Kusini Kwetu
Habari za ndani na nje nchi
recent posts
- TAKUKURU Kuendelea Kufuatilia, Kuthibiti Matumizi Fedha za Miradi ya Serikali
- BARIKIWA NA NYIMBO ZA KWARESMA
- Kukamilika Soko la Samaki Kutaibua Fursa za Uchumi, Ajira kwa Wananchi
- DC Moyo Agawa Miche ya Mikorosho kwa Wakulima Nachingwea
- Mt. Kizito Makuburi – Buriani Baba Pengo (Official Music Video)
about
Category: Uncategorized
-
Na Damas Kalembwe Mkuu wa Ushirikishwaji Jamii wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni, ACP Ally S. Wendo, akimwakilisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, SACP Mtatiro Kitinkwi, ameongoza kikao kazi na Kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Wilaya ya Kinondoni (USHITA), kilichofanyika katika ukumbi wa Club 361, Mwenge jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika kikao…
-
Na Vincent Mpepo Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wametakiwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuboresha utoaji wa huduma na kukuza mapato ya chuo hicho. Makamu Mkuu wa Chuo, Profesa Alex Makulilo, alitoa wito huo jana katika hafla ya uzinduzi wa gari jipya la ofisi yake iliyofanyika Kinondoni, jijini Dar es Salaam.…
-
Na Vincent Mpepo, Songea Wataalamu wa afya wa Zahanati ya Kijiji cha Mlete iliyopo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wamepongezwa kwa moyo wao wa kujitoa na kujituma katika kuhudumia wagonjwa. Hayo yamebainishwa na ndugu wakiwemo watoto wa marehemu Amalia Chilongo wakati wa ibada ya mazishi yake jana huku ikibainika wazi kuwa watumishi wa Zahanati hiyo…
-
Na Vincent Mpepo, Mtwara Wanandoa katika jamii wametakiwa kuishi kwa upendo, kusameheana na kuvumilana kwa kuwa kila mwanadamu ana udhaifu wake na hakuna mkamilifu. Wito huo ulitolewa jana na Paroko wa Parokia ya Yesu Kristo Mkombozi – Magomeni, Jimbo Katoliki la Mtwara, Padre Silvanus Chikuyu wakati wa mahubiri katika ibada ya ndoa kati ya Edgar…
-
Na Damasi Kalembwe-Dar es Salaam Shule ya Sekondari Saranga iliyopo Mtaa wa Matangini, Kata ya Saranga, imefanya mahafali ya kuhitimu Kidato cha Nne ambapo pamoja na sherehe hizo, wanafunzi na wazazi walipata elimu ya ushirikishwaji jamii kutoka Jeshi la Polisi. Katika mahafali hayo, Polisi wa Kata ya Saranga Insp. Elias na Polisi wa Kata ya…
-
Na Vincent Mpepo, Karatu Wakristo wamekumbushwa faida na umuhimu wa kumtolea Mungu kwa uaminifu sadaka mbalimbali hususani fungu la kumi. Ukumbusho huo umetolewa na Mwalimu wa neno la Mungu, Tumsifu Lema katika mahubiri wakati wa ibada ya kwanza katika ibada Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) leo, katika Usharika wa Karatu Mjini, Dayosisi ya Kaskazini,…