Category: Uncategorized

  • Na Vincent Mpepo, (Kwa msaada wa mtandao). Makundi ya WhatsApp na Telegramu katika taasisi za kidini, kama makanisa na jumuiya za waumini, yamekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kiroho na kijamii katika ulimwengu wa leo wa teknolojia. Kupitia makundi haya, waumini hupata nafasi ya kuwasiliana kwa haraka, kushirikishana taarifa muhimu na kuimarisha mshikamano wa kiimani…

  • Na Mwandishi Wetu, Pwani Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia kutoka Mkoa wa Pwani, wakiongozwa na Sajini Taji Wandwi Patrick, wametoa msaada kwa watoto wanaolelewa katika Kituo cha kulea wahitaji cha Buloma kilichopo Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani. Tukio hilo limefanyika leo ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa matendo ya huruma kwa jamii, hususan…

  • Na Vincent Mpepo Makundi sogozi ya mitandao ya kijamii kama WhatsApp, Telegramu ni matokeo ya maendeleo ya sayansi, teknolojia ya habari na mawasiliano na yamekuwa ni njia rahisi na yenye nguvu ya kuwasiliana na kushirikiana. Ikumbukwe kuwa matumizi ya makundi haya huwa na taratibu zinazoongoza uendeshaji wake na wakati mwingine yanapaswa kuwekewa vigezo au masharti…

  • Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Ilala, Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SSP) Salum Morimori, amewataka wamiliki wa magari ya kusafirisha wanafunzi kuhakikisha wanaajiri madereva wenye sifa stahiki ili kuimarisha usalama wa watoto barabarani. Akizungumza hivi karibuni katika viwanja vya Shule ya Msingi Olimpio wakati wa zoezi la…

  • Na Cosmas Msuha Serikali imezindua mradi maalum wa kuboresha huduma za dharura na usalama barabarani  katika jiji la Dar es salaam kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kutoka nchini Japan wenye lengo la kupunguza madhara kwa wahanga wa ajali za barabarani. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa huduma hizo jana jijini Dar es salaam, Mganga…

  • Na Mwandishi Wetu, Ruvuma Mahakama ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma imemhukumu kijana mmoja mwenye umri wa miaka 20, James Hashimu Chingwaru, kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumbaka bibi mwenye umri wa miaka 75. Hukumu hiyo ilisomwa tarehe 16 Machi 2026 na Hakimu Mkazi Mfawidhi, F.M. Philip, katika…

  • Na Mwandishi Wetu, Nachingwea Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI kinachohusisha wilaya za Nachingwea, Ruangwa na Liwale kimefanya kikao na wadau mbalimbali wa kampuni za usafirishaji ikiwa ni maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa mazao wa mwaka 2026/2027. Kikao hicho kilifanyika hivi karibuni katika ofisi za RUNALI zilizopo wilayani Nachingwea, ambapo viongozi wa chama hicho na…

  • Na Mwandishi Wetu, Nachingwea – Lindi Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea imetoa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, sambamba na kukabidhi vifaa mbalimbali ikiwemo matrekta, maguta, magari madogo ya mizigo na pikipiki kwa wanufaika wa mpango huo. Makabidhiano hayo yaliongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nachingwea,…

  • Na Mwandishi Wetu Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, watumishi wanawake wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) wametoa msaada wa vitu, mahitaji na vifaa mballimbali kwa watoto wa Kituo cha kulea watoto yatima na waliofanyiwa ukatili cha Shalom kilichopo Kidenge B, Kata ya Msangani, Halmashauri ya Mji wa Kibaha, mkoani Pwani.…