Kusini Kwetu
Habari za ndani na nje nchi
recent posts
- Tanzania Yaunga Mkono Kuimarisha Ushirikiano wa Kibunge kupitia NAM-PN
- Nidhamu Yatajwa Kuwa Msingi wa Mafanikio kwa Wanafunzi Songea
- Gongo Lita 4.5 Yampeleka Jela, Afungwa Miaka 3
- Fursa za Kiuchumi, Uzalendo: Njia Muhimu kwa Maendeleo ya Vijana Tanzania
- Dhana ya Makundi Sogozi, Taratibu zake na Wahusika Wake katika Jamii
about
Category: Uncategorized
-
Na Cosmas Msuha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU Mkoani Rukwa imefanikiwa kudhibiti vitendo vya rushwa katika miradi ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.7 kwa kipindi cha Oktoba hadi Disemba mwaka 2025. Mkuu waTAKUKURU Mkoa wa Rukwa, Mzalendo Widege aliyasema hayo katika taarifa yake kwa umma ambapo inaonesha kwa kipindi cha…
-
Na Cosmas Msuha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Balozi Dkt. Bashiru Ally amefanya ziara mkoani Geita na kugagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya Soko la Kimataifa Samaki la Chato na kumtaka mkandarasi kukamilisha ujenzi wa mtambo wa kukaushia dagaa kabla ya mwezi April mwaka huu. Dkt. Bashiru alitoa maagizo hayo Februari 28, 2026 baada…
-
Na Mwandishi Wetu, Nachingwea – Lindi Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Mohamed Hassan Moyo ameongoza zoezi la ugawaji wa miche zaidi ya elfu sabini ya mikorosho kwa wananchi, ikiwa ni juhudi za kuongeza uzalishaji wa zao la korosho wilayani humo. Akizungumza wakati wa zoezi hilo tarehe 23/02/2026, Moyo alisema serikali imeamua kuwapatia wakulima miche hiyo…
-
Na Vincent Mpepo Waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Mtaa wa Kwembe, wameungana na watu wengine duniani kuadhimisha Siku ya Wapendanao kwa namna ya kipekee, ambapo wanandoa walipatiwa mafunzo na uzoefu mbalimbali kama njia ya kukumbushana wajibu na haki zao katika ndoa taasisi inayotajwa kuwa msingi wa familia, jamii na taifa kwa…
-
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Katika mwendelezo wa utoaji wa elimu kwa umma, Jeshi la polisi limeendelea na kazi hiyo ambapo jana, Mratibu wa Program ya Usalama Wetu Kwanza Wilaya ya Kati na Kariakoo Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (Insp) Martin Shila alifika katika Shule ya Msingi Olympio Iliyopo Upanga Dar es salaam na kuzungumza…
-
Na Mwandishi Wetu, Dar es salaam Mkuu wa Polisi Jamii Wilaya ya Kariakoo Mrakibu wa Polisi (SP) Rosemary Kitwara amewataka wananchi kujiepusha na taarifa za upotoshaji zinazotolewa na watu mbalimbali wasio na mamlaka ya kutoa taarifa kwa jamii. SP Kitwara aliyasema hayo jana wakati wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Kariakoo Dar es salaam ambapo amewaasa…
-
Na Issa Mwadangala Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe limetoa taarifa ya matukio mawili ambapo katika tukio moja limeripoti kifo cha Feriki Kareai (54) Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Lukululu Wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe, amabaye alikutwa amefariki dunia huku mwili wake ukiwa umefukiwa na kifusi pembeni mwa Mto Itemba. Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la…