Kusini Kwetu
Habari za ndani na nje nchi
recent posts
- Tanzania Yaunga Mkono Kuimarisha Ushirikiano wa Kibunge kupitia NAM-PN
- Nidhamu Yatajwa Kuwa Msingi wa Mafanikio kwa Wanafunzi Songea
- Gongo Lita 4.5 Yampeleka Jela, Afungwa Miaka 3
- Fursa za Kiuchumi, Uzalendo: Njia Muhimu kwa Maendeleo ya Vijana Tanzania
- Dhana ya Makundi Sogozi, Taratibu zake na Wahusika Wake katika Jamii
about
Category: Uncategorized
-
Na Mwandishi Wetu, Ruvuma Mahakama ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imemhukumu kijana mmoja mwenye umri wa miaka 20, James Hashimu Chingwaru, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumbaka bibi mwenye umri wa miaka 75. Hukumu hiyo ilisomwa tarehe 16 Machi 2026 na Hakimu Mkazi Mfawidhi, F.M. Philip, katika…
-
Na Mwandishi Wetu, Nachingwea Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI kinachohusisha wilaya za Nachingwea, Ruangwa na Liwale kimefanya kikao na wadau mbalimbali wa kampuni za usafirishaji ikiwa ni maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa mazao wa mwaka 2026/2027. Kikao hicho kilifanyika hivi karibuni katika ofisi za RUNALI zilizopo wilayani Nachingwea, ambapo viongozi wa chama hicho na…
-
Na Mwandishi Wetu, Nachingwea – Lindi Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea imetoa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, sambamba na kukabidhi vifaa mbalimbali ikiwemo matrekta, maguta, magari madogo ya mizigo na pikipiki kwa wanufaika wa mpango huo. Makabidhiano hayo yaliongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nachingwea,…
-
Na Mwandishi Wetu Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, watumishi wanawake wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wametoa msaada wa vitu, mahitaji na vifaa mballimbali kwa watoto wa Kituo cha kulea watoto yatima na waliofanyiwa ukatili cha Shalom kilichopo Kidenge B, Kata ya Msangani, Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mkoani Pwani.…
-
Na Cartace Ngajiro, Tanga Katika kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2026 watumishi wanawake wa Bandari ya Tanga waliungana na wafanyakazi wanawake wa kutwa wa bandari hiyo kufanya matendo ya huruma. Wanawake hao wametoa msaada wa mashine za kusaidia upumuaji aina ya “C- PAP Bubble Neonates, Oxygen Flowmeter” pamoja na vifaa mbalimbali katika Hospitali…
-
Na Mwandishi wetu,Nachingwea-Lindi Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Mohamed Hassan Moyo, ameipongeza Kamati ya Lishe ya Wilaya pamoja na Maafisa Lishe kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa masuala ya lishe wilayani humo. Moyo alitoa pongezi hizo jana wakati wa kikao cha tathmini ya Mkataba wa Lishe kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026.…
-
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nzuguni iliyopo jijini Dodoma wamepata fursa ya kujifunza na kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na Chuo cha Serikali za Mitaa. Maelezo nae limu hiyo waliipata jana baada ya kutembelea banda la maonyesho la chuo hicho katika maadhimisho ya siku 100 za mafanikio ya serikali ya Rais wa…
-
Na Cosmas Msuha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, ametembelea Banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) wakati wa Maonesho ya Mafanikio ya Siku 100 za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Maonesho hayo yalifanyika jana, katika Uwanja wa Nyerere Square jijini Dodoma yakibeba kaulimbiu “Kero yako,…
-
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Rukwa, Jacqueline Mzindakaya akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari kuhusu utekelezaji wa bima ya afya kwa wote. Na Cosmas Msuha Serikali imepongezwa kwa kuendelea kutekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, hatua inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma za afya bila kujali uwezo wake wa kifedha. Pongezi…
-
Na Mwandishi Wetu Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Ruvuma (TPF–NET) umeendelea kuonyesha moyo wa kujali jamii baada ya kutembelea na kutoa msaada kwa watoto wenye mahitaji katika Kituo cha kulelea watoto yatima cha Mfaranyaki, kilichopo Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma. Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa TPF–NET Mkoa wa Ruvuma, Mrakibu wa Polisi (SP)…