.

    Kwa upande mwingine, Dkt. Noorali Jiwaji, Mhadhiri Mwandamizi wa Fizikia na mtaalamu wa Astronomia kutoka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, alieleza masikitiko yake kuhusu kuondolewa kwa mada ya Astronomia katika mtaala mpya wa somo la Fizikia kwa Kidato cha Nne.

    “Nashangaa tutawapata wapi wanafunzi wenye msingi wa astronomia wakati mtaala wenyewe umelitupa somo hili muhimu,” alisema Dkt. Jiwaji.

    Kuhusiana na utalii wa anga za mbali (Astrotourism), Dkt Noorali Jiwaji amepewa tuzo la kulinda anga-giza hapa Tanzania na Chama cha Kimataifa cha Anga-giza.

    Naye Nalayini Davis, Rais wa Chama cha Kimataifa cha Anga-giza kutoka New Zealand, alisema kuwa ni wakati muafaka kwa Tanzania kuanza rasmi utalii wa anga kwani ina faida ya kijiografia na hali nzuri ya hewa inayofaa kwa shughuli hiyo.

    “Tanzania ina nafasi kubwa ya kuwa kinara wa utalii wa kutazama nyota barani Afrika. Ni lazima ichukue hatua sasa,” alisema Nalayini.

    Mafunzo hayo utalii wa anga yameandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), yameendeshwa na wataalamu kutoka New Zealand na Marekani, na kuhudhuriwa na washiriki 70 kutoka sekta binafsi na ya umma katika tasnia ya utalii wa ndani kutoka nchi mbalimbali.

  • Na Mchungaji Hang’tone Kabuta